Magufuli aikonga sekta ya afya

Magufuli aikonga sekta ya afya

Mariswaga

JF-Expert Member
Joined
Aug 25, 2015
Posts
201
Reaction score
2
MAGUFULI AIKONGA SEKTA YA AFYA
Sekta ya afya ni muhimu na nyeti mno kwakua inagusa kila hatua ya maisha ya mwanadamu. Kwa mfano mtu hawezi kufanya vema kazi yake kama hana afya nzuri hata Mh. Rais hawezi kutekeleza majukumu yake vizuri kama hana afya imara.

Kwa kuliona hili Mh. Magufuli ameamua kuja na sera bora ya afya itakayomfanya kila Mtanzania kuwa na uhakika na afya yake hatimaye kumuwezesha kufanya kazi zake vema na kuinua uchumi wa nchi. Haina maana kwamba haya aliyoadhimia kuyafanya Mh. Magufuli hayakuonekana na viongozi waliotangulia, la hasha bali kila kiongozi hutatua tatizo sugu zaidi lililopo kwenye kipindi chake cha utawala.
Mh. Magufuli ameamua kufanya yafuatayo ili kuhakikisha afya za Watanzania zinaimarika:-
Kuandaa utaratibu utakaomuwezesha kila Mtanzania kupata bima ya afya kwajili ya kupata matibabu hata ule wakati ambao hana pesa kabisa
Kuongeza idadi ya waganga na wauguzi pamoja na kuimarisha upatikanaji wa dawa na vifaa tiba katika vituo vyote vya tiba. Sasa wananchi wanakaribia kusahau suala la kuambiwa wakapate huduma fulani kwenye hospitali binafsi kisha warejee kwenye hospitali ya serikali kuendelea na tiba.
Sambamba na hilo Mh. Magufuli ameapa kupambana na watumishi wa sekta ya afya wanaohujumu upatikanaji wa dawa kwenye hospitali za serikali pamoja na vituo vya afya; ameyasema hayo akiwa kwenye mkutano wa hadhara wa kuwaomba kura Wananchi wa Katavi.
Pia Mh. Magufuli amedhamiria kuboresha makazi ya wahudumu wa sekta ya afya hususani vijijini pamoja na kupambana na madawa ya kulevya ili kutengeneza nguvu kazi bora ya taifa.
Ni ushauri wangu kwa Watanzania wote tumchague Mh. Magufuli ili aweze kutekeleza haya na hatimaye kupata maendeleo kwa kasi zaidi
Mungu ibariki Tanzania
Mungu mbariki Magufuli
#Hapa kazi tu
 
na moyo wako umekongwa? je ushakongwa mara ngapi bila kutimiziwa? jibu baki nalo
 
Nani hakuahidi haya wakati wa kampeni zake??
 
Safi sana.huyu ndie rais wa Tanzania

Mavi yake..ahadi ngapi kama hizo..mbona hazikutekelezwa....50yrs+..nyimbo zilezile..tumechoka kudanganywa..kwanza sisi ni wapumbavu na malofa...safari hii mtauona mziki..hamtupati n'goooo..lowassa nanatosha!
 
MAGUFULI AIKONGA SEKTA YA AFYA
Sekta ya afya ni muhimu na nyeti mno kwakua inagusa kila hatua ya maisha ya mwanadamu.
Kwa kuliona hili Mh. Magufuli ameamua kuja na sera bora ya afya itakayomfanya kila Mtanzania kuwa na uhakika na afya yake hatimaye kumuwezesha kufanya kazi zake vema na kuinua uchumi wa nchi. Haina maana kwamba haya aliyoadhimia kuyafanya Mh. Magufuli hayakuonekana na viongozi waliotangulia, la hasha bali kila kiongozi hutatua tatizo sugu zaidi lililopo kwenye kipindi chake cha utawala.

Msituletee utani.

Wakati huu ndipo mnajua Afya ni muhimu??


Wakati wa Mgomo wa madaktari Serikali si ilisema madaktari wanataka fedha tu na madai yao hayana mantiki?

Si ni Magufuli huyu huyu aliyesema madaktari wanaiba dawa na kupeleka katika maduka yao despite serikali "kununua dawa za kutosha" na kusema atawashughulikia?
-Hivi hospitali zote kuanzia hospitali ya Taifa(MNH) wanaweza kuwa mafaktari wezi hadi zahanati vijijini?
-Vitanda, mipira ya kujikinga, navyo wanaviiba?
-Hivi kama wanaiba kweli, wameshindwa kuwakamata?
-Kama ni kweli wameshindwa kuwakamata kwanini walioshindwa wako kazini hadi sasa?


Tatizo sugu? leo? Usugu upi, madawa, wataalamu wachache, vitendea kazi kukosekana, huduma mbovu au usugu gani unaoungelea?

BIMA? iko wapi mifuko ya bima iliyokuwa ikiwasaidia wananchi mf. Community Health Insurance Fund, CHIF na nyinginezo?

Bima ya afya: Unajua ni dawa ngapi zisizotolewa na mfuko wa bima wa taifa(NHIF) despite mfanyakazi kukatwa kila mwezi?

Afya ya mtanzania imeshachezewa(kuanzia afya ya Akil), hata wao kwenda kutibiwa nje si kwamba wanapenda ila wanajua hali halisi, so msilete porojo hapa.

Tusubiriane tu, Oktoba 25.
 
Miaka 50+ tunadanganywa hivyo hivyo na bado mazuzu yanashangilia? Ina maana Marais waliopita wote walikuwa vilaza ila yeye ndio mwenye akili ya kufanya hayo?
 
Miaka 50+ tunadanganywa hivyo hivyo na bado mazuzu yanashangilia? Ina maana Marais waliopita wote walikuwa vilaza ila yeye ndio mwenye akili ya kufanya hayo?

Zambia walimchukia Kaunda na chama chake kwa madai ya ufisadi mkubwa! Walimuondoa Kaunda, waliofuata wakawa na njaa zaidi chini ya uongozi wa Chiluba, hali ya Zambia ilikuwa mbaya zaidi kipindi cha Chiluba kuliko kipindi cha Kaunda. Hadi leo uchumi wa Zambia uko hoi!

Lowassa anafahamika vizuri, hata Baba wa Taifa aliweka wazi kuwa Lowassa si safi na Watanzania wanalijua hilo, leo anaomba kwenda Ikulu kwa gharama kubwa akitumia fedha zake na za maswahiba wake, hivi akiingia Ikulu hali ya uchumi wa Tanzania itakuwaje?

Nakubaliana kabisa na hoja kuwa CCM imeshindwa kuleta mabadiliko kwa zaidi ya miaka 50 na Lowassa na wafuasi wake ni sehemu ya kushindwa huko, je wakiwa UKAWA watakuja na lipi jipya?
Je, hawatakuwa busy kurejesha fedha zao walizotumia katika mchakato wa kupata nafasi ndani ya CCM, kuwahonga Mbowe et al., na gharama za uchaguzi mkuu kwa ujumla?

Upinzani wa kweli umetupwa nje kwa nguvu ya fedha, ee Mungu isaidie Tanzania, amina.
 
Mavi yake..ahadi ngapi kama hizo..mbona hazikutekelezwa....50yrs+..nyimbo zilezile..tumechoka kudanganywa..kwanza sisi ni wapumbavu na malofa...safari hii mtauona mziki..hamtupati n'goooo..lowassa nanatosha!

Magufuli ndie pekee atakayeweza kutukomboa waTz. Jamaa jembeeeeeeeeeee
 
Miaka 50+ tunadanganywa hivyo hivyo na bado mazuzu yanashangilia? Ina maana Marais waliopita wote walikuwa vilaza ila yeye ndio mwenye akili ya kufanya hayo?
na huyo mnayemnadi amekuwemo kwenye serikali zaidi ya miaka 30.. na hakufanya hayo. Mnadhani ataweza kuyafanya. Saiv kama mnadhalni kuna upinzani mnajidanganya. Ni ccm vs ccm. So hakuna upande wa kumsema upande mwingine. Tuchagua tu nani anaweza kufanya kazi zetu vizuri.
 
Back
Top Bottom