mkurugenzi1
Senior Member
- Mar 22, 2009
- 122
- 28
tujuzane zaidi kuhusu hilo hapo juu....
mie sioni tatizo, wewe ulitaka wazunguke nchi nzima kwa miguu au?
Hakuna ambaye angependa wapate tabu maana tunatarajia kazi nzuri toka kwao kwa ajili ya Tanzania mpya. Ila kama kweli wamenunuliwa magari mapya kuna maswali ya kujiuliza je, huko serikalini hakuna magari mazuri ambayo yangeweza kutumika? au ofisi za wilaya au mikoa hakuna magari ambayo yangeweza kusaidia hawa wateule kufanya kazi katika mkoa husika? Kama yapo tungeweza kuokoa fedha nyingi maana hapo unazungumzia kwa wastani mil 120 x 30.
Wagonjwa watapanda bajaji,Eh nilidhani ni magari ya kubebea wagonywa kumbe ni yakatiba mpya na mchakato ukiisha nani atayachukuwa
Ilibidi wanunue gubasi, liwabebe basi. Hayo mengine anasa.
JF
Tusiweke punda nyuma ya Mzigo hautaondoka! Kwanza hawajatengeneza kanuni, tume haina Hadidu za rejea. Hata ukamilifu wake bado lakini LUkuvi anakimbilia kuagiza Magari. Kwa ujinga wangu nashauri tune itumie public transport, Usafiri wa kawaida ili waweze kuchukua mawazo ya watu hata kwenye mijadala ndani ya daladala.
Tatizo ni kwamba kuna wajumbe wa tume ambao hata kutembea ni tabu. Huu utamaduni wa kununua Magari uko kwenye damu ya Watanzania . Look at the huge number of DFP vehicles on the road.
Pesa nyingi zinatumika kwenye Magari rejea taarifa ya CAG. Magari yanakula sehemu kubwa sana ya pato la Watz right from the family level. This is the problem.
Tungeimarsha mfumo wa Usafiri wa Reli, anga na hata mabasi hakuna haja ya Kila mtu/ mradi kununua gari. Tutoke hapo!
Charity begins at home siku moja toka nje uaangalie ukubwa wa msafara Rais Kiwete unakuwa msururu Magari yasiyopungua thelathini. Hayo Magari wanatakiwa Kila mjumbe na gari lake this is more than crazy!
Basi liwabebe waandamane kama kumbikumbi? likiwapata ajali wote kwisha!!