Madereva wanahitajika

Madereva wanahitajika

KAJAVI

Member
Joined
Jan 30, 2014
Posts
27
Reaction score
3
Kikundi cha WAADU kinahitaji madereva waaminifu , na wanaoweza kutunza pikipiki vizuri, kwa wiki kila mmoja atatakiwa kutoa elfu arobaini(40) na kila jumapili mkurugenzi atasimamia umwagaji wa oil.

Sifa za mwombaji
1, Awe ana leseni na cheti cha udereva kutoka chuo kinachotambulika na serikali.
2. Awe ameoa au kuolewa. Nia hapa ni kumpata kiurahisi na kuepuka kutumia chombo Massa 24 .
3. Awe hajawahi kufungwa au kutuhumiwa na makosa ya utapeli.
4. Awe Mtanzania mwenye umri usiopungua miaka 18 na usiyozidi miaka 50.
5. Awe na mvuto kwa Wateja.

Mwenye sifa atume maombi kwa Mwenyekiti wa kikundi cha WAADU SLP 369 Tabora.
Barua iambatanishwe na nakala za cheti cha VETA, LISENI, PASSPORT SIZE MBILI NA BARUA YA UTAMBULISHO KUTOKA KWA MWENYEKITI WA MTAA.
Mwisho wa kutuma maombi ni jumapili tarehe tisa mwezi wa tatu 2014.
 
oky umeskika vizuri japo sio liseni ni leseni au kiswahili ndio kimekuwa namna hii any way me napita tu nilijua udereva wa magari kumbe bodaboda ngoja wanakuja
 
Mwenye sifa atume maombi kwa Mwenyekiti wa kikundi cha WAADU SLP 369 Tabora.
Barua iambatanishwe na nakala za cheti cha VETA, LISENI, PASSPORT SIZE MBILI NA BARUA YA UTAMBULISHO KUTOKA KWA MWENYEKITI WA MTAA.
Mwisho wa kutuma maombi ni jumapili tarehe tisa mwezi wa tatu 2014.

Yaani mfumo wa Enzi za mwalim,barua hadi ifike si muda umeishakwisha?
Halafu Jamaa wakali kweli,yaani wana Mkurugenzi,duhhh
Cha kushangaza eti mkurugenzi ndio asimamia kazi ya kumwaga Oil(Minor Service),hii kali,Mnajua hadhi na nafasi ya mkurugeniz kwenye kikundi?au ndio vyeo tu,yaani kikundi hakina Katibu wakusimamia hayo?
Halafu kigezo cha kuoa ili dereva asifanye kazi masaa 24 hakina mantik,kwani nyie simnataka pesa?sasa mnafikiria pesa ataipata kwa urahisi.
Umri wa miaka 18 si mnataka kuajiri mwanafunzi huyo?na halafu awea ameoa kwa umri huo.Duhhh
Halafu awe na lugha nzuri kwa wateja,mtajujae?
 
Back
Top Bottom