Mabomu ya Gongo La Mboto: Lini Siku ya Maombolezo?

EMT

Platinum Member
Jan 13, 2010
14,483
15,308
Watu wamepoteza maisha yao kutokana na milipuko ya mabomu Gongo La Mboto. Rais amesema hili nin janga la kitaifa. Je, hakuna siku maalumu iliyotengwa kuwakumbuka ndugu zetu waliopoteza maisha kutokana na janga hilo?
 
kwanza rais wenu hata hakujiandaa kuongea chochote juu ya janga akaishia kututusi eti tusisikilize redio mbao, huku yeye na jeshi lake wakiwa hawana msaada kwa waathirika.

ameshindwa hata kusema anatoa msaada gani kwa waathirika, RED Cross ndo wamekuwa waokozi na clouds, nk but not the government! Aibu, kubwa. ajivunie uzembe wa watz, misri, na tunisia wangemtaka avunje baraza lake na aondoke ikulu mara moja!

hivi inakuja kweli, watu wameathirika na mabomu yapo majumbani kwa watu afu unadai acheni redio mbao, hakuna matatizo rudini nyumbani!

huyu ni mzalendo? au msanii asiyeweza kuchambua a na be?
 
kwanza rais wenu hata hakujiandaa kuongea chochote juu ya janga akaishia kututusi eti tusisikilize redio mbao, huku yeye na jeshi lake wakiwa hawana msaada kwa waathirika.

ameshindwa hata kusema anatoa msaada gani kwa waathirika, RED Cross ndo wamekuwa waokozi na clouds, nk but not the government! Aibu, kubwa. ajivunie uzembe wa watz, misri, na tunisia wangemtaka avunje baraza lake na aondoke ikulu mara moja!

hivi inakuja kweli, watu wameathirika na mabomu yapo majumbani kwa watu afu unadai acheni redio mbao, hakuna matatizo rudini nyumbani!

huyu ni mzalendo? au msanii asiyeweza kuchambua a na be?

kuna mabomu mengine yametua jikoni yapo na sufuria huko....rais ananiambia nirudi kwenye makazi yangu.....usiku uingie nilale kwa raha hakuna shida......hivi yupo siriaz kweli....au shauri halijampata yeye?
 
Kinachoniudhi ni vingozi wetu kuaddress the public huku wakichekacheka au kutabasamu. Hii inaonyesha as if you're are not serious. Watu wamepoteza maisha. Hawa watu ina wakumbukwe kwa kweli. It was not their fault. Kama ni janga la kitaifa then kuwe na siku maalumu ya kuomboleza wale waliofariki na kuwapa pole wahanga. Huwa tunasema Watanzania tuna ubinadamu, but I have not seen on this issue yet. Yaani ni business as usual.
 
kuna mabomu mengine yametua jikoni yapo na sufuria huko....rais ananiambia nirudi kwenye makazi yangu.....usiku uingie nilale kwa raha hakuna shida......hivi yupo siriaz kweli....au shauri halijampata yeye?

Preta sometimes nashindwa kuwaelewa viongozi wetu. Mtu anasema hivyo bila hata kufikiria kuwa kuna wengine makazi yao yamefagiliwa na hayo mabomu. Watarudi wakakae wapi? Ina maana alipotembelea huko hakuona hayo makazi yaliyoadhiriwa na hayo mabomu. Au ina maana aliishia tuu kutembelea ndani ya kambi ya jeshi?
 
Back
Top Bottom