Magufuli na data za uongo

bupepe

Senior Member
Joined
Jun 22, 2015
Posts
114
Reaction score
71
Alichonishangaza Magufuli na nimeanza kuamini hata data alizokuwa anatupa ni za uwongo. Anasema kwa mara ya kwanza Tanzania na duniani itaweka historia ya kuwa na makamu wa rais wa kwanza mwanamke. "Ni uongo uliokithiri"

Correction
Mwaka 1994 mpaka 2003 Uganda walikuwa na makamu wa Rais Madam Specioza Nainda Wangila.

Hadi sasa Zambia wana makamu wa rais wa kike madam Inonge Wina

So ukiwa muongo angalau angalia pa kudanganya

Tukutane Oktoba2015
 
Magufuli hana ajualo ndio mana alisema atawagawia walim laptop hlf nape akaja kukanusha.
 
CCM wamekuwa waongo na watu wa kutoa ahadi za uongo kwa miaka yote,ila watanzania walikuwa bado hawajapata mwamko kama sasa,KWASASA WATANZANIA HATUDANGANYWI TENA NA VIONGOZI WA CCM,sasa kama anadanganya hivyo je hizo laptop kwa walimu si ni uongo pia? KURA ZETU ZITAENDA KWA LOWASSA NA VIONGOZI WA UKAWA. Tumechoshwa na wizi na ufisadi wa CCM.
 
Huyu jamaa huwa anakariri sana, lkn uelewa wake ni mdogo. Alimeza kama alivyoandikiwa akatema kama kilivyo
 
Tunataka Key kwete (aina ya pombe huko kanda ya Ziwa) alete Meli Ziwa Nyasa kabla hajaanza kuomba kura za Magu.....Fulia Pombe.
 

Ccm wamezoea kukariri! Wanadhani kwamba watanzania wa leo ndio walewale wa siku zote wanaotawalika kwasababu hawana taarifa. Ki ukweli nawashangaa watanzania, hivi kura yako kweli unaipa ccm na magufuli? Kwakweli if you are programmed to fail you can never succeed by any means on earth!
 
Nimemsikia hata mimi kasema kwa mara ya kwanza duniani sio Tanzania, acha kubadili kauli za watu
 
Alitoa data za dagaa ziwa victoria, sijui anawafahamu dagaa huyu binaadamu!!!!????
 
Mzee in mwongo Wa data eti Bahari ya Hindi INA Samaki bilioni 2 ,234,000,000 huo in uongo mtupu atakuwa anawadanganya watanzania kwa data kuwa uchumi umepanda kwa asilimia 1,005 hafai
 
Alisema kwa Mara ya Kwanza Tanzania na dunia itajua. Tanzania haijawahi kuwa na Makamu mwanamke hivyo itakuwa ni historia itakayojulikana Tanzania na ulimwenguni.
Kama hujui matumizi ya lugha uliza uelekezwe.
Makamu wa rais mwanamke atatusaidia nini? Sidi tunataka mkate wetu wa kila siku sio mambo ya gender? Dunia ikishajua tuna makqm mwanamke ndio tutapata maisha bora kwa kila mtanzania?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…