Mahakama ya Kenya yazuia kwa muda kupelekwa kwa polisi Haiti

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,502
9,282
Mahakama moja ya Nairobi nchini Kenya imezuia kwa muda mpango wa serikali wa kutuma maafisa wa polisi nchini Haiti kujiunga na ujumbe unaoungwa mkono na Umoja wa Mataifa unaolenga kurejesha hali ya utulivu nchini humo

Mahakama hiyo ilitoa zuio hilo la muda katika kesi iliyowasilishwa na mwanasiasa wa upinzani Ekuru Aukot, ambaye alidai kupelekwa kwa maafisa hao wa polisi nchini Haiti ni kinyume cha katiba kwani hakuambatani na sheria wala mkataba wowote.

Aukot, wakili ambaye alisaidia kuandika katiba ya Kenya ya mwaka 2010 iliyofanyiwa marekebisho, amesema kuwa Kenya inataka kupeleka maafisa wake nje ya nchi wakati ambapo imeshindwa kukabiliana na tatizo la ukosefu wa usalama ndani ya mipaka yake.

Nakala ya uamuzi huo ilioonekana na shirika la habari la AFP, inasema kuwa agizo hilo linazuia kwa muda kusafirishwa kwa maafisa hao wa polisi nchini Haiti ama taifa lingine lolote hadi Oktoba 24, 2023.


DW Swahili
 
Mahakama moja ya Nairobi nchini Kenya imezuia kwa muda mpango wa serikali wa kutuma maafisa wa polisi nchini Haiti kujiunga na ujumbe unaoungwa mkono na Umoja wa Mataifa unaolenga kurejesha hali ya utulivu nchini humo

Mahakama hiyo ilitoa zuio hilo la muda katika kesi iliyowasilishwa na mwanasiasa wa upinzani Ekuru Aukot, ambaye alidai kupelekwa kwa maafisa hao wa polisi nchini Haiti ni kinyume cha katiba kwani hakuambatani na sheria wala mkataba wowote.

Aukot, wakili ambaye alisaidia kuandika katiba ya Kenya ya mwaka 2010 iliyofanyiwa marekebisho, amesema kuwa Kenya inataka kupeleka maafisa wake nje ya nchi wakati ambapo imeshindwa kukabiliana na tatizo la ukosefu wa usalama ndani ya mipaka yake.

Nakala ya uamuzi huo ilioonekana na shirika la habari la AFP, inasema kuwa agizo hilo linazuia kwa muda kusafirishwa kwa maafisa hao wa polisi nchini Haiti ama taifa lingine lolote hadi Oktoba 24, 2023.


DW Swahili
Aisee!
 
Back
Top Bottom