Mungu saidia samatta afike mbali kama wakina messi na neymar.. Natamani siku moja ashinde mchezaji bora wa dunia kutokea Tanzania ..wanawake toeni mchango wenu inapotakiwa kutoa sapoti kama kupiga kura kwenye vipengele mbalimbali watakavyo shindanishwa ili Tanzania isiwe kichwa cha mwendawazimu tena.
Ila tujiulize kidogo, kwanini wachezaji wengi si hapa Afrika tu bali duniani wanapenda sana mahusiano na machangu? Samatta kabla hajapata hii tuzo machangu walimuona wa kawaida, baada ya kushinda rais wa machangu hapa Tanzania alijitahidi kumtafuta na kuongea naye karibia ya saa nzima mpaka jamaa akapigwa stop na wazazi wake kuwa aachane na huyo rais fake wa machangu kwani tabia zake zinaeleweka. Kuna changu mwingine mpya ambaye alishinda tuzo ya kimwana sijuwi wa nini, naye anatafuta namba ya jamaa atoke naye. Si Samatta tu bali wachezaji wengi hapa Bongo niwajuao mimi hutoka na machangu tu, je wanaogopa kudharauliwa na wanawake wanaojiheshimu au ni nini?