Inasikitisha sana kuona baadhi ya wakuu wa wilaya na mkoa wameamua kwa dhati kabisa kuingia mstari wa mbele kuwapigania wale wanaowataka.
Mkuu wa wilaya ya Kibaha Assumpter Mshana na Mkuu wa mkoa wa Simiyu Ndg Antony Mtaka wameamua kwa dhati kumsaidia Kheri Denis James Mgombea uenyekiti UVCCM Taifa.
Tafsiri yake mwenyekiti wa kukumbatiwa na vigogo hawezi kusimamia maslahi ya vijana badala yake watu watamuongoza....
Ningeshauri hawa watumishi wa umma na wateule wa Mhe Rais Dkt Magufuli wajiweke mbali na mchakato huu kwa kuwaunga mkono baadhi ya wagombea kwani yeyote atakayeshinda watafanya naye kazi.
Mkuu wa wilaya ya Kibaha Assumpter Mshana na Mkuu wa mkoa wa Simiyu Ndg Antony Mtaka wameamua kwa dhati kumsaidia Kheri Denis James Mgombea uenyekiti UVCCM Taifa.
Tafsiri yake mwenyekiti wa kukumbatiwa na vigogo hawezi kusimamia maslahi ya vijana badala yake watu watamuongoza....
Ningeshauri hawa watumishi wa umma na wateule wa Mhe Rais Dkt Magufuli wajiweke mbali na mchakato huu kwa kuwaunga mkono baadhi ya wagombea kwani yeyote atakayeshinda watafanya naye kazi.