Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,172
Magufuli akanusha kubomoa ofisi ya RC Dar
na Nuru Yanga
WIZARA ya Ujenzi nchini imekanusha taarifa zilizoandikwa na baadhi ya vyombo vya habari hivi karibuni kuwa Waziri John Magufuli ameagiza kubomolewa kwa jengo la ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Dar es Salaam. Tamko hilo lilitolewa na Kaimu Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Balozi Herbert Mrango, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam.
Aidha, alisema Waziri Magufuli alifanya ziara Januari 31 mwaka huu kukagua utekelezaji wa ujenzi wa barabara zinazojengwa jijini Dar es Salaam kama sehemu ya mpango wa serikali kupunguza msongamano wa magari.
Pia alisema katika ziara hiyo Waziri Magufuli alitoa agizo la kubomolewa jengo la TANROADS ambalo limo ndani ya hifadhi ya barabara kwa mujibu wa sheria namba 13 ya mwaka 2007 na si kubomolewa kwa jengo la ofisi ya mkuu wa mkoa kama ilivyoripotiwa.
Alisema katika hilo, Magufuli aliwataka watendaji wa TANROADS kutekeleza agizo hilo ndani ya siku tano ili kutoa nafasi kwa kituo cha daladala kilichopo maeneo ya Ubungo.
na Nuru Yanga
Aidha, alisema Waziri Magufuli alifanya ziara Januari 31 mwaka huu kukagua utekelezaji wa ujenzi wa barabara zinazojengwa jijini Dar es Salaam kama sehemu ya mpango wa serikali kupunguza msongamano wa magari.
Pia alisema katika ziara hiyo Waziri Magufuli alitoa agizo la kubomolewa jengo la TANROADS ambalo limo ndani ya hifadhi ya barabara kwa mujibu wa sheria namba 13 ya mwaka 2007 na si kubomolewa kwa jengo la ofisi ya mkuu wa mkoa kama ilivyoripotiwa.
Alisema katika hilo, Magufuli aliwataka watendaji wa TANROADS kutekeleza agizo hilo ndani ya siku tano ili kutoa nafasi kwa kituo cha daladala kilichopo maeneo ya Ubungo.