dudus
JF-Expert Member
- Feb 28, 2011
- 22,124
- 49,384
Madiwani: Tunataka mikopo kama wabunge
Kikao hicho kiliongozwa na Katibu wa Madiwani Mkoa wa Dar es Salaam, Julian Bujugo, ambapo madiwani hao walitoa malalamiko yao, ikiwa ni pamoja na mishahara yao ambayo ni sh laki moja na ishirini kwa mwezi.
Chanzo kikuu kiliiambia Tanzania Daima kuwa wameshangazwa na hatua ya wao kudharaulika huku wakiwa ndio watendaji wakuu kwa wananchi katika kutekeleza shughuli mbalimbali za maendeleo.
Madiwani walimtaka Bujugo kuhakikisha anafuatilia suala la masilahi yao kwa kuhakikisha anakutana na viongozi wa serikali ili kupata muafaka juu ya malipo wanayopewa.
Walisema wanasikitika na jinsi hali ngumu inavyowakabili wananchi mbalimbali huku wabunge wakikopeshwa sh milioni 200 na benki moja (jina linahifadhiwa).
Ilielezwa kuwa fedha ya kulipia mikopo ya wabunge hao itatokana na kupangiana semina pamoja na safari za nje ya nchi, bila kutolewa fedha zozote kutoka katika mishahara yao.
"Huwezi kuamini, leo baadhi yetu tunalalamikia kupanda kwa sukari na gharama za maisha lakini ukweli ulio wazi wabunge wanaishi kama wafalme katika nchi hii...inabidi na sisi tusimame imara tuhakikishe tunaongezewa posho na kupewa mikopo," kilieleza chanzo hicho.
Kwa mujibu wa chanzo hicho, madiwani hao walihitaji kuona mabadiliko yanayokaribiana na wabunge, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha serikali inasimamia haki na kuwatafutia mikopo madiwani wote.
Kiliongeza kuwa katika miaka yao ya uongozi madiwani hawajawahi kukopeshwa mkopo hata wa sh milioni 20 wala milioni 10, wakati wabunge wamekabidhiwa hundi za magari za sh milioni 90 hivi karibuni.
"Hapana, ni kudanganyana, ni nani kati yetu anayesimamia masilahi ya wananchi kati yetu na wabunge ...tena hawa bila nguvu yetu hakuna rais wala mbunge anayeweza kupatikana," ilidaiwa.
Kikao kama hicho kinatarajiwa pia kufanyika katika wilaya za Temeke na Ilala na kukutanisha madiwani ili kujadili masuala mbalimbali, ikiwa ni pamoja na masilahi yao.
Hivi karibuni wabunge walipewa mkopo wa hundi za sh milioni 90 kwa ajili ya kununua magari pamoja na kukopeshwa sh milioni 200 kama mkopo wa kawaida.
SOURCE: Tanzania Daima, 18th March 2011 - Madiwani: Tunataka mikopo kama wabunge
- Wasema wao ndio walio karibu zaidi na wananchi
Kikao hicho kiliongozwa na Katibu wa Madiwani Mkoa wa Dar es Salaam, Julian Bujugo, ambapo madiwani hao walitoa malalamiko yao, ikiwa ni pamoja na mishahara yao ambayo ni sh laki moja na ishirini kwa mwezi.
Chanzo kikuu kiliiambia Tanzania Daima kuwa wameshangazwa na hatua ya wao kudharaulika huku wakiwa ndio watendaji wakuu kwa wananchi katika kutekeleza shughuli mbalimbali za maendeleo.
Madiwani walimtaka Bujugo kuhakikisha anafuatilia suala la masilahi yao kwa kuhakikisha anakutana na viongozi wa serikali ili kupata muafaka juu ya malipo wanayopewa.
Walisema wanasikitika na jinsi hali ngumu inavyowakabili wananchi mbalimbali huku wabunge wakikopeshwa sh milioni 200 na benki moja (jina linahifadhiwa).
Ilielezwa kuwa fedha ya kulipia mikopo ya wabunge hao itatokana na kupangiana semina pamoja na safari za nje ya nchi, bila kutolewa fedha zozote kutoka katika mishahara yao.
"Huwezi kuamini, leo baadhi yetu tunalalamikia kupanda kwa sukari na gharama za maisha lakini ukweli ulio wazi wabunge wanaishi kama wafalme katika nchi hii...inabidi na sisi tusimame imara tuhakikishe tunaongezewa posho na kupewa mikopo," kilieleza chanzo hicho.
Kwa mujibu wa chanzo hicho, madiwani hao walihitaji kuona mabadiliko yanayokaribiana na wabunge, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha serikali inasimamia haki na kuwatafutia mikopo madiwani wote.
Kiliongeza kuwa katika miaka yao ya uongozi madiwani hawajawahi kukopeshwa mkopo hata wa sh milioni 20 wala milioni 10, wakati wabunge wamekabidhiwa hundi za magari za sh milioni 90 hivi karibuni.
"Hapana, ni kudanganyana, ni nani kati yetu anayesimamia masilahi ya wananchi kati yetu na wabunge ...tena hawa bila nguvu yetu hakuna rais wala mbunge anayeweza kupatikana," ilidaiwa.
Kikao kama hicho kinatarajiwa pia kufanyika katika wilaya za Temeke na Ilala na kukutanisha madiwani ili kujadili masuala mbalimbali, ikiwa ni pamoja na masilahi yao.
Hivi karibuni wabunge walipewa mkopo wa hundi za sh milioni 90 kwa ajili ya kununua magari pamoja na kukopeshwa sh milioni 200 kama mkopo wa kawaida.
SOURCE: Tanzania Daima, 18th March 2011 - Madiwani: Tunataka mikopo kama wabunge