barafuyamoto
JF-Expert Member
- Jul 26, 2014
- 32,323
- 29,586
Inauma sana pale Masawe apokufunga alafu anakuja fungwa kirahisi na Bocco.Mtanange wa leo wa ligi kuu bara, uliopigwa katika dimba la Kambarage pale Shinyanga, Simba ameibuka na ushindi wa goli 2-0. Hongereni kwa hilo.
Ila kuna kitu kinanipa mashaka, magoli waliyofunga ni marahisi sana, yaani wamerahisishiwa namna ya kupata magoli hayo, kwa kifupi ni kama kupigana na mlevi aliyepo chakari.
Goli la kwanza ni la penati. Mpira umemgusa mchezaji wa Stand begani, refarii akakimbilia kutenga tuta, na John Bocco akafunga.
Goli la pili, offside ya wazi kabisaaaaa, John Bocco alibaki pekee yake na kipa halafu yule kipa sikuelewa ni kwa namna gani mpira uliompitia karibu ashindwe walau hata kuugusa. INASHANGAZA!
Inaonekana Simba kwa sasa wanapeleka miamala pande mbili, kwa wasimamizi wa mchezo bila kusahau kwa mabeki na magolikipa wa timu pinzani. Hebu kumbuka walau goli la faulo alilofungwa kipa wa Lipuli juzi, ni AIBU.
Mpira wetu bado una safari ndefu sana.
Nawasilisha...
Vipi ile penati refa kapeta ya juma rashidi? Goli la pili angalia vizuri kuna jamaa alikuwa analinda goli nguzoni ndiye aliyemuweka boko onside.