Mafuta machafu yarudishwa kutoka rwanda

Wana JF kuna mafuta machafu yaliyoingizwa nchini na TPDC na kuyauza katika nchi za Rwanda, Burundi na Uganda yamerudishwa nchini kwasababu mafuta hayo ni machafu kupindukia na nimepita ktk mpaka wa Kabanga nimekuta kuna malori kama matano ikabidi niende Rusumo nikakuta pia malori mawili moja la kitanzania na lingine la kinyarwanda mali ya Merez la kitanzania ni kampuni ya Bridgeway na nimeambiwa yapo mengine Kampuni ya Worldoil na Liberty yanakuja.

Source mimi mwenyewe. Pia napendekeza mwandishi wa habari aje apige kambi hapa awarushie hiyo taalifa live bila chenga
Aibuuuuuuuuu tanzania aibuuuu kwa serikali aibu kwa TBS na TPDC

hii ni taarifa nzuri sana kwani kuna ndugu zetu Madereva wamehamia Rwanda toka MWezi Feb 2012, ambao walipeleka haya mafuta.

Familiya zao zinaishi kwa shida sana.

Nashauri TBS wale wote waliohusika na kupima haya mafuta na kusema ni masafi wachukuliwe hatua.



MIZAMBWA
NABII MTARAJIWA!!!
 
Mbutalikasu, ni kweli TBS ndo wenye mamlaka ya kuruhusu mafuta safi kuingia nchini. Waliruhusu mafuta machafu mara kadhaa hadi makampuni yakalalamika. Kuona hivyo, wiki mbili zilizopita TBS wakatangaza kuwa mafuta yenye ethanol hayakubaliki, katika kujikosha. Makampuni yakaijia juu kwa kusema wazi kuwa TBS ndo iliruhusu mafuta hayo na mchakato wa kisheria unatarajiwa kuchukuliwa baada ya uchunguzi wa sampuli zote kukamilika.
Ila si sahihi kusema mafuta hayo yaliletwa na TPDC. Yaliletwa kwa tenda na Augusta.

Hivi Augusta ni nani na ana misuli kiasi gani cha kuvuruga mambo kiasi hiki? Ile wizara ya nishati na madini sijui bwana...naona huruma kwa watanzania haipo tena.
 
minzabwa ni kweli kuna madreva wana miezi 3 Rwanda mpaka leo nasikitika sana kuona serikali ipo kimya mpaka leo madreva wanateseka ila niwasihi tu wadau tulichukulie hili suala siriaz kwakweli nimebahatika kuona hayo mafuta ni hatari kubwa sana jamani ni tope kama la volcano na ile petrol siyo ni HATARI....AIBU....
 
Back
Top Bottom