Machali azomewa kwa Kafulila

Machali azomewa kwa Kafulila

chuuma

JF-Expert Member
Joined
May 19, 2015
Posts
363
Reaction score
557
Mbunge wa jimbo la Kasulu mjini alohamia ACT kutoka NCCR-MAGEUZI amejikuta katika wakati mgumu baada ya kukabiliwa na zomeazomea na maswali kutoka kwa wananchi wa kijiji cha Sunuka jimbo la Kigoma Kusini kwa Kafulila.

Hayo yalitokea baada ya Machali kueleza kuwa amehama NCCR kwasababu ni chama cha hovyo na hata wabunge waliobaki ni mafala kwa watu wa Kaskazini.

Machali alisisitiza kuwa mbunge wenu Kafulila ni ---- wala hana ujanja wowote ndio mana amebaki na hoja ya ESCROW wakati jimbo limemshinda.

Akiulizwa maswali, wa kwanza alitaka kujua kwanini jimbo la ---- limepata lami wakati lake halina lami hata mita moja?

Swali la pili akaulizwa kumbe Kafulila ni ---- ndio mana alikutetea usipigwe mawe baada ya kumpiga baba yako makofi hadi kutapika kama ilivoripotiwa radio Kwizera?
 
dogo kabugi sana huyo! kafulila kamuambukiza kale kaugonjwa kake! yeye kafulila kapona!
 
Piga simu Watu wa kigoma watakwambia ili uamini ninachosema
 
Wewe jamaa ni wa kuhurumiwa nadiriki kusema umetumwa ,Watu wa kigoma hawana tabia hizo za kishoga za kuzomea Watu
 
unajua bhana , miaka ile nilikuwa siamini sana laana ya wazazi , lakini tangu huyu jamaa amtandike makofi babaake nimeanza kuamini .
 
Kumbe alimpiga babake???
Hiyo laana inaanza kumtafuna
 
Ningekuwepo eneo tukio tungekuwa tunaongelea habari nyingine kwa sasa kwani msaliti hafai kabisa Machali ameenda kujimaliza ACT
 
unajua bhana , miaka ile nilikuwa siamini sana laana ya wazazi , lakini tangu huyu jamaa amtandike makofi babaake nimeanza kuamini .
Maandiko matakatifu yanasema waheshimu baba na mama upate heri ya kuishi maisha marefu kama Mkosamali ana laana kumpiga baba yake basi itazdi kumtafuta sana ameenda kujimaliza kisiasa huko ACT
 
Maandiko matakatifu yanasema waheshimu baba na mama upate heri ya kuishi maisha marefu kama Mkosamali ana laana kumpiga baba yake basi itazdi kumtafuta sana ameenda kujimaliza kisiasa huko ACT


ni Machali
 
unajua bhana , miaka ile nilikuwa siamini sana laana ya wazazi , lakini tangu huyu jamaa amtandike makofi babaake nimeanza kuamini .

Mkuu amini kabisa Wazazi wana weza kukupa laana au Baraka,Ndiyo maana Mungu mwenyewe aliagiza kwenye Amri zake.
 
Asante kwa wananchi kutambua ACT ni tawi la CCM kudhoofisha upinzani. Ni ngumu kudanganya watu karne hii.
 
Kama machali amediriki kumpiga baba yake makofi ana laana. Tena kumpiga mpaka baba yake atapike hiyo ni laana iliyopitiliza. Watakao mchagua huku wakijua hilo, nao watashiriki laana
 
Kama machali amediriki kumpiga baba yake makofi ana laana. Tena kumpiga mpaka baba yake atapike hiyo ni laana iliyopitiliza. Watakao mchagua huku wakijua hilo, nao watashiriki laana
Izi siasa bhana...kwann hamkwenda kutoa taarifa police kua kuna mtu kamshambulia mwenzake.
 
Back
Top Bottom