Maficho ya Rais Magufuli Chato yawatia kiwewe Mafisadi, CHADEMA na Kenya

Lizaboni

JF-Expert Member
Feb 21, 2013
33,895
20,392
Wadau, habari iwe kwenu.

Rais Magufuli yupo Chato ambako ametembelea kwa mara ya kwanza tangu achaguliwe kuwa Rais. Akiwa Chato, Rais Magufuli pamoja na mambo mengine amechangamana na ndugu, jamaa na marafiki akiwemo rafiki wake wa karibu, Raila Odinga ambapo wametumia nafasi hiyo kubadilishana na kupanuana mawazo.

Ziara ya Raila huko Chato hakika imewashtua wengi ikiwemo Serikali ya Kenya. Ikumbukwe kuwa Raila anamtembelea Rais Magufuli katika kipindi ambacho Serikali ya Kenya inafanya juhudi kubwa kuishawishi Uganda isitishe mpango wake wa kushirikiana na Tanzania kujenga bomba la Mafuta kutoka Ziwa Albert hadi Bandari ya Tanga juhudi ambazo hazijazaa matunda.

Aidha, Mpaka sasa CHADEMA hawajafanikiwa kujua sababu za Rais kwenda kupumzika Chato katika kipindi ambacho utumbuaji wa majipu umeshika kasi na bado hajamaliza kuunda Serikali yake ambapo hajafanya uteuzi wa nafasi mbalimbali zikiwemo nafasi za Wakuu wa Wilaya, Makatibu Tawala wa Mikoa, wakurugenzi wa Halmashauri nk. Wapo wanaobeza uamuzi huo wa Rais kwenda kusalimia kwao Chato huku wakihoji ikiwa Rais anaitendea haki kauli mbiu yake ya Hapa Kazi tu.

Kinachowashangaza zaidi CHADEMA na mawakala wao ni kasi ya Polisi na TAKUKURU katika kutekeleza majukumu yao. Katika kipindi cha Rais kuwa nje ya Ikulu, TAKUKURU wamefanya maamuzi mazito ya kumfikisha mahakamani aliyekuwa Kamishna wa TRA na wenzake ambapo mpaka sasa wapo rumande. Pia TAKUKURU wamewafikisha mahakamani wabunge kadhaa wa CCM na wengine wapo njiani kwa tuhuma za ufisadi. Ikumbukwe pia kuwa Rais akiwa Chato ametangaza kupunguza mishahara ya watendaji wakuu wa serikali na mashirika ya umma ambao wanalipwa mishahara mikubwa ya hadi milioni 40 ambapo amesema kuwa ukomo wa mishahara utakuwa milioni 15 tu.

Mpaka sasa Rais Magufuli kila analofanya Rais linampa credit na kumpandisha chati. Wapinzani wanaumia sana kuona hivyo. Fimbo pekee wanayoendelea kuishikilia ni sakata la MCC ambalo hata hivyo linaonekana kupungua nguvu kutokana na wananchi wengi kusisitiza kuwa Tanzania ifike mahala tuachane na misaada bali tusimame kwa miguu yetu.
 
Mkuu, si kweli. Binafsi ni mpinzani na napenda utendaji kazi wa J.P.M ingawa siridhishwi
na yale yanayotokea Zanzibar.
Mkuu, hujasomeka nini umemaanisha. Kwani kuna mahala nimekugusa?
 
Mkuu, hujasomeka nini umemaanisha. Kwani kuna mahala nimekugusa?
Kwamba anayofanya Magufuli yanampaisha na kumpa chati hivyo Wapinzani Tunaumia
hilo si kweli binafsi kama anayofanya ni mazuri siwezi kuumia bali nitafarijika.
 
Ha ha ha ha haaaa! Kabla ya MCC mlisema basi hatutokua Na hoja nyingine ya kuzungumza! Sasa jiandae kuna nyingine nyingi zinakuja zitakazo wanyong'onyeza!

By the way CDM imekujaje Ktk issue ya Mapumziko ya Magufuli?

Halafu kutumbuliwa watumbuliwe CCM hofu tuwe nayo sisi?

Hilo tu la wabunge wenu kufikishwa Mahakamani Kwa tuhuma nzito Zenye kuaibisha hamjisikii vibaya?

Ngoja wale 18 wengine wapandishwe kizimbani Ndio utakaposhangaa Na kujua Kama Kweli CCM Hakuna mzalendo!

Stay away from CDM please!
 
Kwamba anayofanya Magufuli yanampaisha na kumpa chati hivyo Wapinzani Tunaumia
hilo si kweli binafsi kama anayofanya ni mazuri siwezi kuumia bali nitafarijika.
Ooooooh! Nisamehe Mkuu kwa hilo. Kwa comment yako hii nadhani wewe si mpinzani bali ulichukiwa tu na utendaji mbovu wa serikali. Kwa vile Rais Magufuli anarekebisha mambo, umeridhika kabisa. Hongera sana. Hata Lowasa anaamini kuwa anachofanya Magufuli ni sahihi ila anashindwa tu kutamka hadharani kwa kuogopa kuchekwa
 
Kwa kifupi Mh Pombe anawatisha sana Ccm kuliko wapinzani.. Bado ridhione na wengine wengi vigogo wa ccm wataswekwa lupango na watu watashangaa
 
Ha ha ha ha haaaa! Kabla ya MCC mlisema basi hatutokua Na hoja nyingine ya kuzungumza! Sasa jiandae kuna nyingine nyingi zinakuja zitakazo wanyong'onyeza!

By the way CDM imekujaje Ktk issue ya Mapumziko ya Magufuli?

Halafu kutumbuliwa watumbuliwe CCM hofu tuwe nayo sisi?

Hilo tu la wabunge wenu kufikishwa Mahakamani Kwa tuhuma nzito Zenye kuaibisha hamjisikii vibaya?

Ngoja wale 18 wengine wapandishwe kizimbani Ndio utakaposhangaa Na kujua Kama Kweli CCM Hakuna mzalendo!

Stay away from CDM please!
Upinzani wa Tanzania ni kichekesho kweli. Yaani wenyewe una siasa za matukio na mihemko. Ndo maana mnapigwa kila uchaguzi unapofanyika. Hamna dira wala Mwelekeo. Sidhani kama mnaendelea kuzungusha mikono kuashiria mabadiliko
 
Wadau, habari iwe kwenu.

Rais Magufuli yupo Chato ambako ametembelea kwa mara ya kwanza tangu achaguliwe kuwa Rais. Akiwa Chato, Rais Magufuli pamoja na mambo mengine amechangamana na ndugu, jamaa na marafiki akiwemo rafiki wake wa karibu, Raila Odinga ambapo wametumia nafasi hiyo kubadilishana na kupanuana mawazo.

Ziara ya Raila huko Chato hakika imewashtua wengi ikiwemo Serikali ya Kenya. Ikumbukwe kuwa Raila anamtembelea Rais Magufuli katika kipindi ambacho Serikali ya Kenya inafanya juhudi kubwa kuishawishi Uganda isitishe mpango wake wa kushirikiana na Tanzania kujenga bomba la Mafuta kutoka Ziwa Albert hadi Bandari ya Tanga juhudi ambazo hazijazaa matunda.

Aidha, Mpaka sasa CHADEMA hawajafanikiwa kujua sababu za Rais kwenda kupumzika Chato katika kipindi ambacho utumbuaji wa majipu umeshika kasi na bado hajamaliza kuunda Serikali yake ambapo hajafanya uteuzi wa nafasi mbalimbali zikiwemo nafasi za Wakuu wa Wilaya, Makatibu Tawala wa Mikoa, wakurugenzi wa Halmashauri nk. Wapo wanaobeza uamuzi huo wa Rais kwenda kusalimia kwao Chato huku wakihoji ikiwa Rais anaitendea haki kauli mbiu yake ya Hapa Kazi tu.

Kinachowashangaza zaidi CHADEMA na mawakala wao ni kasi ya Polisi na TAKUKURU katika kutekeleza majukumu yao. Katika kipindi cha Rais kuwa nje ya Ikulu, TAKUKURU wamefanya maamuzi mazito ya kumfikisha mahakamani aliyekuwa Kamishna wa TRA na wenzake ambapo mpaka sasa wapo rumande. Pia TAKUKURU wamewafikisha mahakamani wabunge kadhaa wa CCM na wengine wapo njiani kwa tuhuma za ufisadi. Ikumbukwe pia kuwa Rais akiwa Chato ametangaza kupunguza mishahara ya watendaji wakuu wa serikali na mashirika ya umma ambao wanalipwa mishahara mikubwa ya hadi milioni 40 ambapo amesema kuwa ukomo wa mishahara utakuwa milioni 15 tu.

Mpaka sasa Rais Magufuli kila analofanya Rais linampa credit na kumpandisha chati. Wapinzani wanaumia sana kuona hivyo. Fimbo pekee wanayoendelea kuishikilia ni sakata la MCC ambalo hata hivyo linaonekana kupungua nguvu kutokana na wananchi wengi kusisitiza kuwa Tanzania ifike mahala tuachane na misaada bali tusimame kwa miguu yetu.
Ukiwa (wapinzani) hawana hoja. Ngoja Rais afanye kazi
 
Unaikalia Politiki Asubuhi na mapema yote kazi hautafuti utakula nini ?
 
hizi mada nyingine ni kukosa cha kuandika huku mikono inawasha. haya tumesoma ulicho post....
ila hakuna cha ajabu rais kwenda kwao...
hakuna ajabu kutembelewa na rafiki yake...
hakuna ajabu rais kupumzika...
rais hakuwa 'mafichoni' kama ulivyo andika...
anachofanya rais ni wajibu wake, 'sio extraordinary'
 
CfL2x5eWQAAvDej.jpg
 
Back
Top Bottom