Hongereni na Majukumu wananzengo
Ni kisa ambacho nimekikumbuka baada ya mwanamke huyo kunijualia hali jioni hii kwa sms nikaona si vibaya nikiwamegea kidogo story hii.
Kipindi cha nyuma kidogo(2013)wakati nimeamua kuchomoka kwa wazazi na kuanza kujitegemea nilibahatika kupata chumba kwenye nyumba moja ambayo ilikuwa ni ya familia ya mke na mume na watoto watano watoto wakubwa walikuwa wapo masomoni shule ya bweni, lakini wadogo wawili walikuwa wakisoma shule ya kutwa
Kwakuwa nilikuwa kijana mchangamfu na niliyejali hata madogo wa pale nilipendwa mno na ile familia kiasi cha kuwekwa hata kwenye hesabu ya chakula yaani ikawa kama nimetoka nyumbani halafu nipepanga tena nyumbani.
Ajabu ni kuwa tangu nimefika pale sikuwa nimefanikiwa kumuona father house niliambiwa tu mzee yupo nje ya... kikazi
Basi mama yule tukazoeana sana mpaka wakati mwingine kupiga soga za mahusiano yaliyowahi kupita,aise kumbe shetani alikuwa karibu kuliko mawazo yetu basi.
Siku moja katika story mbili tatu akasema unajua kitambi kina mkera sana na amejaribu dawa nyingi kukitoa ila hazijamsadia.
Kwakweli ushauri niliompa ni aanze mazoezi ya kukata tumbo akauliza ndio yakoje basi nikamueleza (lala chali then weka mikono kichwani halafu unajiinua)kutokana na uzito kila alipojaribu kujinyanyua ilinyanyuka miguu ikanibidi nikae juu ya miguu yake kumpa saport.
Sikuelewa nini kilitokea na mazoezi yaliishia wapi ila (nikala tunda kimasikhara kabisa )mwisho kila mtu alijisikia tabu na kujilaumu kwa tendo lile ila ikawa ndio imeshaliwa hiyo.
Basi tulivunga kama siku mbili tatu ila kwakweli utamu utamu tu tukashindwa kabisa kujizuia
Mambo yakawa hivyo yaani bimdashi yule aliyaweza kweli kweli ni fundi haswa yaani nikasahau kama naiba na mwenyewe yupo, nikanogewa haswa na akajaa moyoni
Basi siku zikapita majira yakasogea mwenye nyumba akarudi!!!!!bhana
Aise usiku ule sikulala moyo uliniuma niliona naonewa yaani nikifumba macho naona jamaa anavyojikadiria.
Kwa mara ya kwanza nikatoa chozi kwa maumivu ya mapenzi,yaani najaribu kuiambia akiri wewe sio wako mwenyewe ndio karudi kwanza ulikuwa unafanya makosa mwenyewe akijua utakufa lakini wapi moyo hauelewi unauma tu.
Nilikula ila nikakonda nikaanza kuwa mlevi viroba mixer fegi yaani ni vururu valangati.
Bimdashi nae akaniambia shika hela nenda kapange sehemu nyingine maana ninapokuona najikuta namchukia mume wangu maana tangu amefika nikama ananibaka yaani sina hisia nae nakuwa mkavu sasa nitakufa kwa michubuko.
Mwisho nikaona ni heri nisepe maana mzee alianza kufanya uchunguzi wa kimya kimya kutokana na mabadiliko ya mkewe..
Siku zimesonga moyo ulipona maisha yakasonga.
N.b(Hakuwa mwanamke wangu wa kwanza ni kama yeye wa 46 au47)na nilikuwa mmoja ya watu wanaoshangaa mtu kulia kwa ajili ya mapenzi. Niliponasa kwenye18 za mapenzi nikatengua kauli
Mapenzi yanaumiza sana hasa kumpoteza uliyempenda kweli unaweza kuplan mauaji hivi hivi.