Mabadiliko ya mziki wetu wapi tunakwenda ?

Mabadiliko ya mziki wetu wapi tunakwenda ?

MO11

JF-Expert Member
Joined
Mar 23, 2014
Posts
19,560
Reaction score
41,523
Nilikua napitia mada hii
Tujikumbushe bendi zetu za zamani miaka ya 80 na 90 mitindo yao na wanamuziki wake


Kisha nikaja kusoma hii

beats kali toka kwa p funk

kichwa kikaniuma baada ya kusoma huu uzi

tujikumbushe nyimbo kali za bongofleva zilizotamba

unajua kwa nini kiliniuma wakati huu ndio muda niliokua napata akili kipindi hiki asilimia kubwa kila mahali utakuta watu wanaimba
Mziki ulikua mziki naweza nikakaa ndani najiuliza niimbe nini ambacho Prof J hajaimba au Mr 2 hajaimba au Afande sele hajagusa ??
Sitaki kuwaongelea akina Jay mo and co hakuna walichoacha hakuna wasichokigusa

Ila kwasasa mambo ni tofauti
nashindwa kujua nchi yetu wasanii wake wanaimba nini watu wote wanataka kuimba kama mafikizolo kama dj cleo
kuna nyimbo mpya ya madee imetengenezwa na uhuru kama sikosei hii ni ladha ya south afrika kabisa acha hii ya chegge na temba mpya wapi tunaenda wapi tumekosea ?

Je ni kweli wote tunapenda akina davido wanavyoimba jibu rahisi ni hapana ni baadhi tu.
je kwanini tunawaiga ?
1)utumwa wa fikra kwamba wanachofanya wao ni kizuri kuliko chetu kitu ambacho ni uongo

2)Media zetu kuwapa mashavu wasanii wa nje badala yake swali je ushawahi kuisikia nyimbo ya prof j ikichezwa channel O mimi sijawahi kama umewahi niambie

bahati mbaya pesa inaonekana wakati mziki hakuna

hivi Kweli wakati prof j anaimba starehe hivi nani angeimba nataka kulewa ?

wakati sugu anaimba nipo mikononi mwa polisi kweli wewe unayemtafuta aliyemwaga pombe ungepata airplay radio gani ?

Wakati umepita na mambo yake na mziki wake ila zimekuja hela zimebadili mziki wetu hatuma tone ya mziki wetu nikisikia kwaito nitajua hii kwa madiba nikisikia mdundo huu najua hawa wanaija wanafanya yao

Ila Tanzania sijui ndio maana hata nikisililiza wimbo wa taifa mpaka nisikie wakiimba ndip nijue ni wa nchi yangu

karibu tujadili
 
Mashabiki ndo tumesababisha haya yote

Pia media influence ime set agenda kuwa that kind of music ndo unalipa.
 
Bwana MO11 kwa sisi wapenzi wa music, kwa kweli muziki wa tanzania umeisha mwelekeo!! hauelewiki unaenda wapi? muziki inayoibwa sasa hivi ni kwa mtu yoyote mwenye sauti zuri na hela za kurekodia basi

hakuna ufundi wowote unaofaatwa katika upangiliaji wa matukio,vina pamoja na shairi lenyewe.
 
Last edited by a moderator:
Tufanyeje ili Tanzania nzima ipate ujumbe huu?.Tufanyeje ili wasanii wote wapate ujumbe huu?
 
Mashabiki ndo tumesababisha haya yote

Pia media influence ime set agenda kuwa that kind of music ndo unalipa.

mashabiki maana yake umenijumuisha na mimi na wale wote ambao hawapendi kuona mziki unakwenda ndipo sipo

kwa nini media wachague aina ya muziki ??
kwa nini hiyo kazi ya kuchagua wasiwaachie wasikilizaji ?
kwa nini unilazimishe niende twanga wakati nataka kwenda mashujaa au malaika ?
hapa ndipo udhaifi wao ulipo waache miziki yote tuchague sisi
 
Bwana MO11 kwa sisi wapenzi wa music, kwa kweli muziki wa tanzania umeisha mwelekeo!! hauelewiki unaenda wapi? muziki inayoibwa sasa hivi ni kwa mtu yoyote mwenye sauti zuri na hela za kurekodia basi

hakuna ufundi wowote unaofaatwa katika upangiliaji wa matukio,vina pamoja na shairi lenyewe.

bora ingekua mwenye sauti nzuri ila tatizo wenye hela kuhodhi muziki industry kwa kuweka watu wao hili ndio tatizo lingine wanataka walambwe miguu tena wana wasanii wao kuna wwngine ni watangazaji ila wanamiliki bendi zao mameneja wa wasanii wao wewe unategemea nini ??
 
Last edited by a moderator:
Wao wanasema muziki unakua,ati wanaenda intaneshino!
Kwa baadae Tz kutakuwa hakuna "radha" ya muziki wetu kama sisi
 
bora ingekua mwenye sauti nzuri ila tatizo wenye hela kuhodhi muziki industry kwa kuweka watu wao hili ndio tatizo lingine wanataka walambwe miguu tena wana wasanii wao kuna wwngine ni watangazaji ila wanamiliki bendi zao mameneja wa wasanii wao wewe unategemea nini ??

Mfano mzuri ni clouds fm kwenye kipindi cha xxl
 
Wao wanasema muziki unakua,ati wanaenda intaneshino!
Kwa baadae Tz kutakuwa hakuna "radha" ya muziki wetu kama sisi

HIZI ZINAITWA PROPAGANDA

haiwezekani ili mmoja awe mkubwa lazima aumie mwengine

kutwa kupiga nyimbo zao huku zetu kusema hazilipi kutwa kuwataja wasanii wao huku wetu hawatajwi kwao kujikomba komba tu kwa watu wasio na mpango na sisi
 
Muziki unaundwa na radha, ujumbe ufuata kutegemea mazingira na aina ya genre
hao hao akina prof jay walifanya kazi ya ziada kuwashawishi na kuvuta mashabiki ili wapende muziki wa rap haikutosha tu ujumbe bali ni pamoja radha na kipindi hicho hicho na producer huyo huyo aliweza kutengeneza nyimbo kama mikasi ya ngwea, hakuna kulala ya nature (style kwaito) na zote zikabamba.
Kama wanamuziki wetu watakopi style na kisha wakafanya vizuri zaidi hata kimataifa hakuna tatizo. Mfano muziki wa reggy chimbuko lake ni jamaica lakini haina maana wanaofanya mziki wa reggy nje ya jamaica hauna kiwango au hawakustahili kufanya. Kingine muziki kwa sasa ni biashara hatuwezi kung'ang'ania taarab ambao umeshindwa kuteka soko la kimataifa na wakati huo huo tukafanya muziki kwa style yao na bado tukafanya vizuri
 
Back
Top Bottom