Magufuli aunguruma BRELA!

Magufuli aunguruma BRELA!

No wonder the Kagoda file is still missing, kumbe wazee wamelikanyaga miguuni! Mizizi ya Mbuyu, mi nakubaliana nawe kuwa JPM anastahili nafasi zaidi ya hii aliyonayo sasa, lakini kwa uzoefu inaonesha watu kama Magufuli ambao ni watendaji zaidi hawafanyi vizuri wanapokuwa kwenye nafasi za kidiplomasia zaidi kama ya urais, unajua rais ni mtoa maagizo zaidi kuliko utendaji sasa mtu kama JPG akiwa rais hatutaona juhudi hizi tunazoziona sasa, nitoe mfano mdogo tu, si unamkumbuka Charles Keenja, alifanya vizuri sana alipokuwa meya wa jiji la Dar, alileta mapinduzi makubwa sana Dar, hali inayoonekena sasa ya dar kwa kiwango kikubwa ni juhudi zake, lakini si uliona alipokuwa waziri wa chakula alifanya nini?madudu matupu. Mimi kwa pendekezo langu JPM akiwa waziri mkuu tutaona mabadiliko makubwa sana
 
Jamani WaTZ,
Kama ni umiliki wa biashara vigogo zaidi ya 80% wamo, lakini kwenye utendaji sidhani kama kuna anaemfikia Magufuli. GIVE THE DEVIL HIS DUE, anapofanya vizuri mtu apewe sifa zake.

Sawa. Basi kama na yeye ni kama hao 80% wengine basi hana distinction. Kusema hayuko peke yake ni kisingizio cha zamani, mtoto anakanywa na mzazi anadai hata mtoto wa jirani kafanya hivyo. Well, wa jirani hatuhusu. Magufuli ndio anawekwa kiti cha enzi, ukisema si peke yake unamaanisha na yeye ni wale wale.

Waziri, Mbunge, makazi kibao, unazunguka BRELA na TRA kusajili ki guest house chako Biharamulo, cha nini?
 
Sawa. Basi kama na yeye ni kama hao 80% wengine basi hana distinction. Kusema hayuko peke yake ni kisingizio cha zamani, mtoto anakanywa na mzazi anadai hata mtoto wa jirani kafanya hivyo. Well, wa jirani hatuhusu. Magufuli ndio anawekwa kiti cha enzi, ukisema si peke yake unamaanisha na yeye ni wale wale.

Waziri, Mbunge, makazi kibao, unazunguka BRELA na TRA kusajili ki guest house chako Biharamulo, cha nini?
Wana JF naona ndugu yetu, mtanzania mwenzetu Dilunga tusimchose sana kurudia rudia phrase za "guest house Biharamulo" inawezekana amekopi kwa hiyo kila post ikija ye ni kupaste tu maneno hayo hayo, labda siku nyingine atakuja na hoja za Mhe. JPM kumiliki salon. Wengi wetu tunamuona JPM ni hardworking kwa uwazi kabisa na wala hatuumi maneno.

Hivyo basi naomba naye amuanike hapa jamvini, bila kuuma maneno, waziri anayemuona angalau ni more hardworking kuliko Mhe. JPM so far at least kwa mifano. Naamini huwezi kumpinga mtu unless unaamini kuna mtu ambaye amedeliver/anadeliver zaidi. Naamini wana JF watatenda haki ktk hili!

Nawasilisha
 
Waziri mwenye muda wa kuzunguka BRELA na TRA kusajili mradi wake wa guest house hawezi kuwa ``by far most hardworking minister. `` Mtu mchapa kazi muadilifu mwenye majukumu mazito angesubiri amalize uwaziri ndio aanze ku run guest house.

Magufuli ni waziri, ni mbunge, ana mishahara kibao, I'm sure hakosi kwenye one of them sekretarieti za kamati kuu, anakula maposho ya mikutano kushoto na kulia.

Na bado una run ki guest house Biharamulo, cha nini? Huyo ndio ``the most hardworking``?

-Ni afadhali waziri anaye amua kuhangaika na kufanya ujasiriamali akapata riziki yake halali, kuliko yule ambaye anajifanya yuko ofisini kumbe anauza nchi ili ajilimbikizie mali ambayo hakuitolea jasho

- Ni afadhali yule anayetumia visenti anavyo pata hata akwekeza tena jimboni kwake, walu ukifika Biharamlo kuna guest nzuri ya kulala, kuliko yule anye waibia wananchi, na kwa vile kaiba anaenda kuwekeza dubai na visiwa vya jers.
-Ni afadhali Magufuri mara elfu kumi anavo kimbia kusajili ka guest kake apate shilingi mia kihalali, kuliko wale mawaziri feki wanaokao ofisini kupika majungu na kupanga mikakati ya kukwapua pesa zetu ili wabaki madarakani!
ni afadhali mara mia.. huyo Pombe... tunaona anacho kifanya hata akipelekwa wizara isiyo kuwa na kichwa wala miguu, kuliko hawa wanao badilishwa na kubebwa kwa kupewa wizara nyeti ambazo zinadodola kila kukicha!
 
Waziri mwenye muda wa kuzunguka BRELA na TRA kusajili mradi wake wa guest house hawezi kuwa ``by far most hardworking minister. `` Mtu mchapa kazi muadilifu mwenye majukumu mazito angesubiri amalize uwaziri ndio aanze ku run guest house.

Yaani astaafu ndio aanze kujifunza biashara? Wewe pale ulipo unasubiri ustaafu ndio uanze ujasiriamali? Muadilifu hastahili kufanya biashara akiwa kazini isipokuwa fisadi?

Magufuli ni waziri, ni mbunge, ana mishahara kibao, anakula maposho ya mikutano kushoto na kulia.

Mishahara kibao ni ipi hiyo? Ana mwajiri mmoja hvyo ana mshahara mmoja kwa mwezi. Au tupe data kama ana mwajiri mwingine pembeni.

I'm sure hakosi kwenye one of them sekretarieti za kamati kuu, anakula maposho ya mikutano kushoto na kulia.

Pure speculation. Wewe Dilunga una yako................
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom