Magufuli baba, kaza kamba UKUTA ni mbinu ya mafisadi

masopakyindi

Platinum Member
Jul 5, 2011
17,882
13,171
Serikali ya CCM awamu ya tano imeingia na gia kubwa ya kutokomeza ufisadi bila kujali uso wa fisadi.
Mafisadi wengi wako humu humu ndani ya serikali na chama tawala, na hata nje ya chama.
Tulimuelewa vizuri Magufuli aliposema tumuombee, maana kikulacho ki nguoni mwako.

Upinzani mkubwa tunaouona wa mafisadi kupitia CHADEMA na UKUTA wao si bure.
Hawa mafisadi wengine wakiongozwa na watu kama Lowassa, mirija yao kuingia mifuko ya hazina imekatwa.
Safari za ulaji nje ya nchi, wafanyakazi hewa, ulaji wa ushuru wa bandarini ni kati ya machache tu yaliyodhibitiwa.

Hii dhana ya UKUTA ni kilio tu cha kisiasa kwa mafisadi kupitia CHADEMA kurusha michanga mchoni kupoteza malengo ya maendeleo.
Ni mbinu ya kuleta fujo, mifarakano na kutoelewana ili azma ya maendeleo iliuoainishwa wakati wa kampeni yasitekelezwe.

Wananchi tulio nyuma yako Mgufuli tunakuombea na kukupa moyo uendelee kuwadhibiti hawa wana 'UKUTA kwa nguvu yoyote ile.

Na haiwezi kushindikana kuwadhibiti maana hata sisi wananchi tunaweza kuwadhibiti mitaani tukipewa jukumu hilo.

Tunataka reli, barabara, umeme wa uhakika ili ahadi ya viwanda tuliojiwekea itekelezwe bila ujinga wa kisiasa uitwao UKUTA, wenye nia ya kuua azma hiyo.
 
Serikali ya CCM awamu ya tano imeingia na gia kubwa ya kuyokomeza ufisadi bila kujali uso wa fisadi.
Mafisadi wengi wako humu humu ndani ya serikali na chama tawala, nabhata nje ya chama.
Tulimuelewa vixuri Magufuli aliposema tumuombee, maana kikulacho ki nguoni mwako.

Upinzani mkubwa tunaouonabwa mafisadi kupitia CHADEMA na UKUTA wao si bure.
Hawa mafisadi wengine wakiongozwa na watu kama Lowassa, mirija yao kuingia mifuko ya hazina imekatwa.
Safari za ulaji nje ya nchi, wafanyakazi hewa, ulaji wa ushuru wa bandarini ni kati ya machache tu yaliyodhibitiwa.

Hii dhana ya UKUTA ni kilio tu cha kisiasa kwa mafisadi kupiyia CHADEMA kurusha michanga mchoni kupoteza malengo ya maendeleo.
Ni mbinu ya kuleta fujo, mifarakano na kutoelewana ili azmabya maendeleo iliuoainishwa wakati wa kampeni yasitekelezwe.

Wananchi tulio nyuma yako Mgufuli tunakuombea na kukupa moyo uendelee kuwadhibiti hawa wana 'UKUTA kwa nguvu yoyote ile, na haiwezi kushindikana maana hata sisi wananchi tunaweza kuwadhibiti mitaani tukipewa jukumu hilo.

Tunataka reli, barabara, umeme wa uhakika ili ahadi ya viwanda tuliojiwekea itekelezwe bila ujinga wa kisiasa uitwao UKUTA, wenye nia ya kuua azma hiyo.
Watanigwa vibaya!, shauri Yao. Zama zao finito, wametupa madhira ya kutosha.
 
Ila ajali nyuso za mafisadi akina Lugumi, IPTL, escrow, Magufuli mnunuzi wa boti uozo na mkwapuzi wa nyumba za Serikali. Endelea kudumaza akili yako. Duh!

Serikali ya CCM awamu ya tano imeingia na gia kubwa ya kuyokomeza ufisadi bila kujali uso wa fisadi.
Mafisadi wengi wako humu humu ndani ya serikali na chama tawala, nabhata nje ya chama.
Tulimuelewa vixuri Magufuli aliposema tumuombee, maana kikulacho ki nguoni mwako.

Upinzani mkubwa tunaouonabwa mafisadi kupitia CHADEMA na UKUTA wao si bure.
Hawa mafisadi wengine wakiongozwa na watu kama Lowassa, mirija yao kuingia mifuko ya hazina imekatwa.
Safari za ulaji nje ya nchi, wafanyakazi hewa, ulaji wa ushuru wa bandarini ni kati ya machache tu yaliyodhibitiwa.

Hii dhana ya UKUTA ni kilio tu cha kisiasa kwa mafisadi kupiyia CHADEMA kurusha michanga mchoni kupoteza malengo ya maendeleo.
Ni mbinu ya kuleta fujo, mifarakano na kutoelewana ili azmabya maendeleo iliuoainishwa wakati wa kampeni yasitekelezwe.

Wananchi tulio nyuma yako Mgufuli tunakuombea na kukupa moyo uendelee kuwadhibiti hawa wana 'UKUTA kwa nguvu yoyote ile, na haiwezi kushindikana maana hata sisi wananchi tunaweza kuwadhibiti mitaani tukipewa jukumu hilo.

Tunataka reli, barabara, umeme wa uhakika ili ahadi ya viwanda tuliojiwekea itekelezwe bila ujinga wa kisiasa uitwao UKUTA, wenye nia ya kuua azma hiyo.
 
20160821_180914.jpg
 
Serikali ya CCM awamu ya tano imeingia na gia kubwa ya kutokomeza ufisadi bila kujali uso wa fisadi.
Mafisadi wengi wako humu humu ndani ya serikali na chama tawala, na hata nje ya chama.
Tulimuelewa vizuri Magufuli aliposema tumuombee, maana kikulacho ki nguoni mwako.

Upinzani mkubwa tunaouona wa mafisadi kupitia CHADEMA na UKUTA wao si bure.
Hawa mafisadi wengine wakiongozwa na watu kama Lowassa, mirija yao kuingia mifuko ya hazina imekatwa.
Safari za ulaji nje ya nchi, wafanyakazi hewa, ulaji wa ushuru wa bandarini ni kati ya machache tu yaliyodhibitiwa.

Hii dhana ya UKUTA ni kilio tu cha kisiasa kwa mafisadi kupitia CHADEMA kurusha michanga mchoni kupoteza malengo ya maendeleo.
Ni mbinu ya kuleta fujo, mifarakano na kutoelewana ili azma ya maendeleo iliuoainishwa wakati wa kampeni yasitekelezwe.

Wananchi tulio nyuma yako Mgufuli tunakuombea na kukupa moyo uendelee kuwadhibiti hawa wana 'UKUTA kwa nguvu yoyote ile.

Na haiwezi kushindikana kuwadhibiti maana hata sisi wananchi tunaweza kuwadhibiti mitaani tukipewa jukumu hilo.

Tunataka reli, barabara, umeme wa uhakika ili ahadi ya viwanda tuliojiwekea itekelezwe bila ujinga wa kisiasa uitwao UKUTA, wenye nia ya kuua azma hiyo.

Akina Lugola na wenzie wamefutiwa mashitaka na DPP, akina Mkapa na JK ameapa kuwalinda!! Mnataka kutudanganya na nini?
 
Akina Lugola na wenzie wamefutiwa mashitaka na DPP, akina Mkapa na JK ameapa kuwalinda!! Mnataka kutudanganya na nini?
Fikiria mbele mkuu.
Tunaenda uchumi wa viwanda umejitayarisha vipi hata kiwanda chako kidogo!
 
Fikiria mbeke mkuu.
Tunaenda uchumi wa viwanda umejitayarisha vipi hata kiwanda chako kidogo!
Uchumi wa viwanda kwa watu wasiomudu hata kununua chumvi? Ninafikiri sana kuliko wewe, situmii makalio kufikiri ndio maana nikauliza nchi ya viwanda ambayo watu wake ndio nyie?
 
Habari hii ilichapishwa kwenye gazeti la RAI miaka michache iliyopita ikisomeka...

Huyu Ndiye Pombe Magufuli:

- Wasema nyumba 8,000 kauza kwa mkono wake mwenyewe
- Apuuza maonyo ya wataalamu- Mafaili ya Sundi na Musa aliyabeba kwapani

ALIYEKUWA Waziri wa Ujenzi, John Magufuli, katika Serikali ya awamu ya tatu, aliteka madaraka na kuwa mwenyekiti wa zoezi la kuuza nyumba za serikali ambazo hadi sasa, zimeshauzwa 8,288 imefahamika.

Habari zilizopatikana ndani ya wakala wa Majengo ya Serikali (TBA), zimethibitishia Rai wiki hii kwamba Magufuli alihakikisha anashiriki kama Mwenyekiti katika zoezi zima la kuuza nyumba, ambalo kimsingi lilistahili kusimamiwa na Mtendaji Mkuu wa TBA.

Kwa mujibu wa vyanzo kadhaa vya habari ndani ya TBA, Magufuli alifanya kila aina ya ‘fujo’ katika zoezi la kuuza nyumba hizo, wakati mwingine akibatilisha maamuzi yaliyofanywa na Kamati ya TBA ya kuuza nyumba hizo, akiwapangia watu nyumba kwa utashi wake na wakati mwingine akiwakemea wale wote waliomshauri kinyume na matakwa.

Ni chini ya utaratibu huo, habari zinaeleza kwamba Magufuli, aliyabeba yeye mwenyewe mafaili ya ndugu zake; Musa Magufuli ambaye ni mdogo wake, na Sundi Malomo ambaye ni mzazi mwenzake na kuwalazimisha watendaji wa TBA wafuate matakwa yake katika kuwapatia nyumba ndugu zake hao.

Habari hizo zinaeleza kwamba awali Mtendaji Mkuu wa TBA alimshauri Magufuli kwamba suala la mauzo ya nyumba kwa ndugu zake ni kinyume cha utaratibu. Hata hivyo, imeelezwa kwamba Magufuli alilazimisha huku akisema mdogo wake hana tatizo kwa sababu alikuwa tayari mfanyakazi wa Serikali.

Musa aliajiriwa kwa mkataba wa miezi mitatu, baada ya mwezi mmoja akauziwa nyumba na baada ya miezi miwili akaacha kazi.

“Kwa upande wa Sundi, kwanza ilikuwa Sundi auziwe nyumba moja kwa moja. Lakini Magufuli alipoonywa akashtuka na kusema suala hilo aachiwe yeye mwenyewe. Na ndipo akaibuka na jina la Stanley Manongi kwamba ndiye mnunuzi halisi na baba yake Sundi,” vinasema vyanzo hivyo vya habari, vingine ambavyo vilishiriki moja kwa moja katika mchakato wa uuzaji nyumba hizo.

Habari hizo zinaendelea kueleza kwamba baadaye, Sundi alishtuka akitilia shaka uaminifu wa Manongi, kwamba angeweza kumdhulumu nyumba hiyo.

“Ndipo Magufuli aliibuka na mpango wa Sundi kuwa mtoto wa Manongi na mrithi wake na kisha kwa kuhakikisha kwamba hakuna dhuluma yoyote, mtoto wa Sundi naye akarithishwa na kama mrithi wa pili,” chanzo hicho cha habari kinaeleza.

Chini ya sheria ya Executive Agency Act No. 30 ya mwaka 1997, TBA ilipewa madaraka yote ya kuuza nyumba za Serikali, kujenga nyumba mpya, kuzikarabati zilizopo pamoja na kugawa nyumba za madaraja A, B na C kwa wafanyakazi wa Serikali.

Sheria hiyo inaipa mamlaka ya kipekee ya kufanya shughuli zote bila kuingiliwa na chombo chochote.

Chini ya sheria hiyo, Waziri anaruhusiwa kuteua wajumbe wa bodi ya ushauri watakaomshauri Katibu Mkuu wa Wizara juu ya namna nzuri ya TBA kusimamia mamlaka yake.

Hadi Machi mwaka huu, wajumbe hao walikuwa ni J. Kijazi, E. Lipambila, E. Lugwisha, Msangi, E. Mwakalinga, D. Kisasi, P. Ncheye, F. Werema na A. Bukuku.

Hata hivyo, sheria haitoi nafasi yoyote kwa Waziri kusimamia shughuli za uuzwaji au upangaji wa nyumba za serikali.

Mtendaji Mkuu wa TBA Togolayi Makumba Kimweri, alipoulizwa kupitia kwa Katibu Muhtasi wake, alimwambia mwandishi wa Rai aandike maswali kisha asubiri kuruhusiwa kuingia ndani ya ofisi.

Hata hivyo, baada ya kusubiri kwa muda wa saa moja, mwandishi alipokwenda kuuliza akaambiwa kwamba Kimweri tayari alikwishaondoka ofisini kupitia mlango wa nyuma na asingeweza kurudi ofisini.

Lakini baadhi ya wafanyakazi wa TBA wameiambia Rai kwamba kinachoandikwa kwenye magazeti kuhusu ushiriki wa Magufuli kuuza nyumba za Serikali ni kidogo mno kuliko hali halisi.

Kama ilivyokuwa kwa mdogo wake Musa, waziri Magufuli alishinikiza mtoto wa dada yake anayeitwa James Doto Mgosha auziwe nyumba za serikali kwa kumtengenezea ajira ya muda mfupi katika TANROADS.

Tofauti na Musa, Doto ameuziwa nyumba hiyo kwa jina la mtu mwingine lakini anaishi katika nyumba hiyo, namba 64 iliyopo Kinondoni Flats.

Habari kutoka TBA zinaonyesha jina la mtu mwingine (tunalihifadhi) kuwa ndiye aliyeuziwa nyumba hiyo mtu huyo alipata kupitia utaratibu wa Magufuli kupeleka jina lake kwenye wakala wa majengo na kulazimisha apewe nyumba.

Alipoulizwa kwa njia ya simu, Doto alisema suala la ajira na nyumba waulizwe waliomwajiri na kumpa nyumba. Akakata simu.

Mfanyakazi mwingine alieleza Rai kwamba msichana mwingine (jina tunalihifadhi) akiwa na miezi minne tu kazini alipelekwa na Magufuli katika Wakala wa Majengo akilazimisha auziwe nyumba hata kabla ya kuthibitishwa kazini. Nyumba hiyo iko Block A, Ocean Road.

Hata hivyo, habari hizo zinaeleza kwamba msichana huyo ambaye hadi sasa anaishi na wazazi wake, ameipangisha nyumba hiyo kwa mfanyakazi mmoja wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa na analipwa kwa dola za kimarekani.

“Kuuza nyumba za serikali sawa, lakini kweli katika mtindo huu? Sisi tunaoshiriki kuzikagua na kuziratibu tukiomba hatupati, lakini wengine wanaingia serikalini miezi miwili wanapata nyumba. Na wengine hata si wafanyakazi, wanapata, hii si sahihi, alilalamika mfanyakazi mmoja aliyeandikia Rai kwa njia ya barua pepe.

Hadi Machi mwaka huu Wakala wa Majengo wa Serikali (TBA) walishauza nyumba 8,288 ambazo hata hivyo zilitakiwa kuuzwa kwa watumishi wa serikali.

Katika mauzo hayo, Serikali ilitarajia kupata jumla ya shilingi 60,016,556,439.00. Hata hivyo hadi sasa Serikali imepata shilingi 22,684,108,115.08.

Kwa sasa, Serikali imebakiwa na nyumba 1,098 zinazosimamiwa na TBA. Kati ya hizo, nyumba 692 zimetengwa kwa wafanyakazi wa Serikali, nyumba 675 kama tied quarters, nyumba 111 zinatumika kama Rest House za Serikali, wakati nyumba 40 zinatumika kama state lodges. Nyumba 24 zinatumika kama ofisi na nyingine 29 ni kama karakana na bohari.

SALVA RWEYEMAMU
RAI
 
Waziri wa Ujenzi Dk. John Pombe Magufuli akikagua ujenzi wa kituo cha Mradi wa Mabasi yaendayo haraka (BRT) Morocco jijini Dar es Salaam siku za hivi karibuni. Picha na Maktaba
By Ibrahim Yamola, Mwananchi
In Summary


Ukaguzi maalumu uliofanywa na ofisi ya CAG katika kipindi cha mwaka wa fedha 2010/11 na 2011/12 umebaini kuwa taarifa iliyotolewa na Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli, bungeni Novemba 2013 kuwa fedha hizo zilitumika kwa miradi ya ujenzi wa barabara, haikuwa sahihi.

Dar es Salaam. Machungu ya Watanzania yakiwa hayajapoa kutokana na kashfa ya Sh306 bilioni kutoka katika Akaunti ya Tegeta Escrow, ufisadi mwingine wa zaidi ya Sh252 bilioni umeibuliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa Assad ndani ya wizara ya ujenzi.

Ukaguzi maalumu uliofanywa na ofisi ya CAG katika kipindi cha mwaka wa fedha 2010/11 na 2011/12 umebaini kuwa taarifa iliyotolewa na Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli, bungeni Novemba 2013 kuwa fedha hizo zilitumika kwa miradi ya ujenzi wa barabara, haikuwa sahihi.

Kutokana na ufisadi huo, habari zilizolifikia Mwananchi zinasema CAG amependekeza hatua stahiki zichukuliwe kwa wahusika wa wizara ya ujenzi na wakala wa barabara ili kuleta imani na uwazi katika bajeti kwa jamii na wahisani.

“Wizara (ya ujenzi) ililidanganya Bunge kuwa kuna ujenzi wa barabara hizo wakati wakijua kwamba walikusudia kulipa madeni ya wakandarasi na washauri wa ujenzi wa barabara...mpango mkakati wa wakala wa barabara wa mwaka wa fedha 2011/12 pamoja na manunuzi ulioidhinishwa havikuonyesha utekelezaji wa mradi huo,” chanzo cha habari kilikariri ripoti ya CAG.

Matumizi hayo yasiyo sahihi yaliibuliwa na Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) Novemba 22, 2013 baada ya kutilia shaka kiasi hicho cha fedha na ofisi ya CAG kuagizwa kufanya ukaguzi.

Katika kikao hicho ambacho wizara ya ujenzi iliwakilishwa na Katibu Mkuu wake wa wakati huo, Balozi Herbert Mrango alihojiwa na Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe kuhusu hati ya mashaka waliyoipata kutoka kwa CAG mwaka 2011/12.

Kamati hiyo ilieleza kuwa kwenye Bajeti ya mwaka huo Sh348.1 bilioni zilizokuwa zimetengwa chini ya fungu lililokuwa limetajwa kuwa ni la mradi maalumu hazikutumiwa kwa malengo yaliyoelezwa bungeni.

“Ni vizuri leo (ilikuwa Novemba 22 mwaka 2013) uiambie kamati fedha hizi ziliombwa kwa kitu gani na zilitumika kwa jambo gani. Tunajua kwamba fedha hizi zilipunguzwa Sh95 bilioni na kupelekwa Wizara ya Uchukuzi, zilibakia Sh252.975 bilioni katika kifungu hicho lakini kuna bilioni 100 zimetumika visivyo,” alisema Zitto.

Alisema katika majumuisho ya bajeti wizara hiyo, Dk Magufuli na Dk Harrison Makyembe aliyekuwa Naibu waziri wa wakati huo aliyekuwa Waziri wa Sera, Uratibu na Bunge, William Lukuvi walitoa maelezo yasiyo ya kweli bungeni kuhusu fedha hizo.

Zitto alikariri maneno yaliyorekodiwa kwenye Hansard ya Bunge yaliyosemwa na viongozi hao watatu.

“Tunaomba fedha Sh252 bilioni kwa ajili ya kuanzia kazi za ujenzi wa barabara.”

“Fedha hizi zitachangia miradi ya wafadhili,” haya yalikuwa maneno ya Dk Makyembe ambaye sasa ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakati akifafanua majumuisho.

“Hizi ni fedha kwa ajili ya Counterpart fund,” alimkariri Lukuvi ambaye sasa ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi wakati akichangia hotuba ya wizara hiyo.

Chanzo cha habari kimeeleza kuwa ripoti ya CAG imeeleza kuwa, “Katika kikao cha kuanza ukaguzi huo Aprili 3, mwaka jana uongozi wa wizara ulithibitisha kwamba hakukuwa na barabara mpya bali walifanya hivyo baada ya kuona madeni yamekuwa makubwa kiasi cha Sh420 bilioni kama yalivyokuwa kwenye hesabu za wakala wa barabara za mwaka wa fedha 2010/11.”

Katika ukaguzi huo imebainishwa kuwa Sh3 bilioni hazikujulikana matumizi yake.

Taarifa zaidi zinasema baada ya wizara kupeleka fedha kwa wakala wa barabara, fedha hizo zilifanyiwa mchakato wa kuzigawa upya lakini nyaraka halisi zilizotumika kugawa fedha hizo hazikuwasilishwa kwa ukaguzi.

“Hata hivyo, kati ya Sh175.3 bilioni zilizopitia kwenye akaunti ya maendeleo ya wakala wa barabara, kiasi cha Sh3,048,365,229 hakikuweza kupatiwa maelezo jinsi kilivyotumika.

“Pia, kati ya malipo ya Sh77.7 bilioni yaliyofanyika kwa wakandarasi au washauri wa barabara moja kwa moja kupitia Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Novemba 30, mwaka 2011 kupitia barua ya kumbukumbu namba GA.65/263/01/VOL.XI Gavana Mkuu wa BoT, alikanusha kulipa asilimia 30 ya fedha hizo Sh30.6 bilioni.

“Gavana wa BoT amekanusha kulipa Sh30.6 bilioni kwa kampuni ya M/S Strabag Internationl Gmbn na M/S China-Engineering Corporation Co, kati ya Sh77.7 ambacho kilipelekwa BoT kwa ajili ya malipo kwa wakandarasi au washauri mbalimbali,” alifafanua zaidi mtoa habari hizi na kuongeza:

“Ukaguzi maalumu umeshindwa kuthibitisha malipo yenye jumla ya Sh47.1 bilioni sawa na asilimia 61 kama yalilipwa kwa walengwa waliokusudiwa kwa sababu Gavana wa BoT amesema kuwa kisheria hatakiwi kutoa taarifa za wateja.”

Pia, habari za ndani kutoka ofisi ya CAG zinadai kuwa, Sh13.4 bilioni za ujenzi wa barabara za mikoa zilitumika kulipia barabara binafsi na za halmashauri za wilaya ambazo hutengewa fedha kupitia mfuko wa barabara kinyume na makusudio yaliyopitishwa na Bunge.

“Pia, nimebaini kwamba baadhi ya miradi haikuwamo kwenye kasma zilizopitishwa na Bunge kwenye makisio ya mwaka wa fedha 2010/11 na miradi mingine ilitengewa fedha kidogo lakini wakala wa barabara alitumia fedha nyingi kulipia miradi hiyo bila kuonyesha jinsi alivyozipata,” chanzo cha habari kimekariri ripoti ya CAG.

Katika ukaguzi huo, ufisadi mwingine wa Sh36.6 bilioni ambazo ni malipo ambayo hayakutolewa taarifa kwenye ripoti za washauri au wakandarasi, jambo linaweza kuwapo kwa uwezekano mkubwa wa wakandarasi kuidai Serikali zaidi ya mara moja na kuitia Serikali hasara.

Mtoa habari wetu alisema kuwa Sh6.2 bilioni zilitumika kuwalipa wakandarasi ambao hawakuonyeshwa katika orodha ya madeni yaliyowasilishwa bungeni pamoja na malipo ya Sh6.6 bilioni yaliyokwishalipwa yaliombewa tena.

“Madeni hayo yalikuwa yamelipwa na wakala wa barabara katika mikoa husika. Hali hii inaashiria kwamba kwa hati ya madai moja kuna uwezekano wa mkandarasi kulipwa mara mbili au zaidi.

Katika mapendekezo ya jumla, chanzo chetu kimesema ofisi ya CAG imeishauri Serikali kusimamisha kuingia mikataba mipya ya ujenzi wa barabara na ilipe madeni ya wakandarasi yaliyopo kwa sasa ili kuepuka ukuaji wa deni hilo kwa siku za baadaye na kuwa mzigo kwa Taifa na wananchi.

“Serikali ihakikishe inaheshimu mikataba iliyowekwa kati yake na wakandarasi ili kuepuka malipo yenye riba na kushtakiwa na wakandarasi kutokana na kuvunja masharti yaliyowekwa kwenye mikataba,” kilifafanua chanzo chetu na kuongeza:

“Zabuni za ujenzi wa barabara mpya ziendane na fedha zilizotengwa katika mwaka wa fedha husika kama itakavyokuwa imeainishwa katika mpango wa manunuzi wa mwaka huo.”

Ukaguzi huo maalumu uliohusisha miradi 46 ya ujenzi wa barabara kuu na barabara za mikoa ambazo wakandarasi na washauri wa ujenzi wa barabara walitoa huduma kwa wakala wa barabara.

“Mbali na miradi hii 46, miradi yote ya wakala wa barabara ilikuwa imezalisha madeni ya jumla ya Sh420 bilioni kama yalivyo kwenye hesabu za wizara kufikia mwaka wa fedha 2010/11,” kilieleza chanzo chetu.

Sakata hili limeibuka wakati lile la uchotwaji wa fedha za Akautni ya Tegeta Escrow halijapoa na hadi sasa limesababisha Rais Jakaya Kikwete kufanya mabadiliko madogo ya baraza lake la mawaziri kufuatia kumfukuza kazi, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka huku Profesa Sospeter Muhongo alitangaza kuachia wadhifa wa Waziri wa Nishati na Madini.

Mbali na hao, pia Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema alitangaza kujiuzuru huku Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue akimsimamisha kazi, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi kupisha uchunguzi wa sakata hilo.

Katika mlolongo wa hatua za kinidhamu kuchukuliwa, baadhi ya watumishi wa umma wamefikishwa mahakamani na wengine mbele ya Baraza la Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma.
 
Habari hii ilichapishwa kwenye gazeti la RAI miaka michache iliyopita ikisomeka...

Huyu Ndiye Pombe Magufuli:

- Wasema nyumba 8,000 kauza kwa mkono wake mwenyewe
- Apuuza maonyo ya wataalamu- Mafaili ya Sundi na Musa aliyabeba kwapani

ALIYEKUWA Waziri wa Ujenzi, John Magufuli, katika Serikali ya awamu ya tatu, aliteka madaraka na kuwa mwenyekiti wa zoezi la kuuza nyumba za serikali ambazo hadi sasa, zimeshauzwa 8,288 imefahamika.

Habari zilizopatikana ndani ya wakala wa Majengo ya Serikali (TBA), zimethibitishia Rai wiki hii kwamba Magufuli alihakikisha anashiriki kama Mwenyekiti katika zoezi zima la kuuza nyumba, ambalo kimsingi lilistahili kusimamiwa na Mtendaji Mkuu wa TBA.

Kwa mujibu wa vyanzo kadhaa vya habari ndani ya TBA, Magufuli alifanya kila aina ya ‘fujo’ katika zoezi la kuuza nyumba hizo, wakati mwingine akibatilisha maamuzi yaliyofanywa na Kamati ya TBA ya kuuza nyumba hizo, akiwapangia watu nyumba kwa utashi wake na wakati mwingine akiwakemea wale wote waliomshauri kinyume na matakwa.

Ni chini ya utaratibu huo, habari zinaeleza kwamba Magufuli, aliyabeba yeye mwenyewe mafaili ya ndugu zake; Musa Magufuli ambaye ni mdogo wake, na Sundi Malomo ambaye ni mzazi mwenzake na kuwalazimisha watendaji wa TBA wafuate matakwa yake katika kuwapatia nyumba ndugu zake hao.

Habari hizo zinaeleza kwamba awali Mtendaji Mkuu wa TBA alimshauri Magufuli kwamba suala la mauzo ya nyumba kwa ndugu zake ni kinyume cha utaratibu. Hata hivyo, imeelezwa kwamba Magufuli alilazimisha huku akisema mdogo wake hana tatizo kwa sababu alikuwa tayari mfanyakazi wa Serikali.

Musa aliajiriwa kwa mkataba wa miezi mitatu, baada ya mwezi mmoja akauziwa nyumba na baada ya miezi miwili akaacha kazi.

“Kwa upande wa Sundi, kwanza ilikuwa Sundi auziwe nyumba moja kwa moja. Lakini Magufuli alipoonywa akashtuka na kusema suala hilo aachiwe yeye mwenyewe. Na ndipo akaibuka na jina la Stanley Manongi kwamba ndiye mnunuzi halisi na baba yake Sundi,” vinasema vyanzo hivyo vya habari, vingine ambavyo vilishiriki moja kwa moja katika mchakato wa uuzaji nyumba hizo.

Habari hizo zinaendelea kueleza kwamba baadaye, Sundi alishtuka akitilia shaka uaminifu wa Manongi, kwamba angeweza kumdhulumu nyumba hiyo.

“Ndipo Magufuli aliibuka na mpango wa Sundi kuwa mtoto wa Manongi na mrithi wake na kisha kwa kuhakikisha kwamba hakuna dhuluma yoyote, mtoto wa Sundi naye akarithishwa na kama mrithi wa pili,” chanzo hicho cha habari kinaeleza.

Chini ya sheria ya Executive Agency Act No. 30 ya mwaka 1997, TBA ilipewa madaraka yote ya kuuza nyumba za Serikali, kujenga nyumba mpya, kuzikarabati zilizopo pamoja na kugawa nyumba za madaraja A, B na C kwa wafanyakazi wa Serikali.

Sheria hiyo inaipa mamlaka ya kipekee ya kufanya shughuli zote bila kuingiliwa na chombo chochote.

Chini ya sheria hiyo, Waziri anaruhusiwa kuteua wajumbe wa bodi ya ushauri watakaomshauri Katibu Mkuu wa Wizara juu ya namna nzuri ya TBA kusimamia mamlaka yake.

Hadi Machi mwaka huu, wajumbe hao walikuwa ni J. Kijazi, E. Lipambila, E. Lugwisha, Msangi, E. Mwakalinga, D. Kisasi, P. Ncheye, F. Werema na A. Bukuku.

Hata hivyo, sheria haitoi nafasi yoyote kwa Waziri kusimamia shughuli za uuzwaji au upangaji wa nyumba za serikali.

Mtendaji Mkuu wa TBA Togolayi Makumba Kimweri, alipoulizwa kupitia kwa Katibu Muhtasi wake, alimwambia mwandishi wa Rai aandike maswali kisha asubiri kuruhusiwa kuingia ndani ya ofisi.

Hata hivyo, baada ya kusubiri kwa muda wa saa moja, mwandishi alipokwenda kuuliza akaambiwa kwamba Kimweri tayari alikwishaondoka ofisini kupitia mlango wa nyuma na asingeweza kurudi ofisini.

Lakini baadhi ya wafanyakazi wa TBA wameiambia Rai kwamba kinachoandikwa kwenye magazeti kuhusu ushiriki wa Magufuli kuuza nyumba za Serikali ni kidogo mno kuliko hali halisi.

Kama ilivyokuwa kwa mdogo wake Musa, waziri Magufuli alishinikiza mtoto wa dada yake anayeitwa James Doto Mgosha auziwe nyumba za serikali kwa kumtengenezea ajira ya muda mfupi katika TANROADS.

Tofauti na Musa, Doto ameuziwa nyumba hiyo kwa jina la mtu mwingine lakini anaishi katika nyumba hiyo, namba 64 iliyopo Kinondoni Flats.

Habari kutoka TBA zinaonyesha jina la mtu mwingine (tunalihifadhi) kuwa ndiye aliyeuziwa nyumba hiyo mtu huyo alipata kupitia utaratibu wa Magufuli kupeleka jina lake kwenye wakala wa majengo na kulazimisha apewe nyumba.

Alipoulizwa kwa njia ya simu, Doto alisema suala la ajira na nyumba waulizwe waliomwajiri na kumpa nyumba. Akakata simu.

Mfanyakazi mwingine alieleza Rai kwamba msichana mwingine (jina tunalihifadhi) akiwa na miezi minne tu kazini alipelekwa na Magufuli katika Wakala wa Majengo akilazimisha auziwe nyumba hata kabla ya kuthibitishwa kazini. Nyumba hiyo iko Block A, Ocean Road.

Hata hivyo, habari hizo zinaeleza kwamba msichana huyo ambaye hadi sasa anaishi na wazazi wake, ameipangisha nyumba hiyo kwa mfanyakazi mmoja wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa na analipwa kwa dola za kimarekani.

“Kuuza nyumba za serikali sawa, lakini kweli katika mtindo huu? Sisi tunaoshiriki kuzikagua na kuziratibu tukiomba hatupati, lakini wengine wanaingia serikalini miezi miwili wanapata nyumba. Na wengine hata si wafanyakazi, wanapata, hii si sahihi, alilalamika mfanyakazi mmoja aliyeandikia Rai kwa njia ya barua pepe.

Hadi Machi mwaka huu Wakala wa Majengo wa Serikali (TBA) walishauza nyumba 8,288 ambazo hata hivyo zilitakiwa kuuzwa kwa watumishi wa serikali.

Katika mauzo hayo, Serikali ilitarajia kupata jumla ya shilingi 60,016,556,439.00. Hata hivyo hadi sasa Serikali imepata shilingi 22,684,108,115.08.

Kwa sasa, Serikali imebakiwa na nyumba 1,098 zinazosimamiwa na TBA. Kati ya hizo, nyumba 692 zimetengwa kwa wafanyakazi wa Serikali, nyumba 675 kama tied quarters, nyumba 111 zinatumika kama Rest House za Serikali, wakati nyumba 40 zinatumika kama state lodges. Nyumba 24 zinatumika kama ofisi na nyingine 29 ni kama karakana na bohari.

SALVA RWEYEMAMU
RAI

Kwenye nepotism na ukabila huyu bwana amwombe sana Mungu wake amponye.... hatusemi mengi ila Yetu Macho.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Rais Magufuli mambo hadharani
Posted by: Faki Sosi May 18, 2016

KASHFA zimeanza kumiminika baada ya Dk. John Magufuli wakati akiwa Waziri wa Ujenzi katika Serikali ya Awamu ya Nne kudaiwa kuridhia ununuzi wa Kivuko cha Mv. Dar es Salaam feki na kibovu, anaandika Faki Sosi.

Manunuzi ya kivuko hicho kibovu, feki yalifanywa na Wakala wa Ufundi Umeme (TAMESA) na kugharimu Dola za Marekani 4,980,000 sawa na Sh. 7.916 Bil.

James Mbatia, Msemaji wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni katika Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano amesema hayo wakati akisoma hotuba yake jana bungeni. Ifuatayo ni sehemu ya hotuba hiyo;

UFISADI KATIKA VIVUKO NA MADARAJA NCHINI

3.2.1.Ununuzi wa Kivuko Kibovu cha Dar es Salaam -Bagamoyo

Mheshimiwa Spika, Kivuko kutoka Dar es Salaam kwenda Bagamoyo ni jipu ambalo limeiva kwa viwango vyote na sasa linatakiwa litumbuliwe mara moja.

Ni dhahiri kuwa Kivuko cha Dar es Salaam kwenda Bagamoyo kilichonunuliwa na TEMESA chini ya uongozi wa waziri wa Ujenzi wa serikali ya awamu ya nne ambaye ndiye Rais wa Tanzania wa sasa.

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) katika Hesabu za Serikali kuu akikagua Taarifa za fedha kwa mwaka ulioishia tarehe 30 Juni 2015 iliyotolewa mwezi Machi 2016 (Ukurasa wa 132 na 133), alibaini ununuzi wa boti feki na mbovu uliofanywa na TEMESA na kugharimu Dola za Marekani 4,980,000 sawa na shilingi 7,916,955,000 kupitia mkataba namba AE/006/2012-13/HQ/G/CN-39 uliosainiwa tarehe 25 April 2013 kati ya TEMESA kwa niaba ya Serikali na Mzabuni M/s Johs.Gram-Hanssen Bergensgade.

Mheshimiwa Spika, CAG alibaini masuala makuu mawili kuhusu ununuzi huo wa kivuko feki na kibovu cha Dar es Salaam – Bagamoyo.

Jambo la kwanza CAG alibaini kasi ya kivuko hicho ni tofauti na kasi iliyotakiwa kuwepo, jambo la pili ni kuwa cheti cha kukikubali kivuko hicho kilikuwa hakijatolewa kinyume na Kanuni ya 247 ya Manunuzi ya Umma.

Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inahoji, tabibu wa kutumbua jipu hili yuko wapi? Au msemo usemao kuwa“mganga hajigangi” unatumika hapa?
 
Ahsante sana Mkuu halafu kuna wasiojitambua wanafumbia macho mambo chungu nzima yanayofanywa na huyu dikteta uchwara na aliyoyafanya kabla hajaingia madarakani. Hafai huyu ni JANGA KUBWA LA TAIFA.

Kwenye nepotism na ukabila huyu bwana amwombe sana Mungu wake amponye.... hatusemi mengi ila Yetu Macho.
 
Habari hii ilichapishwa kwenye gazeti la RAI miaka michache iliyopita ikisomeka...

Huyu Ndiye Pombe Magufuli:

- Wasema nyumba 8,000 kauza kwa mkono wake mwenyewe
- Apuuza maonyo ya wataalamu- Mafaili ya Sundi na Musa aliyabeba kwapani

ALIYEKUWA Waziri wa Ujenzi, John Magufuli, katika Serikali ya awamu ya tatu, aliteka madaraka na kuwa mwenyekiti wa zoezi la kuuza nyumba za serikali ambazo hadi sasa, zimeshauzwa 8,288 imefahamika.

Habari zilizopatikana ndani ya wakala wa Majengo ya Serikali (TBA), zimethibitishia Rai wiki hii kwamba Magufuli alihakikisha anashiriki kama Mwenyekiti katika zoezi zima la kuuza nyumba, ambalo kimsingi lilistahili kusimamiwa na Mtendaji Mkuu wa TBA.

Kwa mujibu wa vyanzo kadhaa vya habari ndani ya TBA, Magufuli alifanya kila aina ya ‘fujo’ katika zoezi la kuuza nyumba hizo, wakati mwingine akibatilisha maamuzi yaliyofanywa na Kamati ya TBA ya kuuza nyumba hizo, akiwapangia watu nyumba kwa utashi wake na wakati mwingine akiwakemea wale wote waliomshauri kinyume na matakwa.

Ni chini ya utaratibu huo, habari zinaeleza kwamba Magufuli, aliyabeba yeye mwenyewe mafaili ya ndugu zake; Musa Magufuli ambaye ni mdogo wake, na Sundi Malomo ambaye ni mzazi mwenzake na kuwalazimisha watendaji wa TBA wafuate matakwa yake katika kuwapatia nyumba ndugu zake hao.

Habari hizo zinaeleza kwamba awali Mtendaji Mkuu wa TBA alimshauri Magufuli kwamba suala la mauzo ya nyumba kwa ndugu zake ni kinyume cha utaratibu. Hata hivyo, imeelezwa kwamba Magufuli alilazimisha huku akisema mdogo wake hana tatizo kwa sababu alikuwa tayari mfanyakazi wa Serikali.

Musa aliajiriwa kwa mkataba wa miezi mitatu, baada ya mwezi mmoja akauziwa nyumba na baada ya miezi miwili akaacha kazi.

“Kwa upande wa Sundi, kwanza ilikuwa Sundi auziwe nyumba moja kwa moja. Lakini Magufuli alipoonywa akashtuka na kusema suala hilo aachiwe yeye mwenyewe. Na ndipo akaibuka na jina la Stanley Manongi kwamba ndiye mnunuzi halisi na baba yake Sundi,” vinasema vyanzo hivyo vya habari, vingine ambavyo vilishiriki moja kwa moja katika mchakato wa uuzaji nyumba hizo.

Habari hizo zinaendelea kueleza kwamba baadaye, Sundi alishtuka akitilia shaka uaminifu wa Manongi, kwamba angeweza kumdhulumu nyumba hiyo.

“Ndipo Magufuli aliibuka na mpango wa Sundi kuwa mtoto wa Manongi na mrithi wake na kisha kwa kuhakikisha kwamba hakuna dhuluma yoyote, mtoto wa Sundi naye akarithishwa na kama mrithi wa pili,” chanzo hicho cha habari kinaeleza.

Chini ya sheria ya Executive Agency Act No. 30 ya mwaka 1997, TBA ilipewa madaraka yote ya kuuza nyumba za Serikali, kujenga nyumba mpya, kuzikarabati zilizopo pamoja na kugawa nyumba za madaraja A, B na C kwa wafanyakazi wa Serikali.

Sheria hiyo inaipa mamlaka ya kipekee ya kufanya shughuli zote bila kuingiliwa na chombo chochote.

Chini ya sheria hiyo, Waziri anaruhusiwa kuteua wajumbe wa bodi ya ushauri watakaomshauri Katibu Mkuu wa Wizara juu ya namna nzuri ya TBA kusimamia mamlaka yake.

Hadi Machi mwaka huu, wajumbe hao walikuwa ni J. Kijazi, E. Lipambila, E. Lugwisha, Msangi, E. Mwakalinga, D. Kisasi, P. Ncheye, F. Werema na A. Bukuku.

Hata hivyo, sheria haitoi nafasi yoyote kwa Waziri kusimamia shughuli za uuzwaji au upangaji wa nyumba za serikali.

Mtendaji Mkuu wa TBA Togolayi Makumba Kimweri, alipoulizwa kupitia kwa Katibu Muhtasi wake, alimwambia mwandishi wa Rai aandike maswali kisha asubiri kuruhusiwa kuingia ndani ya ofisi.

Hata hivyo, baada ya kusubiri kwa muda wa saa moja, mwandishi alipokwenda kuuliza akaambiwa kwamba Kimweri tayari alikwishaondoka ofisini kupitia mlango wa nyuma na asingeweza kurudi ofisini.

Lakini baadhi ya wafanyakazi wa TBA wameiambia Rai kwamba kinachoandikwa kwenye magazeti kuhusu ushiriki wa Magufuli kuuza nyumba za Serikali ni kidogo mno kuliko hali halisi.

Kama ilivyokuwa kwa mdogo wake Musa, waziri Magufuli alishinikiza mtoto wa dada yake anayeitwa James Doto Mgosha auziwe nyumba za serikali kwa kumtengenezea ajira ya muda mfupi katika TANROADS.

Tofauti na Musa, Doto ameuziwa nyumba hiyo kwa jina la mtu mwingine lakini anaishi katika nyumba hiyo, namba 64 iliyopo Kinondoni Flats.

Habari kutoka TBA zinaonyesha jina la mtu mwingine (tunalihifadhi) kuwa ndiye aliyeuziwa nyumba hiyo mtu huyo alipata kupitia utaratibu wa Magufuli kupeleka jina lake kwenye wakala wa majengo na kulazimisha apewe nyumba.

Alipoulizwa kwa njia ya simu, Doto alisema suala la ajira na nyumba waulizwe waliomwajiri na kumpa nyumba. Akakata simu.

Mfanyakazi mwingine alieleza Rai kwamba msichana mwingine (jina tunalihifadhi) akiwa na miezi minne tu kazini alipelekwa na Magufuli katika Wakala wa Majengo akilazimisha auziwe nyumba hata kabla ya kuthibitishwa kazini. Nyumba hiyo iko Block A, Ocean Road.

Hata hivyo, habari hizo zinaeleza kwamba msichana huyo ambaye hadi sasa anaishi na wazazi wake, ameipangisha nyumba hiyo kwa mfanyakazi mmoja wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa na analipwa kwa dola za kimarekani.

“Kuuza nyumba za serikali sawa, lakini kweli katika mtindo huu? Sisi tunaoshiriki kuzikagua na kuziratibu tukiomba hatupati, lakini wengine wanaingia serikalini miezi miwili wanapata nyumba. Na wengine hata si wafanyakazi, wanapata, hii si sahihi, alilalamika mfanyakazi mmoja aliyeandikia Rai kwa njia ya barua pepe.

Hadi Machi mwaka huu Wakala wa Majengo wa Serikali (TBA) walishauza nyumba 8,288 ambazo hata hivyo zilitakiwa kuuzwa kwa watumishi wa serikali.

Katika mauzo hayo, Serikali ilitarajia kupata jumla ya shilingi 60,016,556,439.00. Hata hivyo hadi sasa Serikali imepata shilingi 22,684,108,115.08.

Kwa sasa, Serikali imebakiwa na nyumba 1,098 zinazosimamiwa na TBA. Kati ya hizo, nyumba 692 zimetengwa kwa wafanyakazi wa Serikali, nyumba 675 kama tied quarters, nyumba 111 zinatumika kama Rest House za Serikali, wakati nyumba 40 zinatumika kama state lodges. Nyumba 24 zinatumika kama ofisi na nyingine 29 ni kama karakana na bohari.

SALVA RWEYEMAMU
RAI
Rai walisharipoti kuwa laigwanan nae alihusika na Richmond!
 
Leo Dkt.Magufuli amewaongoza wananchi wa Dsm kwenye majaribio ya uzinduzi wa Kivuko kipya Cha MV DAR ES SALAAM kitakachofanya safari zake kati ya Dsm na Bagamoyo, ambapo mamia ya wananchi wakiongozwa na Waziri Magufuli wamesafiri bure kutoka Dsm kwenda Bagamoyo na kurudi.

Kivuko hicho kimejengwa na kampuni ya Denmark na kwamba kimegharimu Sh7.9 bilioni.
"Kivuko hiki kitakuwa mkombozi kwa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam na kitakuwa kikifanya safari zake kuanzia Dar es Salaam hadi Bagamoyo," amesema Dk Magufuli.


Dk Magufuli anesafiri watu wengine wapatao 300 kwenda Bagamoyo na kurudi Dar ES Salaam, wengine alioongozana nao ni katika kivuko hicho ni; Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi - Mhandisi Mussa Iyombe, Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dsm, Balozi H.Mlango - M/Kiti Bodi ya TEMESA, Mkuu wa Mkoa wa Pwani - Mhandisi Everest Ndikilo, Mkurugenzi Mtendaji wa TEMESA, Mkurugenzi Mtendaji TANROADS .

Awali Waziri Dk Magufuli aliahidi kufanya jitihada za kupunguza foleni jijini Dar es Salaam ikiwa ni pamoja na kununua kivuko ambacho kitakuwa kinafanya safari kupitia Bahari ya Hindi Kutokea maeneo ya Feri(Dsm) mpaka Bagamoyo.

Dk Magufuli amesema sifa za kivuko hicho ni;


A) Kimetengenezwa kwa ubora wa hali ya juu na kina mwendo (speed) kubwa kuliko vivuko vyote Tanzania.
B) MV Dar es Salaam, kina ghorofa mbili.
C) Kimetengenezwa kwa teknolojia hal ya juu (teknolojia ya kisasa)
D) Muonekano wa ndani ni wa kisasa yakiwamo makochi mazuri na life jacket.
E) Kivuko hicho kina uwezo wa kubeba abiria kati ya 306 hadi 400.


Dkt. Magufuli aongoza wananchi kwenye majaribio ya uzinduzi wa kivuko cha MV Dar es Salaam
 
Back
Top Bottom