Maghufuli ''is next level''

Tanzaniaist

Senior Member
Joined
Nov 29, 2011
Posts
161
Reaction score
158
Nani Kama John Pombe Magufuli..,
1.Kiongozi mchapakazi anayejituma
2.Kiongozi ambaye hajajilikimbizia mali, tujiulize magufuli anamiliki kampuni gani..?
3.Anatanguliza mbele maslahi ya Taifa, na maslahi ya chama. kwani hajihusishi na makundi kuleta mgawanyiko katika chama
4.Kiongozi anyesimamia ukweli na mwenye msimamo thabiti..!
5.Kiongozi huyu hatumii pesa kujisafisha au kujijengea njia kuwa raisi 2015, zaidi ya uongozi wake bora na sio kumwaga fedha na kuunda mitandano au makundi
6.Anajiamini (self confident) hatawachekea mafisadi na wazembe serikalini, na hata wananchi wavivu na wabishi mfano wa kigamboni waliombishia kuhusu nauli, watanzania tunapendwa kubebwa kila wakati kwenye sehemu ambako hatubebeki, ndio chanzo kikubwa cha umaskini
7.Ni mfuatiliaji mzuri wa matatizo, kama alipanda lori na kujifanya abiria kukamata wanaochukua rushwa kwenye mizani,..kiongozi gani ambaye atakuwa tayari kufanya jambo kama hili serikalini..? zaidi ya kuandaa warsha na vikao kutatua matatizo

Napenda kumfananisha John Magufuli na Paul Kagame, kwa style zao za uongozi bora na kupambana na ufisadi,rushwa na hujuma dhidi ya taifa...!

Magufuli ameweza kuwa mtu pekee mwenye kukiletea heshima chama cha mapinduzi (ccm), kama kufanikisha ushindi Igunga,na pia atakuwa ndio striker kwnye uchaguzi Arumeru..,kweli anatimiza Ilani ya CCM kwa asilimia 100..!

Watanzania Kama tunapenda maendeleo, tumpe moyo viongozi kama hawa wenye kujituma na kutetea maslahi ya Taifa...!
Ningepanda nishauri Mh.John Magufuli apewe Ulinzi maalumu maanake wasije wakamfanyia mabaya hasa wale wanaokamia urasi 2015..! kwakuwa wanaamini ni tishio kwao
 
Hata kama ni aina fulani ya kampeni lakini nafikiri iko sawa maana inaendana na kauli ya wahenga "Chema chajiuza, kibaya chajitembeza." Mafisadi ni lazima watumie nguvu nyingi (pamoja na pesa) maana hawakubaliki, bali wachapa kazi na waadilifu kama Dr. J. P. Magufuli matendo yao yanawasemea.
 
unakumbuka magari ya govt watu walikua wamejimilikisha!amebuni mfumo mpya wa namba za magari,anawapa tenda suma jkt
 
hakuna waziri muongo kama magufuli..kwa wasio mjua ndio mnaona ana chapa kazi..kelele nyiingii lakini hamna kitu pale..wale wale tu!!
huyu jamaa ni waziri wa vyombo vya habari anavyopenda sifa ni muongo wa kutupwa hafai hata ujumbe wa nyumba kumi ameshalitia taifa hasara sana kwa maamuzi yake ya kibabe na machafu yasiozingatia maadili ya uongozi
 
Hakuna waziri muongo kama Magufuli..kwa wasio mjua ndio mnaona ana chapa kazi..kelele nyiingii lakini hamna kitu pale..wale wale tu!!

Mdau anamfahamu Magufuli kwa aliyoyataja hapo juu. Wewe unayemfahamu kwa upande mwingine weka hadharani unayoyafahamu tumpime. Hatutaki porojo hapa lete facts.
 
sawa anafaa, lakini jk anamkubali!? ...je anatokea 'Pwani' maana vijana walishasema kuwa safari hii ni zamu ya hili eneo
 
Hiyo namba sita ni kwamba anajihami na sio kujiamini. We kila kitu lazima ataje ccm? Si ajabu hata mkewe alipewa na ccm
 
Hakuna waziri muongo kama Magufuli..kwa wasio mjua ndio mnaona ana chapa kazi..kelele nyiingii lakini hamna kitu pale..wale wale tu!!

Acha kuropoka tuu,kAmA unAsema mtu hafAi nai lazimA utoe sabAbu kwA kufAfAnua kwa kinA kwanini unAsemA ivo.Sio kutuAchA pending bilA ku support hojA yako,Sio Facebook hapa.AlaAaa
 
huyu jamaa ni waziri wa vyombo vya habari anavyopenda sifa ni muongo wa kutupwa hafai hata ujumbe wa nyumba kumi ameshalitia taifa hasara sana kwa maamuzi yake ya kibabe na machafu yasiozingatia maadili ya uongozi

Labda ungetaja hasara alizolitia taifa nasi tuzijue
 
jana kafungua stend pale mbezi
haina hata choo.
 
mnyonge mnyongeni lakini haki yake apewe. Jamaa anachapa kazi kweli kweli.
 
Kama mtu una argument yako hafai basi tupe facts ulizonazo..mkuu apo katoa facts anazozijua kwamba ni kiongozi mzuri,why dnt u draft urs kwamba hafai?
Achaneni porojo bwana,ss uyo anaefaa ni nani mleteni apa nayeye tumjadili sio mnakua negative tu bila sababu watanzania bwana!!
 
Ni mtu wa kawaida tu.

ukitaka kujua ubora wa pombe magufuli nenda brbr ya morogoro
saa kumi na moja jioni au asubuhi saa kumi na mbili.
 

he is my mentor
 
Ukweli ni kwamba Magufuli ni mchapakazi, mfutiliaji, anajiamini, hana woga wala longolongo, haoni haya kuwaonea haya wazembe, wavivu, wezi na wadanganyifu. Katika CCM ya leo, Magufuli anaweza kabisa kuuzika na kukubalika kwa wananchi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…