Madiwani wa kata za Kigamboni wawasaliti wananchi wao

SAVERA

Senior Member
Jun 25, 2013
114
42
Madiwani wa Kata zilizo ktk mpango wa ujenzi wa mji mpya yaani KDA wamekubali kupofushwa macho na Wizara na waziri Mama Tibaijuka kwa kukubali kusafirishwa na Wizara eti kwa lengo la kwenda kujifunza juu miji mingine inavyojengwa.

Mwaliko huo pia ulikuwa ni pamoja na Mbunge wa Kigamboni Dr.Ndungulile,lakini hongera kwa Mbunge huyu alikataa ofa hiyo.

Kwa nini tunasema ni usaliti,kwenye kikao cho Full Council Temeke kikiongozwa na Meya ilionekana kuwa ofa hiyo si halali kwani Council haina taarifa ila alitafutwa kila diwani na kupewa ofa hiyo kama yeye.Na makubaliano yakawa ni kwamba wasiende mpaka wizara,ilete taarifa kwenye council na kueleza faida na hasara za safari hiyo,na lengo lake.

Lakini cha kushangaza madiwani hao wakakubaliana wao pembeni na kuamua kukubali ofa hiyo na kusafiri zao kwenda China na kwingineko eti kujifunza miji inavyojengwa.

La kujiuliza ni je kweli wakirudi watakuwa na ujasiri wa kusimama pamoja na wananchi na kukataa matakwa ya wizara ambayo imewafanya wengi wao kupanda ndege na kwenda nchi ambako hawakutegemea kufika?Je Meya atakuwa na ujasiri huo? baada ya kuwasiliti hata wenzao kwenye Full council? Kazi kwenu Wana Kigamboni'
 
Kwahiyo diwani kusafiri kwenda China kwa gharama za serikali ni kuwasaliti wananchi?!!!

Kweli Bavicha kiboko...
 
Kwahiyo diwani kusafiri kwenda China kwa gharama za serikali ni kuwasaliti wananchi?!!!

Kweli Bavicha kiboko...

Ni kawaida yenu CCM kuangalia maslahi ya Chama chenu na wala sio ya wananchi.......Umeambbiwa hayakuwa makubaliano katika Council........wamepewa Ofa kinyemela...what do u expect......?
 
We mtoa post acha kuwa ADUI WA MAENDELEO, kuna ubaya gani watu kujifunza jinsi miji inavyojengwa, au wewe unataka watu wajifunze miji inavyobomelewa! kwanini tusimsapoti mtu anapofanya jambo zuri?,.. yani watanzania tumefika point ya kupinga hata UJENZI wa miji!! kwali kazi ipo!
 
Kwahiyo diwani kusafiri kwenda China kwa gharama za serikali ni kuwasaliti wananchi?!!!

Kweli Bavicha kiboko...

Mh. Mkunga unafahamu kuna mgogoro mkubwa na wa muda mrefu baina ya wananchi wa Kigamboni na wizara ya ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi.
Kitendo cha madiwani wachache wa Kigamboni kukubali offer ya trip ya China kutoka kwa wizara tuhumiwa ni dhahiri kuwa wamekula rushwa ikizingatiwa kuwa hoja hiyo ilikataliwa katika kikao cha full council ya manispaa ya Temeke.

Hili halihitaji kuwa na degree kama ya JK kulifahamu bali ni suala la common sense tu mtu unatambua kuwa Prof. Tibaijuka ametoa rushwa kama alivyofanya juzi Muleba kwa kutembea na masufuria ya pilau kuvutia wananchi katika mikutano yake.
 
Diwani hawajawahi kupanda ndege hata siku moja sasa hapo unategemea nini? hizi ndiyo Rushwa zenyewe tunazozipigia kelele kila siku. Watu wa Kigamboni mtakuwa mmejimaliza wenyewe kama mtakubali kuiachia ardhi yenu ili waje wakae wazungu na mafisadi wenye mahela yao unless walipe hela inayoeleweka na muonyeshwe sehemu iliyopimwa yenye miundo mbinu iliyokamilika; msije mkawa Mabwepande nyingine!!!
 
We mtoa post acha kuwa ADUI WA MAENDELEO, kuna ubaya gani watu kujifunza jinsi miji inavyojengwa, au wewe unataka watu wajifunze miji inavyobomelewa! kwanini tusimsapoti mtu anapofanya jambo zuri?,.. yani watanzania tumefika point ya kupinga hata UJENZI wa miji!! kwali kazi ipo!

Wewe hata hujui kinachojadiliwa hapa.
Kwanza, hiyo rushwa ya safari ya China ilikataliwa katika kikao cha full council ya manispaa ya Temeke, lakini madiwani wachache kwa sababu ya ubinafsi na njaa zao wakaamua kuwa wasaliti wa wananchi na madiwani wenzao na kushobokea trip ya China.

Pili, waliotakiwa kweda China kujifunza juu ya ujenzi wa miji ya kisasa ni wataalanu wa mipango miji, wahandisi wa ujenzi, wakadiriaji majenzi na wakandarasi.

Wao madiwani wanatakiwa kusimamia haki za wananchi wao kulipwa fidia inayokidhi mahitaji ya sasa na kuzingatia uhalisia wa soko la ardhi.
 
Huo ni usaliti na hiyo safari wameipokea kama rushwa,kama si rushwa kwa nini waende kinyemela,
Wizara wameamua kutumia "Divide and rule" ili kufanikisha malengo yao Kigamboni'
 
Wewe hata hujui kinachojadiliwa hapa.
Kwanza, hiyo rushwa ya safari ya China ilikataliwa katika kikao cha full council ya manispaa ya Temeke, lakini madiwani wachache kwa sababu ya ubinafsi na njaa zao wakaamua kuwa wasaliti wa wananchi na madiwani wenzao na kushobokea trip ya China.

Pili, waliotakiwa kweda China kujifunza juu ya ujenzi wa miji ya kisasa ni wataalanu wa mipango miji, wahandisi wa ujenzi, wakadiriaji majenzi na wakandarasi.

Wao madiwani wanatakiwa kusimamia haki za wananchi wao kulipwa fidia inayokidhi mahitaji ya sasa na kuzingatia uhalisia wa soko la ardhi.

Jibu zuri sana'
 
Kwahiyo diwani kusafiri kwenda China kwa gharama za serikali ni kuwasaliti wananchi?!!!

Kweli Bavicha kiboko...

Kwa hiyo wewe Diwani kwenda kujifunza kujenga mji wao ni mainjinia wa mipango miji??
Jinsi mnavyopenda kutetea uovu kila mmoja unamuona ni BAVICHA kwa sababu wao ndio watetezi
wa wananchi siyo'
 
Kwahiyo diwani kusafiri kwenda China kwa gharama za serikali ni kuwasaliti wananchi?!!!

Kweli Bavicha kiboko...
Kwani hile ziara mafunzo kuhusu gesi waliyoifanya mawaziri wa CCM kutoka Mtwara imesaidiaje kutatua mgogoro na wananchi wa Mtwara?kinachotakiwa ni ushirikishwaji wa wananchi kujadiri miradi na si ujanjaujanja wa viongozi makanjanja wa CCM.Wanakwenda china kufanya nini wakati nyumbani kuna mgogoro unaofukuta?na wakishajifunza hiyo miji wanakwenda kujifunza watajenga wapi wakati wenye ardhi yao wanagoma kutoa kwa kutoshirikishwa?
 
We mtoa post acha kuwa ADUI WA MAENDELEO, kuna ubaya gani watu kujifunza jinsi miji inavyojengwa, au wewe unataka watu wajifunze miji inavyobomelewa! kwanini tusimsapoti mtu anapofanya jambo zuri?,.. yani watanzania tumefika point ya kupinga hata UJENZI wa miji!! kwali kazi ipo!
Kwani mji unajengwa na madiwani au wakandarasi?huo ni uwizi wa mchana kweupe,kwani hile ziara ya makada wa CCM kuhusu gesi ya mtwara imesaidia NINI?kama ni kujifunza waende wajumbe wa bodi ya wakandarasi (CRB),Chuo kikuu Ardhi na waziri wa nyumba na makazi ndiyo wataleta mabadiliko sio hao vilaza wa siasa za maji taka.
 
Kwani hile ziara mafunzo kuhusu gesi waliyoifanya mawaziri wa CCM kutoka Mtwara imesaidiaje kutatua mgogoro na wananchi wa Mtwara?kinachotakiwa ni ushirikishwaji wa wananchi kujadiri miradi na si ujanjaujanja wa viongozi makanjanja wa CCM.Wanakwenda china kufanya nini wakati nyumbani kuna mgogoro unaofukuta?na wakishajifunza hiyo miji wanakwenda kujifunza watajenga wapi wakati wenye ardhi yao wanagoma kutoa kwa kutoshirikishwa?


Pili, waliotakiwa kweda China kujifunza juu ya ujenzi wa miji ya kisasa ni wataalanu wa mipango miji, wahandisi wa ujenzi, wakadiriaji majenzi na wakandarasi.


Wao madiwani wanatakiwa kusimamia haki za wananchi wao kulipwa fidia inayokidhi mahitaji ya sasa na kuzingatia uhalisia wa soko la ardhi.

Hii ungesema wakati Slaa anatuma picha za ziara yake ya Marekani ungeeleweka.

Ziara ya Slaa umeisifia, ya madiwani unasema waende mafundi! Je, Slaa ni fundi wa solar energy?

View attachment 117813

Cc Ritz
 
Hao wana Kingamboni walipochagua MADIWANI wa CCM walitegemea nini? Tangu lini CCM hii mpya ikawa pamoja na wananchi.

Tena mimi nitafurahi kama wakirudi wasimame kidete hata fidia wasipate hao wana-Kigamboni labda ndiyo watatia akili kichwani 2015. Hongera madiwani wa CCM. Kelele za chura haziwazuii kunywa maji.
 
Madiwani wa Kata zilizo ktk mpango wa ujenzi wa mji mpya yaani KDA wamekubali kupofushwa macho na Wizara na waziri Mama Tibaijuka kwa kukubali kusafirishwa na Wizara eti kwa lengo la kwenda kujifunza juu miji mingine inavyojengwa.

Mwaliko huo pia ulikuwa ni pamoja na Mbunge wa Kigamboni Dr.Ndungulile,lakini hongera kwa Mbunge huyu alikataa ofa hiyo.

Kwa nini tunasema ni usaliti,kwenye kikao cho Full Council Temeke kikiongozwa na Meya ilionekana kuwa ofa hiyo si halali kwani Council haina taarifa ila alitafutwa kila diwani na kupewa ofa hiyo kama yeye.Na makubaliano yakawa ni kwamba wasiende mpaka wizara,ilete taarifa kwenye council na kueleza faida na hasara za safari hiyo,na lengo lake.

Lakini cha kushangaza madiwani hao wakakubaliana wao pembeni na kuamua kukubali ofa hiyo na kusafiri zao kwenda China na kwingineko eti kujifunza miji inavyojengwa.

La kujiuliza ni je kweli wakirudi watakuwa na ujasiri wa kusimama pamoja na wananchi na kukataa matakwa ya wizara ambayo imewafanya wengi wao kupanda ndege na kwenda nchi ambako hawakutegemea kufika?Je Meya atakuwa na ujasiri huo? baada ya kuwasiliti hata wenzao kwenye Full council? Kazi kwenu Wana Kigamboni'


njaa mkuu
 
Hii ungesema wakati Slaa anatuma picha za ziara yake ya Marekani ungeeleweka.

Ziara ya Slaa umeisifia, ya madiwani unasema waende mafundi! Je, Slaa ni fundi wa solar energy?

View attachment 117813

Cc Ritz

Dkt. Slaa kama raisi mtarajiwa alikwenda study tour ya vision Tanzania kwa lengo la kujifunza na kuchota uzoefu wa US katika sera, mipango na utekelezaji wake ili atakapokuwa raisi wako kuanzia 2015 aweze kusimamia kwa ukamilifu utekelezaji wa sera na mipango husika.
Mji wa Kigamboni uko kwenye hatua za mwisho za utekelezaji kwa maana ya ujenzi wake ambapo maafisa mipango miji na wahandisi ndio walitakiwa kwenda China kujifunza namna ya kutekeleza mradi wa ujenzi na sio kupeleka madiwani ili waje kuwaongopea wananchi ambao bado hawajafikiana muafaka na serikali hii ya kifisadi juu ya malipo yao,
 
We mtoa post acha kuwa ADUI WA MAENDELEO, kuna ubaya gani watu kujifunza jinsi miji inavyojengwa, au wewe unataka watu wajifunze miji inavyobomelewa! kwanini tusimsapoti mtu anapofanya jambo zuri?,.. yani watanzania tumefika point ya kupinga hata UJENZI wa miji!! kwali kazi ipo!

acha ukilaza wewe,habu nambie baada ya hao madiwani kuona miji inavyojengwa huko china,what do they add on the project?hebu sema faida hasa tunazozipata kama wakazi wa kigamboni,temeke,dar na taifa kwa ujumla kuhusu ziara ya madiwani hao?common sense a big problem eh?
 
Back
Top Bottom