Magufuli hii nimeipenda

italiwa hiyo tukaishiwa kupewa porojo kodi nyingi wanatukata, bandari zetu pekee zikiendeshwa vizuri sie umaskini tutakuwa tunaangalia BBC tu uko
 
Kwa Dar hapakuwa na haja ya kusumbua Watu tungemtafuta Mzee wa Maharambeee akapiga harambee moja takatifu tukamaliza kazi.
Aliwahi kuitwa Mwanza na Masheikh alipiga harambee malengo ilikuwa 250M ikapatikana 500 Million. JPM amtafutie kitengo cha Harambee
 
Kama kweli wako serious na Elimu yetu atunge sheria ya watoto wote wa viongozi wasome shule Za serikali
 
Sioni logic yoyote hapo.
Eti raisi anatoa M6 ya mshahara wake ili kuchangia ujenzi wa shule.
Kweli Tanzania ya Leo ndio tumefika hapo?
Namkumbuka Lowassa alivyoweza kuhamasisha shule za Kata na vyuo vikuu kujengwa na ndani ya miaka miwili tukaona shule na vyuo vikiota kama uyoga.
Hii nchi imegota na kinachotupumbaza ni hayo maigizo na Sikh hizo skip zikiisha ndio wadanganyika watafunguka macho na kupaza sauti "kwanini majirani zetu Kenya,Uganda,Burundi na Rwanda wametuacha kiuchumi" lakini It will be too late.

M6 x 12 x 5 = M360
Hapo ndio upige hesabu na uone ndani ya miaka 5 ya mpito tutajenga shule ngapi.

Tumechoka maigizo
 
Anatoa mara moja sh milioni 6 mbona unampigia kwa miaka mitano?
 
Kuna watu katikati uzi huu hawaitakii nchi yetu mema.
Raisi na serekali yake wametoa michango ya pesa kwa kusaidia maendeleo ya mkoa wa Dar
Nyie mnalaumu tu. Eti wanalala,kula na mambo mengi bure. Je wasinge zitowa hizo pesa? Kitugani kingebadilika.
Wametoa mifano ya kusaidia watu wa chini.
 
Kufanya hivyo sawa... kwa sababu wana misamaa ya kodi...
 
Namtafuta huyo anayewakata atujibie swali lililokosa majibu ya kuaminika la kiwango halisi cha mshahara wa rais wa Tanzania
 
ana lala bure,kula bure,anasomeshewa million 6 kwenye million 55 kwa mwezi sawa na tone la maji ktk bahari.
pia nani atahakiki kuwa atakuwa anakatwa
Kama kila kitu kinaonekana ni uongo na usanii, basi duniani kusingekuwa na serikali zinazochaguliwa na watu. Mtu ambaye haamini kila anachoambiwa, maana yake ni kwamba yeye binafsi hana uaminifu na sio wale wanaomzunguka.
 

Hata akikatwa milioni kumi bado mshahara wake hautakuwa umeshtuka maana kila kitu bure na kodi hakatwi.Nilifikiri angesema kuanzia sasa Mishahara yote ya Mawaziri,wa kwake ,wa Makamu na wabunge lazima ikatwe kodi.Atleast 30% ya mshahara ingeingia kwenye Maendeleo.Lakini milioni sita,kwa mshahara na marupurupu yake bado ni kama tone la maji kwenye Bahari hindi
 


Tayari unatoa zaidi ya hapo. Au tuseme unatakiwa kutoa. Kupitia kodi yako.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…