Magufuli anasafisha nchi, tumuunge mkono

Magufuli anasafisha nchi, tumuunge mkono

Sasunimg

Member
Joined
Aug 3, 2016
Posts
58
Reaction score
34
Niliwaambia acheni jembe Magufuli asafishe, sasa mtafurahi. Hio ndio dawa ya nchi hii ingawa ni chungu, chungu, chungu, chungu!!

Tunatakiwa kufanya kazi kwa uadilifu jamani watanzania wenzangu ili kumuunga mkono Rais wetu.

Nawasilisha
 
Nakuunga mkono taifa lilipokuwa limefikia kama sio jpm sijui tungeenda wapi
 
Naunga mkono mia kwa mia nasubili nionge kama kutakuwepo jasiri anayeweza kuiba Yale mabilioni yaliyokuwa yanaibiwa kama vile taifa linavipofu tupu,
 
Waliharibu taratibu huku wapinzani wakiwambia. Wangalisikia wakati huo tusinge fikishana mahali pa kusimamisha katiba na sheria. Ni maamivu tu hamna cha kusifia.
 
Uhuru wa vyombo vya habari uhuru wa kupata habari na kutoa habari siasa safi kama sheria zinavyo sema kinyume na hapo tutakuwa tunadanganyana nibora ukubali kukosolewa ili uweze kujirekebisha huku kuminya minya mambo kuna tia mashaka nini kinafichwa kwa nguvu kubwa kiasi hiki hili la kujiuliza pia
 
Niliwaambia acheni jembe Magufuli asafishe, sasa mtafurahi. Hio ndio dawa ya nchi hii ingawa ni chungu, chungu, chungu, chungu!!

Tunatakiwa kufanya kazi kwa uadilifu jamani watanzania wenzangu ili kumuunga mkono Rais wetu.

Nawasilisha

Mtukufu, mwenye heri anasafisha sebule na kuweka taka chumba cha kulala, uvunguni mwa kitanda. Haya wewe endelea kumsifia na kumuunga mkono.
 
Niliwaambia acheni jembe Magufuli asafishe, sasa mtafurahi. Hio ndio dawa ya nchi hii ingawa ni chungu, chungu, chungu, chungu!!

Tunatakiwa kufanya kazi kwa uadilifu jamani watanzania wenzangu ili kumuunga mkono Rais wetu.

Nawasilisha
Tupo pamoja,
Alisema "jipu linauma sana", ila usaaa ukishatoka basi unapona, tuvumilie jamani hii ni process ya kuondoa usaa, soon tutapona.
 
Atabak na ndugu zake tu, hakuna wa kumuunga mkono mtu mgomvi na asife thamini utu wa mwingine
 
Hakuna raisi nzuri atakayefikiria kuvunja sheria alizoapa kuzilinda. Hakuna 'raisi nzuri' atakayefikiria kuwanyamazisha wanaothubutu kukemea uvunjifu wake wa sheria. Hakuna 'raisi nzuri' atakayeweza kuleta maendeleo ya kweli kwa wananchi wake waliojawa hofu na matendo yake yasiyotafsirika na yasiyotabirika. Hakuna 'raisi nzuri' atakayeweza kuwaletea mabadiliko ya kweli raia wake anayeamini kuwa uwezo alionao uko juu kuliko wengine wote na hivyo maamuzi yake ni ya mwisho. Kama tunataka kufanyia majaribio mambo hayo katika Tanzania ingekuwa busara kuwauliza Watanzania ama kwa kura ya maoni ama kwa njia nyingine yeyote ya kidemokrasia kama hivyo ndivyo wanavyotaka. Kando ya hapo ni kuifanyia nchi majaribio ya kuiongoza kwa kuweka kando utawala wa kisheria jambo ambalo matokeo yake hayajawahi kuwa mema kwa nchi yoyote iliyojaribu kufanya hivyo. Mungu ibariki Tanzania
 
Mtaisoma namba lazima tunyooke heshima irudi mlozoea vibaya niambieni nani kiongozi anaenda kunywa chai marekani kwa kodi za walala hoi ovyo saiz
 
Hakuna binadamu aliekamilika. Lakinii Magufuli anajitahidi sana kutaka nchi yetu iende mbele Ila kuna baadhi ya watu hawana subira.kasi yake ya utendaje kwa Kipindi hiki kidogo kimeleta mabadiliko makubwa hasa katika huduma za Serikali. Na kwa wa Tanzania tulipofikia tunahitaji rais kama Huyu wa kuleta adabu na nidhamu. Na azidishe kamba Hata kama wakimwita dictator ukweli tunahitaji dictator nchi ilishaoza
 
Alikuwa anaenda vizuri tu, lakini sasa anakosea kwa kuvunja katiba.
 
Back
Top Bottom