Naomba tujadili kidogo pengine na kutoa ushauri kuhusiana na ukorofi wa madereva wa magari ya serikali barabarani. Utakuta dereva anakimbiza sana huku kawasha taa zote na hata wakati mwingine anatanua na kuvunja sheria za barabarani. Ukimnyima nafasi ya kupita anakutukana na kukutishia kuwa anaweza kukusababishia matatizo au kukufunga kwa kuwa eti anamuendesha mkubwa fulani. Je wao wanaruhusiwa kuvunja sheria?