Magufuli aliahidi kitu gani katika elimu yetu?

Magufuli aliahidi kitu gani katika elimu yetu?

Deadbody

JF-Expert Member
Joined
May 30, 2015
Posts
4,274
Reaction score
6,632
Wanabodi!

Hatimaye uchaguzi mkuu umeisha na Dr Magufuli John Pombe Joseph ametangazwa kuwa mshindi wa kiti cha urais.

Katika mikutano ya mgombea urais anayeungwa na vyama vinavyounda umoja wa katiba ya wananchi(ukawa) kwamba atatoa elimu bure na kuwafanya wanafunzi wengi kuwa matumaini nae kutoka na umaskini miongoni watanzania.

Hivyo kushindwa kwa mh.lowassa kumepelekea kupotea kwa matumaini kwa wanafunzi wengi.matumaini hayo yameyayuka kutokana na maono kwamba ccm ndo ileile.

Je rais wetu huyu wa awamu ya 5 aliahidi nini kuhusiana na elimu yetu ili tuendelee kuyaishi na kuamini kuwa ipo siku atafanya mana ameseme HAPA KAZI TU.

Karibuni kwa michango yenu wakuu.
 
Aliahidi tutapata mikopo wote..... Mi nasubili nione.kwa sababu mpka sasa loanboard kimya...ni jumatatu tu vyuo vinafunguliwa
 
Ninacho kumbuka ni kuwa
  • Elimu ya Msingi hadi kidato cha nne itakuwa bure
  • Kwa Elimu ya juu, watu wanapewa mikopo na itakuwepo kwa wakati sio hadi wagome. Nchi za ulaya wanafanya hivyo pia.
  • Pia alisema shule zetu hasa za kata zitapitiwa upya ziwe na vifaa stahiki
  • Ila cha muhimu pia, kutakuwa na mkakati maalam wa kujenga nyumba za waalimu awamu kwa awamu
  • Stahiki za waalimu zita angaliwa ili wawe na ari ya kufundisha na kuipenda kazi yao
  • Kuna maswala madogo madogo kama ya madawati ambayo ni uzembe tu wa wilaya na mikoa husika..
Uliza kingine
 
Alisema pia akiingia atawafundisha adabu TANESCO na hili nalisubiria lifanyike ASAP kwani halina mlolongo mkubwa kama la elimu
 
alituahaidi ajira kwa vijana haitakuwa ya kuyumba yumba kwa jambo hili na hamu nalo sana kuliona utekelezwaji wake
 
Doing the same thing over and over again....and expecting different results, Tanzanians we are not serious.
 
Ninacho kumbuka ni kuwa
  • Elimu ya Msingi hadi kidato cha nne itakuwa bure
  • Kwa Elimu ya juu, watu wanapewa mikopo na itakuwepo kwa wakati sio hadi wagome. Nchi za ulaya wanafanya hivyo pia.
  • Pia alisema shule zetu hasa za kata zitapitiwa upya ziwe na vifaa stahiki
  • Ila cha muhimu pia, kutakuwa na mkakati maalam wa kujenga nyumba za waalimu awamu kwa awamu
  • Stahiki za waalimu zita angaliwa ili wawe na ari ya kufundisha na kuipenda kazi yao
  • Kuna maswala madogo madogo kama ya madawati ambayo ni uzembe tu wa wilaya na mikoa husika..
Uliza kingine

Hilo hapo la mkopo alisema mkopo utatoka kwa wakati na sio kua wanafunz wote watapewa mikopo
 
Pia alisema ole wao wakuu wa shule watakaotafuna michango ys shule....na kabla elimu itakuwa bure kuanzia chekechea hadi kidato cha nne !
 
Mimi nasubiri tu ahadi kutekelezwa kwani hakuna linaloshindikana chini ya jua kama kuna mipango thabiti.
 
Tutaisoma Namb Mwaka Huu.Tumepewa Nafasi Ya Kusoma Bure Tumeichezea Wenyewe Afu Saiv Tulia Lia Tu Mara Mikopgo Mara Sijui Bodi..Kilio Na Kicheko Cha Loan Kpo Njiani Wakuu.
 
Alisema HAPA KAZI TU Maana yake ni kwamba kila MTU ATAKULA KWA JASHO LAKE,SO Uctegemee cha ajira wala mikopo miaka mitano mtaisoma namba
 
Back
Top Bottom