Madawa ya Kulevya: Hii inatisha Tz

Madawa ya Kulevya: Hii inatisha Tz

SWEEPER

JF-Expert Member
Joined
Jul 16, 2012
Posts
269
Reaction score
87
Vijana 123 wa Kitanzania wanakabiliwa na kesi za kuingiza madawa ya kulevyawa Hong pekee. Vijana wa Kitanzania 43 nchini China (Macau). Walio China (macau) wakithibitika ni kunyongwa au kifungo cha maisha. Wale wa Hong Kong ni ahueni kidogo kisheria.

Source: Balozi wa Tanzania nchini China akiongea na VOA.
 
Kwahiyo tuna vijana 166 Macau na Hongkong pekee mwenye kesi za madawa..!bado Italy, Brazil, Pakistan, South, Thailand, Shanghai na Beijing China, Dubai, Japan ulaya nk nk nk....! So pity ni aibu kwa Taifa, ni aibu kwa watanzania
 
Kweli rais tunaye, hapo taarifa anayo, majina yote ya wauza unga wakubwa hapa bongo anayo ila yeye kimyaaa huku akitucheka tu. Juzi juzi tu hapa alimtibia Ray C na vijana walioathirika huko mitaani anawaona kwenye TV lakini wapi. Huyu rais huyu? Anamfunga Nguza na watoto wake kwa kutokuwa na makosa ila waharifu wa nchi anawaacha wanapeta kisa ni watu wake wa karibu wanaoshirikiana na Ridhiwani.
 
Marmo alishaondolewa, sasa hivi yuko mjeshi Shimbo
Jifunze kuelewa acha kukurupuka, unaambiwa ni Phirip Marmo ndio ameongea na DW. yeye ndio alikwenda kuwatembelea magerezani na siyo Shimbo.
 
Vijana 123 wa Kitanzania wanakabiliwa na kesi za kuingiza madawa ya kulevyawa Hong pekee. Vijana wa Kitanzania 43 nchini China (Macau). Walio China (macau) wakithibitika ni kunyongwa au kifungo cha maisha. Wale wa Hong Kong ni ahueni kidogo kisheria.

Source: Balozi wa Tanzania nchini China akiongea na VOA.

Jifunze kuelewa acha kukurupuka, unaambiwa ni Phirip Marmo ndio ameongea na DW. yeye ndio alikwenda kuwatembelea magerezani na siyo Shimbo.

Soma post iliyobeba mada ndiyo utajua nani anakurupuka.
 
Kwahiyo tuna vijana 166 Macau na Hongkong pekee mwenye kesi za madawa..!bado Italy, Brazil, Pakistan, South, Thailand, Shanghai na Beijing China, Dubai, Japan ulaya nk nk nk....! So pity ni aibu kwa Taifa, ni aibu kwa watanzania

Ni zaidi ya aibu mkuu. Haya ni matokeo ya kuporomoka kwa maadili, uroho wa mali, udhaifu wa dola, ufisadi na kutoweka kwa uzalendo. Hatuwezi kujivunia amani na utulivu na usalama wa nchi iwapo Tanzania ya leo ni uchochoro wa kupitishia madawa ya kulevya kwa kiasi kikubwa namna hii halafu tunadai tuna ulinzi wa kuaminika. Soon tutakuwa blacklisted.
 
Nimemsikia marmo kwa masikio yangu akihojiwa VOA, mleta mada amesahau kdg ukiacha HONG KONG NA MACAU, watz zaidi ya hamsini waliokatwa CHINA, wamehukumiwa kunyongwa akiwemo mama mmoja anaemiliki maduka mawili ya nguo kinondoni, marmo hakumtaja jina. swali kama jk anawajua hawa vigogo wanaotuma wenzetu wakanyongwe huko china, kwanini asiwachukulie hatua kunusuru roho za wenzetu zinazongoja vitanzi?
 
Nimemsikia marmo kwa masikio yangu akihojiwa VOA, mleta mada amesahau kdg ukiacha HONG KONG NA MACAU, watz zaidi ya hamsini waliokatwa CHINA, wamehukumiwa kunyongwa akiwemo mama mmoja anaemiliki maduka mawili ya nguo kinondoni, marmo hakumtaja jina. swali kama jk anawajua hawa vigogo wanaotuma wenzetu wakanyongwe huko china, kwanini asiwachukulie hatua kunusuru roho za wenzetu zinazongoja vitanzi?

mh tutapigwa x-ray kwenye ma airport hadi tukome ukionekana tu na passport ya tz
 
Rais mstaafu MWINYI alipigwa xray kiwanja cha ndege huko ughaibuni! ilimuuma akakemea sana dili hii ya vigogo wa cccm, wakamdharau matokeo ni hiyo idadi ya kutisha ya wabongo wanaosubiri kunyongwa kama sadam!
 
Kwahiyo tuna vijana 166 Macau na Hongkong pekee mwenye kesi za madawa..!bado Italy, Brazil, Pakistan, South, Thailand, Shanghai na Beijing China, Dubai, Japan ulaya nk nk nk....! So pity ni aibu kwa Taifa, ni aibu kwa watanzania
Mshana wewe
 
Nilikataaga hizi mambo za madawa namshukuru sana M/MUNGU. Nikimuona mtu ameathirika na madawa ya kulevya najisikiaga vibaya sana na sababu kuu ya kuachana na kujihusisha na hizi mambo.. sio nzuri kabsa kujihusisha nazo
 
Back
Top Bottom