Madai ya Lema kugoma kula hayana mashiko

Madai ya Lema kugoma kula hayana mashiko

Mimi sio CDM lkn huu upuuzi utolewe.Kagoma kula na mtu katoa sababu alafu mnaitaka ile sababu iongezwe nyanya chumvi na binzali ili aeleweke hamuoni huo ni ukandamizaji...
 
lema amewabadili sana wana arusha wamekuwa majasiri kwa hili analofanya anajenga kitu kwa wana Arusha
 
steve nyerere yuko wapi, kuna actor yuko mahabusu
 
hivi siku za weekend kunatolewa dhamana? maana watu kadhaa waliokamatwaga ijumaa naonaga dhamana ni jumatatu ila sijui kwa nini?
 
Amegoma kwa kunyimwa dhamana ambayo ni haki yake kimsingi
Mbona madai ya kitoto sana kamanda gani sasa huyo, navyojua mimi kamanda lazima uwe na roho ngumu hata ikibidi unakula hata panya au mijusi ili usife kwa njaa kwenye vita.
 
Huo ndio mwanzo tu bw gomba ameanza kazi na uthibitisho wa kuchaguliwa kwake unaonekana na hii ni kupasua ukuta tu bado kubomoa ukuta sept 1 wana arusha kaeni chonjo
 
Halafu tunaambiwa malengo ya UKUTA yametimia.

Yametimia vipi ilhali bado mnalalamika makamanda kunyimwa dhamana ilhali ni haki yao kikatiba?

Udikteta upi mlioutokomeza sasa?
 
hivi siku za weekend kunatolewa dhamana? maana watu kadhaa waliokamatwaga ijumaa naonaga dhamana ni jumatatu ila sijui kwa nini?
Madam mzima hujui kwanini jumamosi na jpili watu hawatolewi? Katika kalenda ya serikali ni siku gani wameweka ambazo siyo siku za kazi katika wiki?
 
nakumbuka kuna padre SA alijaribu kufunga siku 40 kama yesu lakini alipata umauti.ila ngoja tuone km huyu wa kwetu atafudhu teh teh teh.natania tu pole sn
 
Madam mzima hujui kwanini jumamosi na jpili watu hawatolewi? Katika kalenda ya serikali ni siku gani wameweka ambazo siyo siku za kazi katika wiki?

hiyo point ya weekend naijua ila kuna watu wanalalamikaga sana kuwa ndugu yake kafungiwa siku mbili bila dhamana! sasa sijui huwa wanamaanisha nini! it was literal question
 
Let me remind mtoa thread, kuna nchi inaitwa India walipata Uhuru baada ya jamaa mmoja kugoma kula alikuwa anaitwa Mahatma Gandhi! Soma history, that's all.
 
hiyo point ya weekend naijua ila kuna watu wanalalamikaga sana kuwa ndugu yake kafungiwa siku mbili bila dhamana! sasa sijui huwa wanamaanisha nini! it was literal question
Kama kawekwa ijumaa na wakashindwa mtoa ijumaa hiyohiyo hawana jinsi zaidi ya kusubiri hadi jtatu..ila kama wanalalamika kwa siku za kazi ni haki yao
 
Let me remind mtoa thread, kuna nchi inaitwa India walipata Uhuru baada ya jamaa mmoja kugoma kula alikuwa anaitwa Mahatma Gandhi! Soma history, that's all.
[emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] we mtie ujinga lema.

Anabeep kifo, kwanza naskia watamuongezea kosa lingine kujaribu kujiua.

Hayuko serious huyu.
 
Swala la kula au kutokula ni hiari ya mtu na ni uhuru wa kidemokrasia ndio maana hata Yesu alifunga siku 40 bila kula hakuulizwa na mtu kwa nini hali sembuse Lema ambaye hajala siku moja,sijui,mbili sijui ngapi hazifiki hata wikiKatiba inampa uhuru wa kuamini chochote kula au kutokula asibughudhiwe akitaka kula sawa asipotaka sawa.
 
Mh mbunge wa Arusha mjini amegoma kula tangu amewekaa maabus zinaendelea kusambaa kwa kasi,hiii ni baada ya maelezo yaliyotolewa na meya wa jiji la arusha bwana Calist Lazaro ambapo amesema Mh.Lema amelazimika kugoma kula baada yakutoridhika na ukamatwaji wake ambao ameutafsiri kama udhalilishwaji mbele ya familia yake.

Nalazimika kusema madai ya muheshimiwa mbunge Kugoma kula niyamsingi ila ameyafanya kwa kukurupuka,kiasi chakukosa mashiko,haswa kwa wanaomshikilia, mh lema Hajatuambia ni nini hasa anataka afanyiwe ili arejee kula kama kawaida,alipaswa kuliambia Jeshi la Polisi kama walimkamata kwakumdhalilisha mbele ya familia yake,basi polisi Wakaombe radhi kwa familia na watoto wake ndio arejeshe hali yake ya kula kama kawaida,

Niwazi watu wote wanaotumia njia hii kudai haki huweka masharti ambayo yakitekelezwa hurejea kula kama kawaida,mh Mbunge hoja yake ya msingi lakini ameishia kusema amegoma kula Kwa sababu amekamatwa kwakudhalilishwa mbele ya familia yake,ingependeza kama angeenda mbali zaidi kuliambia Jeshi la Polisi lifanye jambo gani ili arejee kula kama kawaida.

Baada ya kusema hayo naomba nimpe pole za dhati mh lema,sote tunafahamu maabusu sio pazuri Mh LISU alikaaa siku moja akatupa ushuhuda MAABUSU sio pazuri,LEMA umekaa siku Tatu tunakila sababu kukupa Pole.

Nawasilisha
Kati ya wabunge au wanachama wenye uchungu na chama chao pia wanapigania haki ni Godbless Lema NDIO MAANA WANA ARUSHA KAMWE hawatamani kumuacha,hongera Lema wengi tuko nyuma yako,Mola akusaidie,hakika ipo siku dunia itakufahamu
 
Mbona madai ya kitoto sana kamanda gani sasa huyo, navyojua mimi kamanda lazima uwe na roho ngumu hata ikibidi unakula hata panya au mijusi ili usife kwa njaa kwenye vita.
Hayo yote ni mepesi,hebu jaribu wewe kukaa siku tatu bila kula!Watoto laini hamuyawezi haya mambo
 
Back
Top Bottom