Ifike mahali twende mbele zaidi, badala ya kushangilia "ushindi" au kumshukuru mungu kwa kutenda "mema", tutumie akili zetu vyema. Baada ya Polisi kushindwa kesi hiyo ya uchochezi ndugu machemli afunge kesi mahakamani ya kudai findia kwa kubambikiwa shitaka lisilokuwepo.
Napendekeza fidia hiyo iwe kama anayodai Manji kwa Mengi. Hii itasaidia kuwadhibiti Polisi ambao hufanya kazi kama Roboti kwa kufahamu kwamba kesho wakifungua kesi za aina hiyo watafikishwa mahakamani kulipa fidia kutokana na madhila ambayo wamekuwa wakiyatekeleza kwa wananchi.
Nategemea Ndugu Machemli, ambaye ni kiongozi kuongoza njia kwa hjili kwa kufungua shauri la kutaka fidia n sio kushangilia "ushindi" kuwa amewabwaga polisi mahakamani, maana yake kesho watamtafuta kwa namna nyingine na kuendeleza mchezo wa paka na panya.