Mabasi ya Dar - Mwanza ni hatari!

Mabasi ya Dar - Mwanza ni hatari!

Bad boy99

Member
Joined
Jun 1, 2014
Posts
9
Reaction score
0
Mimi ni mkazi wa mikoa ya kusini lakini ktk pita pita zangu nikapata safari ya kwenda Mwanza,nakumbuka tumetoka Ubungo dereva akiwa na mwendo wa kistaarabu sana.

Lakini tulipo anza kuicha Dar nikagundua kumbe jamaa alikuwa anahofia traffic tu mara akaanza kuweka gia za ajabu mwendo wa kasi usiopimika mpaka ikabidi nitafute mkanda upo wapi ndo nikagundua magari ya huko hayana utamaduni wa kuhimiza watu wavae mikanda,kwa kuhofia usalama wangu ikabidi nitafute kiti chenye mkanda lakini nikakuta abiria wenzangu wakanidharau sana kwa kitendo changu hicho.

Hata hivyo sikujali sana nikaamua kuvaa na nakutulia,sijakaa sawa tukawa tumefika Singida kutokana na dereva "kufukia matuta" mara kuna jamaa jirani yangu akalia kwa sauti kuu "mamaa" kumbe tayari kagonga kule juu sehemu ya kuwekea mizigo midogo midogo na kupasuka kichwa na damu nyingi zikamvuja sana!

Sikutaka kuongea kitu chochote ila kumsaidia jamaa apate nafuu,kuanzia hapo jamaa wakawa wapole baada ya abiria kuwapigia kelele nyingi!Naomba polisi watatue hali hii
 
basi gani hilo limalofukia matuta kiasi hicho? Bilashaka hao ni Super Najmnisa. Hawa jamaa Mi sipandi basi zao tena kama basi zimejaa bora niakhirishe safari vinginevyo kuwa nadharura kubwa.
 
kuna hawa wanaitwa zubery nilifika dar saa 2 waliofuata saa4 hadi saa 6
 
Mimi ni mkazi wa mikoa ya kusini lakini ktk pita pita zangu nikapata safari ya kwenda Mwanza,nakumbuka tumetoka Ubungo dereva akiwa na mwendo wa kistaarabu sana.Lakini tulipo anza kuicha Dar nikagundua kumbe jamaa alikuwa anahofia traffic tu mara akaanza kuweka gia za ajabu mwendo wa kasi usiopimika mpaka ikabidi nitafute mkanda upo wapi ndo nikagundua magari ya huko hayana utamaduni wa kuhimiza watu wavae mikanda,kwa kuhofia usalama wangu ikabidi nitafute kiti chenye mkanda lakini nikakuta abiria wenzangu wakanidharau sana kwa kitendo changu hicho.Hata hivyo sikujali sana nikaamua kuvaa na nakutulia,sijakaa sawa tukawa tumefika Singida kutokana na dereva "kufukia matuta" mara kuna jamaa jirani yangu akalia kwa sauti kuu "mamaa" kumbe tayari kagonga kule juu sehemu ya kuwekea mizigo midogo midogo na kupasuka kichwa na damu nyingi zikamvuja sana!Sikutaka kuongea kitu chochote ila kumsaidia jamaa apate nafuu,kuanzia hapo jamaa wakawa wapole baada ya abiria kuwapigia kelele nyingi!Naomba polisi watatue hali hii

Hiyo ya kujigonga kwenye keria ya mabegi ni tatizo la matuta yametengenezwa vibaya. Hata mimi nilishawahi kuona jamaa alijigonga akaumia kichwani damu zikawa zinatoka lakini mwendo wa basi sio kwamba ulikuwa mkubwa. Niliendelea kuyachunguza yale matuta nikaona yako sharp, hayafanani na yale ya brbr ya Dar-Moshi.
 
kuna basi inaitwa leina hiyo ni kiboko ya njia hiyo
 
Niliwahi kuongozana na gari moja ya Mwanza hapo Kimara suka kuja Ubungo, speed aliyotumia ni hatari sana, baada ya kufika ubungo kwenye foleni nilisikia watu kwenye Dala dala wakihamaki na kumjadili hata dereva wa hiyo dala dala ilibidi amwambie dereva wa basi hilo punguza speed ushafika Dar.
 
Mabasi kama hayo ndo nayapenda.Hakuna kupoteza tym!!
 
Kuna mdau mmoja ametaja gari la Leina, inaitwa LEINA TOURS, route ya DAR - KAHAMA, ni balaa tupu. Nshawahi kutoka Kahama sa 12 asbh, sa 1 jioni, tulikuwa foleni ya Ubungo, hilo basi linaovertake mpaka mashangingi.
 
Kuna mdau mmoja ametaja gari la Leina, inaitwa LEINA TOURS, route ya DAR - KAHAMA, ni balaa tupu. Nshawahi kutoka Kahama sa 12 asbh, sa 1 jioni, tulikuwa foleni ya Ubungo, hilo basi linaovertake mpaka mashangingi.

duh hiyo kali!!
 
Pandah Super Sam Xaah 2 upo nyegez
Co Mohamed Trans xafar ya dar - mwz km unatokah songeah bhanah Xaah 7 ndo nyegez

Bt huyu mjingah ALLYS ndo maanah xaxah hv ayupo hii road Mwxhoh wake Dodomah tyu coz anapaparah xn japo kuah xaah 2 ndo ulkuwah mdah wake kuingiah Nyegez Stand
Algongah HAICE mlmah wah Buhongwah{Nyashsh} aliuah abiriah wote wah HAICE 18
 
wajameni mashabiki wa treni....pinda anatutengenezea reli....
 
Back
Top Bottom