Magufuli na ikulu

Magufuli na ikulu

kajisemea Mwapachu Maneja na Kiongozi. Jamaa kazoea Kukariri tu Ma Benzene na Hydrochloric acid. Pale hamna strategist; yaani presidential material
:majani7:
 
Walianza na maisha bora kila mtanzania tukaitikia ndio mzeeeee sasa wamekuja na watajenga barabara sita sita kutoka dar hadi chalinze tukajibu ndio mzeeeee , watajenga barabara. Za juu ( flyovers ) saba ndio mzeeeee . Yaani ni Kama michezo ya watoto !!!!! Hivi kweli ninyi mnatuweka sisi watanzania kundi gani ? Zile Airbus na meli alizoahidi basi wako ziko wapi ? Au ndio Yale malori ya kaka Rizi ? Na meno ya tembo unayouliza yamepitaje kwani mkurugenzi wa kampuni inayosafirisha si ndio amekukaribisha kilingeni ? Acha Trisha toto wewe, tumeamka na tumeashana.
 
Wewe ndio utakuwa kundi la aliowasema Mkapa, yaan mwizi na fisadi Lowassa ndio akukomboe?ndoto za mchana.Lowassa anaenda akiwa na maslahi yake na mafisadi wenzake ambao wameishatumia pesa nyingi sana kuutafuta urais huo,akifika huko ni kujilipa tu kama alivyojilipa Richmond.

Hivi alijilipa Richmond? Duuu
 
Hivi UKAWA wanafanyaje kuweze kuleta ukombozi wanaodai?[/QUOTE

Simple, ccm ikiwa chama kikuu cha upinzani ubadhirifu wa mali za umma utakuwa mdogo sana kwa kuwa wanafahamu mbinu zote walizotumia kufanya ufisadi, hawatakubali kuona viongozi wa serikali ya ukawa wanaanza kujineemesha kwa ufisadi, watapiga kelele kabla haujafanyika. Kodi zetu zitatumika inavyostahiki. Mishahara itaongezeka kwa kuwa pesa ya kulipa bila longolongo ipo, na miradi ya maendeleo itaongezeka, ajira pia.

Thamani ya shilingi itaongezeka kwa kuwa hatutategemea sana misaada kuendesha nchi yetu, mishahara itakutana. Kwa sasa wakishagawana kodi zetu wanatembeza bakuli nje ya nchi, no free lunch, wanazidi kudidimiza uchumi.

Tukirudisha sura zilezile kwenye uongozi baada ya miaka miwili wataanza kusema bil. 10 ni hela ya mboga, kwa mshahara upi? Baada ya miaka mitano watakuja na ahadi zingine kibao za uongo, ili waendelee kutuvuna. Tutakapohoji walichotufanyia tutaitwa wanywa gongo, sio viroba tena.

Je unafahamu kuwa asilimia 99 ya uchumi wa tanzania unamilikiwa na asilimia 1 ya watu?
Ukombozi utaletwa kwa kufanya asilimia 99 ya watanzania wanufaike na rasilimali za nchi yao, na ccm haiwezi kufanya hivyo, ingeshafanya. Danganya toto ni nyingi huku wanakula wao. Tutakufa tunadanganywa, tuamke, woga wetu ndio umaskini wetu.

Kwa kifupi ccm ikiwa chama kikuu cha upinzani ukombozi wa kweli wa wananchi utaanza kuonekana ndani ya miaka mitano, wanywa viroba kwa mawazo tutaanza kujua ladha ya mvinyo, sio mvinyo waujue wao tu.
 
Siasa haina marafiki wa kudumu au maadui wa kudumu. Kuhamia chama pinzani na kupewa madaraka ni mojawapo ya mikakati ya ushindi. Ni sawa na kununua mchezaji wa timu pinzani ili kuhakikisha ubingwa unapatikana.

Kumbe!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
magufuli anaweza hilo halina ubishi tena na huyu mtu atatuvusha

Kama alishindwa kuwavusha watu wa kigamboni tu ndo ataiweza nchi?
C ata waambia wanafunzi kama hamuwezi kujilipia ada rudini kijijini?
Unamuona he is wise enough to handle pressure?
 
UKAWA inaongozwa na viongozi WAPUMBAVU, sasa si bora tubakie na CCM yetu tu. Anayegombea UKAWA katoka CCM, mbaya zaidi ni mzee na afya inayumba na ni Fisadi. Sasa bora tumchague Magufuli, tuchape kazi, hapa kazi tu.

Baba yako akiwa mgonjwa ndo humueshimu tena? Ccm ni yaka na ukoo wako. Enough ts enough.
 
atazuiaje meno ya tembo wakati waliomteua ndio wapitisha?Ee Mungu fungua wtz wajielewe.
 
Me bado nasubiri zile ajira milioni moja kwa vijana
 
MUNGU tuonyeshe kiongozi bora na maneno ya watu wajukwaani ili nchi hii ya TANZANIA ipate maendeleo kiroho, kiuchumi, kielimu n.k
 
Josephave P. ameshangazwa na mambo mengi lakini hakushangazwa na biashara haramu ya madawa ya kulevya inayomaliza kizazi chetu hiki na kijacho. Kwa nini hakushangazwa na hili?
 
CCM B vipi maji mtayaweza na mitego tuliyowafurumishia wakati nyie mnakenua?
 
Kama alishindwa kuwavusha watu wa kigamboni tu ndo ataiweza nchi?
C ata waambia wanafunzi kama hamuwezi kujilipia ada rudini kijijini?
Unamuona he is wise enough to handle pressure?

Kwani daraja kigamboni umejenga wewe?
 
CCM B vipi maji mtayaweza na mitego tuliyowafurumishia wakati nyie mnakenua?
Mwaka huu ccm A mmepanic hamjui nani atafuatia kuwatoroka, jukwaani mnaporomosha matusi tu.
Na bado watatoka wengine.
 
Sasa tumpe nani,ukawa hawana mawazo mbadala maana waliomo ni walewale walokua ccm hakuna jipya hapo,bora tuendelee kutawaliwa na ccm
 
Kimsingi simkubali lowasa hata kidogo hata wale wanaomfuata wengi wao ni kutoka ukanda wao,lowasa hana vision pia hana mission kwa taifa letu kinachombeba ni umaarufu wa pesa,na vijana wengi kukosa imani na ccm,kiukweli jamaa hana uwezo wowote kiongozi,laiti slaa angekuwepo angelamba kura yangu kwa kosa walilofanya chdm kumweka fisadi lowas inadhihirisha kuwa wao lengo ni kuchukua dola lakin hawana misingi yoyote ya kimaadili,sasa uwadilifu wao waliokua wanasema upo wapi tuendelee kuiamini chadm?rudi nyuma kijana mwenzangu chagua magufuli uwezo anao akiboronga tumdilete miaka 5,
 
Sasa tumpe nani,ukawa hawana mawazo mbadala maana waliomo ni walewale walokua ccm hakuna jipya hapo,bora tuendelee kutawaliwa na ccm
Wanazungukwa na watu wapya, kuna ambayo hawakuweza kufanya wakiwa ccm.
 
Back
Top Bottom