Madiwani CCM Wachapana Ngumi Kikaoni

Madiwani CCM Wachapana Ngumi Kikaoni

Hapo Mangula na Nape itawabidi wafungue KAMATI? Unajua tena PerDem's
 
Dah,wamechapana sababu ya mambo binafsi!!!!wataundiwa tume kuchunguza hizo tofauti zao binafsi.
 
Tushawazoea hao, ccm ni wagomvi kwa kuwa hawana tena sera wala muelekeo. Ukiwapa hoja wanajaa upepo na kurushia watu mawe na ngumi!
 
Mpwa wangu usilie sana kwani Machozi yetu yamefika mbali sana nayo yamelowanisha mioyo na kuburudisha nia zetu, nyayo za miguu yetu zimepoozwa na machozi ya mioyo yetu dhidi ya ufedhuli na ukatili huu, Kilio chetu kitageuka kuwa Furaha yetu.....maumivu yetu yatageuka kuwa kelele za shangwe kwetu, ndio ni kweli naiona kesho ileeee, ndio inakuja si kwa kusita sita bali inakuja kwa nguvu nayo imejaa furaha na ujasiri mkubwa, Naona vilio vya Vijana wale waliodhulumiwa haki yao ya kusoma, nao wanakuja tena kwa bidii wako pamoja na kesho yetu, ndio tutakua kitu kimoja kesho, si mmoja kwa umoja bali pamoja kwa umoja........Usilie tena, usilie kabisa MANI, zumbemku na saudari msilie saa bebeni shoka zenu twendeni
Mkuu lakini walishatuumiza!
 
Last edited by a moderator:
Wengine wanachukua chao mapema na mali za chama,wengine wanalambana bakora,wengine wako na CDM wanampinga meya wao n.k

Ukiona watoto wanataka kugawana mali ujue mzazi ziko zako duniani zimekwisha
 
Taarifa mbona haisemi sababu za wawili hao kurushiana makonde hadharani?

Halafu ati Gazeti la Mtanzania nalo litajivuna kuwa na Mhariri/Wahariri makini! shame!
 
CCM hapo ndipo ilipofika hakuna kubishana kwa hoja tena ni kutukanana na makonde basi,.. Nimeota ndoto nimeiona CCM ikiporomoka kwa kasi kama radi kuelekea shimoni hizo ndio dalili! chadema tujipange sawasawa 2014 serikali za mitaa na 2015 uchaguzi mkuu,.. tujipange maana baaada ya ushindi wa kimbunga 2015 tuna kazi kubwa sana ya kujenga nchi na wananchi wana matumaini makubwa mno!
 
na bado muda wana ccm watapigana sana kwa mtindo huu

Ni kawaida kwa sisiemu kuzichapa kavukavu, sio mara ya kwanza. In case mmesahau, nawakumbusha hizi:-
  • Shyrose Bhanji hivi majuzi alikwidana shati na kutaka kuzichapa na mashabiki wa Sofia Simba pale Shyrose alipokuwa anabishana nao kuhusu kukithiri kwa rushwa kwenye chaguzi zao UWT
  • Sophia Simba alizichapa kavukavu na Halima Mamuya pale walipokuw wameshindwa kuelewana kwenye mikutano yao ya ndani.n
  • Florence Kyendesya, mjumbe wa zamani wa UWT Mbeya alikwidana mashati na wenzake mkutanoni baada ya kushindwa kuelewana, mwishowe akavua nguo ya ndani na kumrushia mgomvi mwenzake, ili kumaliza hasira
  • Hizo picha hapo juu ni ushahidi tosha kwamba mambo si mambo huko ndani kwao!
 
Waacheni wafu wawazike wafu wenzao.
pia maandiko yanasema utawala unaojipinga kamwe hauwezi kusitirika(kudumu) utaanguka tu'.......sisi tupo waking'oana meno ......hatuna la kusema maana wajawazito wanaopoteza maisha kila siku kwa huduma duni wao hawaguswi....go on tungepata taarifa ya mazishi tungehudhuria mura!
 
Hivi madiwani hawana kinga Kama za wabunge wawapo bungeni? Kwa sababu hayo mambo yanapaswa kuishia humo humo - wachapane tu wakitoka nje wanakunywa chai pamoja. Ila wakizichapa nje ya ukumbi watakamatwa na sheria ichukue mkondo wake.
 
Kabla ya kikao walianzia hapa: New Mama Pungo.jpg
 
Back
Top Bottom