VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,140
- 18,004
Ni dhahiri sasa Mahakama,kama Mhimili wa Kutoa Haki Tanzania,imechoka kutumiwa na Serikali na chama tawala kukandamiza demokrasia nchini Tanzania.Imechoka kuwa kichaka cha hujuma juu ya demokrasia. Mahakama imechoka kuwa na Wabunge wa Mahakama na vimbelembele-makada wa kupinga hata visivyowahusu. Sasa Mahakama imeamka.
Kilichotokea kwa Yamsebo-kule Sumbawanga,Mnyika-Ubungo,Lema-Arusha Mjini,na kwa Madiwani wa Mwanza na Arusha ni ushahidi tosha. Kama CCM na Serikali yake haijui,kesi hizi zinaipaisha CHADEMA kwenda juu zaidi na kuelekea Ikulu 2015. Hebu vuta picha ya nchi hii leo baada ya Ushindi wa Lema wa CHADEMA!
Vuta picha ya Arusha na mikoa mingine atakapopita Lema kama Mbunge wa Arusha mjini.Nchi itatikisika kwa furaha na kukubalika kwa CHADEMA. CCM na vibaraka wake wanafanya kosa kubwa. Wanaifanya Mahakama iipaishe CHADEMA juu na juu zaidi kiumarufu.
Sasa wale wa M7 mtulie. CHADEMA ijipange kimkakati na kihoja luelekea Ikulu 2015.Njia imefunguka. Njia nyeupe. Eee Mwenyezi Mungu niongeze umri wa kuishi niione siku ya ukombozi wa nchi hii toka kwa hawa waliochoka kutuongoza CCM na vibaraka wao. Nakuomba sana Mwenyezi Mungu.Amina.
Kilichotokea kwa Yamsebo-kule Sumbawanga,Mnyika-Ubungo,Lema-Arusha Mjini,na kwa Madiwani wa Mwanza na Arusha ni ushahidi tosha. Kama CCM na Serikali yake haijui,kesi hizi zinaipaisha CHADEMA kwenda juu zaidi na kuelekea Ikulu 2015. Hebu vuta picha ya nchi hii leo baada ya Ushindi wa Lema wa CHADEMA!
Vuta picha ya Arusha na mikoa mingine atakapopita Lema kama Mbunge wa Arusha mjini.Nchi itatikisika kwa furaha na kukubalika kwa CHADEMA. CCM na vibaraka wake wanafanya kosa kubwa. Wanaifanya Mahakama iipaishe CHADEMA juu na juu zaidi kiumarufu.
Sasa wale wa M7 mtulie. CHADEMA ijipange kimkakati na kihoja luelekea Ikulu 2015.Njia imefunguka. Njia nyeupe. Eee Mwenyezi Mungu niongeze umri wa kuishi niione siku ya ukombozi wa nchi hii toka kwa hawa waliochoka kutuongoza CCM na vibaraka wao. Nakuomba sana Mwenyezi Mungu.Amina.