Magendo ya mamilioni ikiwemo magari yanaswa Rombo, baadhi kutaifishwa

JMP Mchungu

Member
Jun 30, 2015
49
125
Bidhaa za magendo na Magari ya kifahari zaidi ya 20 vimekamatwa katika mpaka wa Holili uliopo wilaya ya Rombo

=====

Gabriel Mwangozi, meneja TRA mkoa wa Kilimanjaro amesema magari hayo yanatofautiana makosa, mengine yalibeba magendo ambapo mengine yatatozwa faini na mengine yakitaifishwa kutokana na urudiaji wa kosa au kuangalia ukubwa wa kosa lenyewe.

"Magari mengine, watu wengine waliingiza tu bila kujua. Anaingiza analeta, amenunua tu huko gari lake, kwa mfano ile Amarok, kuna kijana alikuwa anasoma South Africa. akaona amependa gari akainunua akajua akishanunu akija nalo hapa tu haina shida na akawa anaitembelea, likawa limekamatwa kwa sababu muda ule uliokuwa utatakiwa ukawa umeshapita na taratibu ambazo alitakiwa afanye hakuzifanya" Alisema Gabriel

Mkuu wa wilaya ya Rombo, Dr. Athuman Kihamia anasema licha ya kukamata bidhaa za magendo bado haijawa dawa kwa waingizaji wa bidhaa hizo.

Pia wapo wanaojaribu kutumia wafanyakazi hasa wa chini kuwarubuni kwa njia moja au nyingine. Dr. Kihamia kasema wote hawako salama na kusema hata wanaopitisha bangi wanawafahamu na kama wamefanikiwa kupita bahati mbaya wasiwadanganye wenzao kwamba kunapitika.
 
Ukiona hakuna magendo mpakani jua hakuna biashara hapo, Border lazima kuwe na harakati na ndio maana kuishi border ni zaidi ya elimu ya chuo kikuu, hiwezi kumfaninisha mtoto wa tunduma na mtoto wa chato geita, mtoto wa border ni mjanja kuanzia akili hadi kufikiri maana border hakuna shamba ili ule akili inabidi icheze
 
Na ndio maana serikali inajitahidi kupambana nayo ili uchumi wa nchi usifeli Mkuu.
Umeelewa nilichoandika?Nimesema ya kwamba magendo ni matokeo ya uchumi wa nchi kufeli,maana yake ukitaka kuzuia magendo unapaswa kuimarisha uchumi uwe rafiki kwa kila mtu ikiwa ni pamoja na wafanyabiashara na siyo kutuma TRA mipakani.
 
Bidhaa za magendo na Magari ya kifahari zaidi ya 20 vimekamatwa katika mpaka wa Holili uliopo wilaya ya Rombo

=====

Gabriel Mwangozi, meneja TRA mkoa wa Kilimanjaro amesema magari hayo yanatofautiana makosa, mengine yalibeba magendo ambapo mengine yatatozwa faini na mengine yakitaifishwa kutokana na urudiaji wa kosa au kuangalia ukubwa wa kosa lenyewe.

"Magari mengine, watu wengine waliingiza tu bila kujua. Anaingiza analeta, amenunua tu huko gari lake, kwa mfano ile Amarok, kuna kijana alikuwa anasoma South Africa. akaona amependa gari akainunua akajua akishanunu akija nalo hapa tu haina shida na akawa anaitembelea, likawa limekamatwa kwa sababu muda ule uliokuwa utatakiwa ukawa umeshapita na taratibu ambazo alitakiwa afanye hakuzifanya" Alisema Gabriel

Mkuu wa wilaya ya Rombo, Dr. Athuman Kihamia anasema licha ya kukamata bidhaa za magendo bado haijawa dawa kwa waingizaji wa bidhaa hizo.

Pia wapo wanaojaribu kutumia wafanyakazi hasa wa chini kuwarubuni kwa njia moja au nyingine. Dr. Kihamia kasema wote hawako salama na kusema hata wanaopitisha bangi wanawafahamu na kama wamefanikiwa kupita bahati mbaya wasiwadanganye wenzao kwamba kunapitika.


Naona mwenye Amarok anatetewa hapa...atalipa fine mambo yanaenda......wengine mwendo wa kutaifishwa
 
Back
Top Bottom