GreatConqueror
Member
- Mar 27, 2009
- 75
- 5
Wana jamvi leo katika pitapita zangu za kuganga njaa nilijikuta nikiwa BRELA. Katika kupita huku na kule nikamuona Maghufuli akiwa na maafisa wa BRELA akistaajabu mafaili kuhifadhiwa hadi miguuni kwa maofisa wa Brela. Baadaye nikapata taarifa kuwa walimpa kisingizio kuwa hawana jengo na mafaili ni mengi sana. Nampongeza angalau kwa kuhoji ile hali kwani sijawahi kusikia waziri mwenye dhamana ya BRELA (WA VIWANDA NA BIASHARA) katembelea Agency hiyo nyeti serikalini. BRELA mtaendelea kuhifadhi mafaili kama maembe hadi lini? Mbona pesa mnakusanya?
NAWASILISHA!
NAWASILISHA!