Magufuli hatambuliki E.A.C?

Muwe mnachunguza kwamba kabla hamjaandika: Hao wengine sina sababu ya kutafuta ikiwa wamepongeza au hapana coz' hakuna hata mmoja miongoni mwao ambae yupo madarakani kwa kupitia uchaguzi halali kwahiyo mnageuka kiroja mnaposema eti mtu kama Museven au Nkruziza au Kagame hawajaridhishwa na mwenendo wa uchaguzi wa Tanzania!!!
 

Unauliza swali halafu unajibu. Nini faida ya kusign protocol bila ya azma ya kuitekeleza? Ukiachilia mbali free movement na miradi ya northern corridor hata mambo madogo mfano one network tumeshidwa kutekeleza. One network imepunguza gharama ya regional calls kwa zaidi asilimia hamsini mataifa ya COW.
 
Sidhani maendeleo yetu yatategemea pongezi za watu. Na nani atakuambia salamu hizo na kama nani?

Hebu tubadilike kifikra na kiakili
 

Acha kufikilia v2 ambavyo havina faida.,mbona kapongezwa na watu wengi tuu..! Au unafikil nn kichwan mwako..?
 
Kama unaifuatilia vizuri issue ya East African Community, suala la hadi lini One Network Area liwe implemented, walijadiliana mwaka jana Kampala... sio kwenye kikao cha EAC bali cha CoW na katika kikao kile; sawa na vikao vingine vyote vya CoW, Burundi na Tanzania hazikuwepo! Kwahiyo Tanzania inaweza kujiunga at the right time kwake na sio kwa matakwa ya CoW na ndio maana hata Director wa TCRA ameshapata kulizungumzia suala hilo.

Kwamba nauliza swali halafu najibu coz' hao wanaosema tunachelewesha hizo ndiyo hoja zao ambazo mtu hapahitaji shahada kufahamu ni kwanini wanazungumzia sana issue hizo!!!!!! Kwamba, wanatengeneza CoW halafu wanatarajia TZ waunge mkono wakati haina faida yoyote kwetu!
 

Mkuu povu la nn,si uhamie huko cow!
 
Nyie mnaolalamikia ushindi wa Magufuli mlitaka ashinde nani. Huyo mnyemdhania alishindwa kabla hajaanza kampeni. Hakukuwa na mshindi zaidi ya Magufuli. A wasindikizaji lazima wawepo.
 
Mbona hata hiyo SADC yenu ilikua kimya na hamuongei.
 
Mkuu kiluuj
TUPOOOOO.....

nadhani umelipata jibu la maswali yako leo kwenye sherehe za kuapishwa Urais Dr John Joseph Pombe Magufuli kuhusu kutokutambulika kwake na viongozi wa E.A.C Kwenye Uwanja wa Taifa
 

Hata kupongeza ni protocol tu, kama hawamkubali wasingekuja.
 

margin ya kura million 2 hapo hapo unamawakala nchi nzima unibiwaje!? kale ndimu na kaongeze na ukwaju kama umechukia
 
nyie nyumbu viongozi wenu waliokataliwa na watanzania kama mnawapenda nendeni mkaishi nao masaki...sio mnalilia hapa eti kura zimeibiwa. kwani hamkuwa na mawakala...au hamkulinda kura?????
 

Kama huna cha Ku post kwanini usikae kimya
 
Ukawa wamechanganyikuwa vibaya sana.wanajaribu kuchora picha ionekane magufuli haungwi mkono na nchi jirani.poleni sana.watanzania wameshaamua.subirini 2020
 
margin ya kura million 2 hapo hapo unamawakala nchi nzima unibiwaje!? kale ndimu na kaongeze na ukwaju kama umechukia

Nina shaka na umakini wako. Nimesema kilichofanyika haikuwa wizi wa kura - rejea matukio niliyonakili hapo. Huu ulikuwa ubabe usio na mfano. Mbona unatoa makucha saaana?
 
Nina shaka na umakini wako. Nimesema kilichofanyika haikuwa wizi wa kura - rejea matukio niliyonakili hapo. Huu ulikuwa ubabe usio na mfano. Mbona unatoa makucha saaana?

Nani kachomwa kisu!? Nani kauwawa!? Hivi unaujua ubabale wewe?
Ila ipo siku mtakuja kuuona ubabe hasa ndipo mtakapojua kuwa mlikua kwenye nafasi nzuri sema nyie wenyewe mmeichezea
 
Watu wengine wanafikiri Lowassa ndiye rais!
Afadhali hao wanaofikiri, kuna baadhi ya maeneo watu wanafahamu kuwa Nyerere bado ni Rais hivyo wakati wa kura lazima wakipigie kura chama cha Nyerere
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…