Magufuli: Tujadili uwezo wake

Hivi Lowassa na Magufuli nani anauwezo wa kidiplomasia?

Sio huyu Lowassa aliyekurupuka na kutangaza vita na Malawi wakati jukumu sio lake na hakuna viashiria vyovyote vya kivita.?
 
Ni mjivuni na mwenye kiburi cha kishamba.Bila kusahau kupenda sifa ndio sifa yake kuu.


Naomba maelezo kidogo.
Kiburi cha Kishamba kivipi?
Mjivuni kivipi?
Kupenda sifa zipi? nzuri au mbaya?
 
Magufuli sifa yake kubwa ni UKUTUPUKAJI kwenye uraisi hatufai hata kidogo

Ni kweli Magufuli na Lowasa wote wanamaamuzi ya haraka bila kuangalia hatari ya mbele.

Kwamfano. Magufuli alishawahi kuvunja mikataba ambayo serikari iliingia hasara kulipa.

Lowasa alisababisha hatari ya kutokea vita dhidi ya Malawi pale alipo kurupuka na kutoa kauli iliyoashiria kutangaza vita.
 
Sifa kubwa ya magufuli, Hapendi uzembe. Pia anataka kila kitu kifanyike kwa wakati
 

Kwanini hafai? hujaeleza hoja yeyote.
Nani anafaa?
Na kwa nini anafaa?
 

Nmekupata ktka hoja yakwanza, ya kuhitaj mshauri.

Naomba ufafanizi hapo kwnye vyama vya siasa na democrasia ya vyama vingi
 
Last edited by a moderator:
yaani huyo mgombea ni chenga hana cha kumjadili; kaangushiwa jumba bovu bila kujijuwa atajibeba.
 
Hivi Lowassa na Magufuli nani anauwezo wa kidiplomasia?

Sio huyu Lowassa aliyekurupuka na kutangaza vita na Malawi wakati jukumu sio lake na hakuna viashiria vyovyote vya kivita.?

Lowassa naye tutamjadili , hiyo itakuwa topics nyengine...topic hii inamhusu magufuli. hivyo lete fikta zako vipi unamuona Magufuli , bila ya kutukana jadili constructively😛ray2:
 
Lowassa naye tutamjadili , hiyo itakuwa topics nyengine...topic hii inamhusu magufuli. hivyo lete fikta zako vipi unamuona Magufuli , bila ya kutukana jadili constructively😛ray2:
Huwezi kumjadili Magufuli bila kumtaja Lowassa, maana ndio mpinzani wake mkubwa.

Na ikifahamika Magufuli haifai nani tumpe? Bila shaka utasema Lowassa.

Huwezi kumhubiri Mungu bila kumtaja shetani.!
 
Hivi Lowassa na Magufuli nani anauwezo wa kidiplomasia?

Sio huyu Lowassa aliyekurupuka na kutangaza vita na Malawi wakati jukumu sio lake na hakuna viashiria vyovyote vya kivita.?

Malawi na Tanzania walipigana lini?.
 

Kama unafikiri Magufuli atakuwa na muda huo wa kushauriana na wenzake umechelewa,kwa Magufuli ni kazi tu hayo mengine ni upuuzi.
 
mwahiyo wewe ulitaka lowassa aanze kuchekacheka kwenye maswala ya siliasi huoni alivyo ongea vile saizi wamalawi wametulia
 
Na yule mgonjwa atatupa hasara zaid maana nahofu kila mara itabid awe anaenda kutibiwa.. Ni mtazamo tu
 
mwahiyo wewe ulitaka lowassa aanze kuchekacheka kwenye maswala ya siliasi huoni alivyo ongea vile saizi wamalawi wametulia

Lile lilikua ni swala la kidiplomasia.
Na mpaka sasa kesi haijaisha lkn inaendeshwa kidiplomasi na sio kivita kama alivyotaka Lowasa
 
Nmekupata ktka hoja yakwanza, ya kuhitaj mshauri.

Naomba ufafanizi hapo kwnye vyama vya siasa na democrasia ya vyama vingi

..fuatilia hotuba zake mbalimbali na jinsi anavyovipiga vijembe vyama vya upinzani.

..kwa muda mrefu amekuwa akipiga vijembe vyama vya upinzania, haswa suala la maandamano.

..hali hiyo inatilia shaka kama ana-appreciate umuhimu wa vyama vya upinzani. zaidi kama anaamini ktk maandamano kama njia ya watawaliwa kupeleka ujumbe kwa watawala--uwe mzuri au mbaya.

..pia kama ameshindwa kutofautisha mabadiliko yaliyotokea Libya, Iraq, Zaire, na hiki kinachoendelea hapa Tanzania, basi huenda huyu akawa mtu hatari sana kwa demokrasia yetu ya vyama vingi.

cc crabat
 
Last edited by a moderator:

nmekupata
 
Last edited by a moderator:
Barabara nyingi quality mbovu sana
mitaro ya pembeni haifunikwi

aliahidi kuondoa foleni ndani ya miezi sita ya Dar..
kivuko cha mv daresalaam kibovu ni hasara tupu..
 

Hili la Libya la kushangaza kidogo...sasa sijui kwa makusudi kapotosha au haelewi masuala ya kimataifa na sio mfuatiliaji wa mambo ya nje...
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…