ni maneno ya kutafuta umaarufu kwa kupigiwa makofi kwa wingi.
wewe ulitaka afanyaje mkuu,akae kimya ili keshokutwa ukiwa ktk foreni uanze kupiga kelele tena?
Tatizo letu watanzania ni kwamba hatuwapendi wachapakazi,tunapenda sana kudanganywa danganywa na mwisho wa siku kupiga kelekele kwa makosa tuliyoyafanya wenyewe.mbona nchi za wenzetu haya mambo hayapo?
Jamani tembeeni muone,msikae tu mbagara ukazani ndio umemaliza Dunia.
Tukitaka barabara kama hizi ni lazima tumwache magufuri afanye kazi yake,kuliko kuleta siasa wakati bado msongamano wa magari unatuleta matatizo ktk jiji la DSM
katika nchi za wenzetu huwezi ona mtu kajenga ktk hifadhi ya barabara,na ndio maana hata barabara zao wanazipanua wakati wowote watakao kwani hakuna mwingiliano wa makazi na hifadhi za barabara.
lakini hapa bongo ni tatizo kubwa,tena watu hawataki kuguswa kabisa lakini ni wa kwanza kupiga kelekele pindi kunapotokea matatizo
Mimi ninge kuwa Magufuri,nisinge mwangalia mtu usoni,kwani barabara hizo si kwa manufaa ya magufuri ni kwa manufaa ya Taifa na wananchi wake.
Nch hii ukitaka kuwaonea huruma waliojenga ktk hifadhi ya barabara kamwe hatutafika mahali popote pale