Mahabusu ya magereza na mahabusu ya polisi wapi kuzuri?

Mahabusu ya magereza na mahabusu ya polisi wapi kuzuri?

Mugabe one

JF-Expert Member
Joined
Nov 15, 2016
Posts
2,327
Reaction score
1,684
Wanajf, let me declare that sijawahi ingia humo kote kote, Mungu anisaidie sana nisiingie huko!
Mliowahi ingia huko Na wenye ufahamu Halisi ni wapi kuna unafuu wa kutuliza akili?
Ninachokumbuka hapo ZAMANI kijijini kwetu kulikuwa askari mmoja alijurikana kwa jina la Magori akikamata watu wenye makosa madogo alikuwa anawapa adhabu kwenda kutafuta Kupe / papasi 10 Na kunguni 10 ili wawekwe humo mahabusu na mwisho wa adhabu yake.
Nasikia mahabusu ya magereza iko vizuri hakuna bughuza.
Je huko Magerezani wafungwa Na mahabusu hukaa Na kulala pamoja au kila kundi kivyao?
Kwa FIKIRA zangu nadhani askari magereza wana roho ya huruma kuliko askari wa majeshi mengine.
Nasikia kule kwenye magereza makubwa yenye watu wengi ndio hayana ustaarabu je ni sahihi?
Magereza wana silaha zao lakini kukiwa Na jambo lenye vurugu kwann waitwe wa Polisi FFU?
 
Wanajf, let me declare that sijawahi ingia humo kote kote, Mungu anisaidie sana nisiingie huko!
Mliowahi ingia huko Na wenye ufahamu Halisi ni wapi kuna unafuu wa kutuliza akili?
Kote hakuna unafuu ila mazingira ya selo za polisi kidogo si mazuri

Ninachokumbuka hapo ZAMANI kijijini kwetu kulikuwa askari mmoja alijurikana kwa jina la Magori akikamata watu wenye makosa madogo alikuwa anawapa adhabu kwenda kutafuta Kupe / papasi 10 Na kunguni 10 ili wawekwe humo mahabusu na mwisho wa adhabu yake.
Nasikia mahabusu ya magereza iko vizuri hakuna bughuza.
Kuna magereza maalumu kwa ajili ya mahabusu na mchanganyiko, mahabusu hafanyi kazi yoyote yeye ni mfalme mpaka mahakama itakavyoamua tofauti.

Selo za magereza ya kitanzania sio rafiki ziogope sana.

Je huko Magerezani wafungwa Na mahabusu hukaa Na kulala pamoja au kila kundi kivyao?
Soma hapo juu, yapo ya mahabusu peke yao na ni machache sana mengi ni mchanganyiko

Kwa FIKIRA zangu nadhani askari magereza wana roho ya huruma kuliko askari wa majeshi mengine.
hahaha kila mwana damu ana huruma.

Nasikia kule kwenye magereza makubwa yenye watu wengi ndio hayana ustaarabu je ni sahihi?
Sio yote

Magereza wana silaha zao lakini kukiwa Na jambo lenye vurugu kwann waitwe wa Polisi FFU?

si kweli.
Magereza wana FFU yao inaitwa KM ipo kwenye magereza yenye idadi kubwa ya wafungwa na hata magereza mengine ikitokea vurugu huimaliza wao wenyewe ni moja ya mambo waliyojifunza kiwira.

Mimi si askari mkubwa ila nakaufahamu tu
 
Ndio hawa ukimpiga pingu analia na kutaja maneno yote ya kwenye biblia! Imagine mtu anataka kutuliza akili chini ya askari wenye virungu saa 24/7
 
mkuu za polisi ni sero za muda mfupi,so unaweza imagine tu jinsi ambavyo zinawekwa.

magereza zina unafuu sababu ni sehemu ya maisha mtu anaishi hapo.
 
si kweli.
Magereza wana FFU yao inaitwa KM ipo kwenye magereza yenye idadi kubwa ya wafungwa na hata magereza mengine ikitokea vurugu huimaliza wao wenyewe ni moja ya mambo waliyojifunza kiwira.

Mimi si askari mkubwa ila nakaufahamu tu

KM kozi yao hufanyikia ukonga na kule Mvuti.
 
Wanajf, let me declare that sijawahi ingia humo kote kote, Mungu anisaidie sana nisiingie huko!
Mliowahi ingia huko Na wenye ufahamu Halisi ni wapi kuna unafuu wa kutuliza akili?
Ninachokumbuka hapo ZAMANI kijijini kwetu kulikuwa askari mmoja alijurikana kwa jina la Magori akikamata watu wenye makosa madogo alikuwa anawapa adhabu kwenda kutafuta Kupe / papasi 10 Na kunguni 10 ili wawekwe humo mahabusu na mwisho wa adhabu yake.
Nasikia mahabusu ya magereza iko vizuri hakuna bughuza.
Je huko Magerezani wafungwa Na mahabusu hukaa Na kulala pamoja au kila kundi kivyao?
Kwa FIKIRA zangu nadhani askari magereza wana roho ya huruma kuliko askari wa majeshi mengine.
Nasikia kule kwenye magereza makubwa yenye watu wengi ndio hayana ustaarabu je ni sahihi?
Magereza wana silaha zao lakini kukiwa Na jambo lenye vurugu kwann waitwe wa Polisi FFU?
Haroo mripokee hiri rimwizi rikarare Chooni .Moja ya kauli zenye kutia hofu kabisa ukifika polisi mbaya zaidi unapekuliwa huku unachezea na makofi ukilalamika unaambiwa wacha kuuriza makofi polisi.Usiombe ikawa ijumaa jioni loh Vibaka wamejaa mahabusu wengine wanamadonda yenye damu wananuka balaa ukiingia unakutana na wababe wa mahabusu wanaanza na kauli ya toka mlangoni unaziba hewa sasa nitoke mlangoni naingiaje Mara unapigwa Kofi la USO unavurugwa akili unaambiwa nenda chooni mbumbavu unatujazia mahabusu kwa vishauri vya kwa mjumbe.Hapo mahabusu unakutana na makundi ya vibaka ambao ni mahasimu Yaani kutoka mitaa miwili tofauti hapo ni ngumi makofi nje nje.Yaani acha kabisa habari ya mahabusu utakuta vidirisha vipo juu kweli kweli hewa ndogo.Nasema kila siku nikiwaona polisi Doria wanakuja upande wangu nabadili hadi njia maana kuna mwaka mpya mmoja ulinikuta mahabusu maana nilidakwa utafikiri panya road mpaka nafika mahabusu Niko nimechakaa.Safari nyingine kwenye maandamano ya siasa nilidakwa na wale jamaa wanavaaga vikofia vyekundu mbumbavu kabisa wale si binadamu kabisa mpaka Leo hili bega la kulia huwa naisi nimetwishwa nguzo ya umeme.
 
KM kozi yao hufanyikia ukonga na kule Mvuti.
Sijasema kozi za KM zinatolewa wapi na wapi mkuu, kila Askari lazima afundishwe namna ya kutuliza ghasia na hiki kinafanyikaga kwenye kozi za awali za maafisa wa magereza Kiwira.
 
Mwaka jana, nilikorofishana na trafiki moja hivi kumbe siku hiyo bos wao yuko hapo na wako kwenye opereshen kagua kagua. Huyo bos akatoa amri nipelekwe kituoni. Bila mjadala wakaninyaganya cm na kuswekwa lupango. Ndio ilikuwa mara yangu ya kwanza kuingia sero ya polisi alafu ilikuwa jioni nikadhani ningewapa hela alafu tumalizane. Kumbe walikuwa na mipango ya kunipeleka mahakamani.... Sero la polisi ni mbaya sana kulala sakavu tupu alafu choo likiwapumulia mbaya. Asubuhi tukakurupuliwa ndo tukakabidhiwa CM na vitu vyetu alafu tupande mahakamani. Nikapiga cm hom kwa msaada nikiwaelekeza tukutane mahakama ya wilaya. Tulipofika mahakamani ilivyokuwa nuksi hakimu hakuwepo bali kuna hakimu mgeni akasoma tu mashtaka alafu unapanda karandinga la magereza. Huko nako ni mara yangu ya kwanza kufika magereza. Tukaingizwa magereza sa 11 jioni nilikuwa na njaa kali sana afu siku ya pili sikuoga wala kupiga mswaki. Vueni nguo zote!! Akaagiza askari magereza tukavua tukabakiwa uchi wa mnyama. Hapo ndo nilicheka mbaya. Kuna machinga anashanga na mahirizi kiunoni, alafu kavaa viatu ndani yake amejaza matambara mengi sana........ Tukaingizwa uani kwa kichura na mizigo yetu tukaacha hapo alafu tukaingizwa ndani. Nikashangaa humo ni pasafi na kuna magodoro. Tukapewa maji ya kunywa, kunywa maji ni lazima kule ndani hata km huna kiu.pagumu kidogo ni pale unapokaririshwa sheria za jela. Tukalala, asubuhi baada ya uji tukakaririshwa zile sheria tena. Baada hapo sasa nikukaa uani na kipiga stori hadi sasa6:30 kwa msosi alafu saa 9;30 mnaingizwa ndani kwakuhesabiwa kila siku. Kadiri siku inavyoeenda jela inakuwa shwari. Mi nilikaa siku 3 tu mle nikatolewa. Wafungwa na mahabusu hawakai pamoja. Kuna watu kule ndani wanavitambi tayari na miaka ya kutosha na wanavaa vizuri km vile wako nyumbani tu
 
Brooooo usiandike kitu usichokijua uliza kwanza wapi zilitokea vurugu magereza waliita FFU....
Wanajf, let me declare that sijawahi ingia humo kote kote, Mungu anisaidie sana nisiingie huko!
Mliowahi ingia huko Na wenye ufahamu Halisi ni wapi kuna unafuu wa kutuliza akili?
Ninachokumbuka hapo ZAMANI kijijini kwetu kulikuwa askari mmoja alijurikana kwa jina la Magori akikamata watu wenye makosa madogo alikuwa anawapa adhabu kwenda kutafuta Kupe / papasi 10 Na kunguni 10 ili wawekwe humo mahabusu na mwisho wa adhabu yake.
Nasikia mahabusu ya magereza iko vizuri hakuna bughuza.
Je huko Magerezani wafungwa Na mahabusu hukaa Na kulala pamoja au kila kundi kivyao?
Kwa FIKIRA zangu nadhani askari magereza wana roho ya huruma kuliko askari wa majeshi mengine.
Nasikia kule kwenye magereza makubwa yenye watu wengi ndio hayana ustaarabu je ni sahihi?
Magereza wana silaha zao lakini kukiwa Na jambo lenye vurugu kwann waitwe wa Polisi FFU?
 
Back
Top Bottom