Lord Denning
JF-Expert Member
- Jun 3, 2015
- 23,494
- 57,869
Amani iwe nanyi Wanabodi.
Leo napenda kuwaambia ukweli mchungu sana ambao inabidi tuupokee na kuufanyia kazi kweli.
Wanaotegemea Samia atabadilika na kuwa Kiongozi mwema atakayewapa Watanzania haki zao bila kuwepo kwa shinikizo (hofu) la kushtakiwa na kufungwa jela nawaonea huruma sana.
Wanaotegemea CCM hii ya leo itabadilika na kuacha kiburi, kulewa madaraka, ukatili na mauaji kisha kuwapa Watanzania Katiba bora inayosimika mifumo imara bila Viongozi wa CCM kuwa kwenye hofu ya kufungwa jela na kushtakiwa basi wanajidanganya sana.
Wanaotegemea Viongozi wa Serikali hii ya CCM watabadilika na kutenda haki huku wakiweka maslahi ya Wananchi mbele bila kuwa na hofu ya kushtakiwa na kufungwa jela basi nawaonea huruma maana wanajidanganya sana.
Wanaotegemea nchi hii itakuwa bora kama nchi yenye haki na maisha bora kwa kila Mwananchi bila Viongozi na Watendaji wa Serikalini kuwa na hofu ya kushtakiwa na kufungwa jela basi nawaonea huruma maana wanajidanganya sana.
CCM ilipofika wanajiona wao ndo wenye hatimiliki ya Tanzania. Wanajiona wao ndo wenye hatimiliki ya Watanzania. Chochote unachowaambia leo kamwe hawatakifanyia kazi endapo wataona kiko kinyume na maslahi yao haijalishi kinawanufaisha kwa kiasi gani Watanzania wa kawaida. Kwa msingi huu ndo mana nawaonea huruma sana wanaodhani nchi hii itapata Katiba bora chini ya CCM hii ambayo haijapata sababu ya kuogopa na kuhisi kuna umuhimu wa Katiba bora.
Kati ya jambo ambalo Watanzania tunapaswa kumshukuru Mungu ingawa limetuumiza hakika ni Mauaji yaliyofanywa na Samia na Serikali yake katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika mwaka jana.
Mauaji yale yameweka uwezekano kutokea jambo moja tu ambalo linaweza kuwapa CCM na Samia hofu ya kweli na hivyo kutusikiliza Wananchi na Matakwa yetu. Jambo hilo ni hofu ya kushtakiwa na kufungwa jela (Uwezekano wa kushtakiwa na kufungwa jela)
Pamoja na kiburi na ujanja wao wote, Samia na CCM yake hofu pekee inayoweza kuwatuliza na kuwafanya wawasikilize kweli Wananchi ni suala la kushtakiwa na kufungwa jela.
Kwa sababu hizo Watanzania hatuna budi kuyatumia mauaji yaliyofanya na Samia, Serikali yake na CCM yake kama suala kuu ambalo linaenda kubadili mustakabali wa Taifa letu. Kwa njia zozote zile tunapaswa kufanya kila liwezekanalo sio tu Samia na washirika wake wanatolewa hati za kukamatwa na Mahakama ya Makosa ya Jinai ya Kimataifa ICC bali pia Wanatolewa hati za Kukamatwa na Mahakama nyingine zilizopo maeneo mbalimbali Duniani ikiwemo Marekani na Mataifa ya Ulaya.
Samia, CCM na Viongozi wa vyombo vya ulinzi na usalama hawatatishwa na vikwazo vya kusafiri au kiuchumi au vya kununua silaha, hawatatishwa na wito mwingine wa maandamano au migomo au kelele tunazopiga humu, mitaani na kwenye social media's ( zaidi ya kutingishwa kidogo tu). Jambo pekee la kuwatisha na kuwafanya warudi nyuma na kutusikiliza Wananchi ni uwezekano wa kushtakiwa na kufungwa jela tu.
Wito wangu kwa Watanzania tuliopo ndani ya nchi na wengineo mliopo nje ya nchi, Vyovyote vile katika mwaka huu wa 2026 tuhakikishe Samia na Washirika wake wote wanatolewa hati za kukamatwa na Mahakama ya ICC, Mahakama yeyote ya Marekani au Mahakama yeyote katika Taifa lolote la Ulaya alafu tushughulikie kuzishurutisha nchi hizo wawakamate na kuwafikisha katika Mahakama hizo.
Kupitia haya ni lazima Wananchi tutasikilizwa kweli, kutendewa haki kweli na Taifa letu litapata Katiba Mpya iliyo bora kweli.
Leo napenda kuwaambia ukweli mchungu sana ambao inabidi tuupokee na kuufanyia kazi kweli.
Wanaotegemea Samia atabadilika na kuwa Kiongozi mwema atakayewapa Watanzania haki zao bila kuwepo kwa shinikizo (hofu) la kushtakiwa na kufungwa jela nawaonea huruma sana.
Wanaotegemea CCM hii ya leo itabadilika na kuacha kiburi, kulewa madaraka, ukatili na mauaji kisha kuwapa Watanzania Katiba bora inayosimika mifumo imara bila Viongozi wa CCM kuwa kwenye hofu ya kufungwa jela na kushtakiwa basi wanajidanganya sana.
Wanaotegemea Viongozi wa Serikali hii ya CCM watabadilika na kutenda haki huku wakiweka maslahi ya Wananchi mbele bila kuwa na hofu ya kushtakiwa na kufungwa jela basi nawaonea huruma maana wanajidanganya sana.
Wanaotegemea nchi hii itakuwa bora kama nchi yenye haki na maisha bora kwa kila Mwananchi bila Viongozi na Watendaji wa Serikalini kuwa na hofu ya kushtakiwa na kufungwa jela basi nawaonea huruma maana wanajidanganya sana.
CCM ilipofika wanajiona wao ndo wenye hatimiliki ya Tanzania. Wanajiona wao ndo wenye hatimiliki ya Watanzania. Chochote unachowaambia leo kamwe hawatakifanyia kazi endapo wataona kiko kinyume na maslahi yao haijalishi kinawanufaisha kwa kiasi gani Watanzania wa kawaida. Kwa msingi huu ndo mana nawaonea huruma sana wanaodhani nchi hii itapata Katiba bora chini ya CCM hii ambayo haijapata sababu ya kuogopa na kuhisi kuna umuhimu wa Katiba bora.
Kati ya jambo ambalo Watanzania tunapaswa kumshukuru Mungu ingawa limetuumiza hakika ni Mauaji yaliyofanywa na Samia na Serikali yake katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika mwaka jana.
Mauaji yale yameweka uwezekano kutokea jambo moja tu ambalo linaweza kuwapa CCM na Samia hofu ya kweli na hivyo kutusikiliza Wananchi na Matakwa yetu. Jambo hilo ni hofu ya kushtakiwa na kufungwa jela (Uwezekano wa kushtakiwa na kufungwa jela)
Pamoja na kiburi na ujanja wao wote, Samia na CCM yake hofu pekee inayoweza kuwatuliza na kuwafanya wawasikilize kweli Wananchi ni suala la kushtakiwa na kufungwa jela.
Kwa sababu hizo Watanzania hatuna budi kuyatumia mauaji yaliyofanya na Samia, Serikali yake na CCM yake kama suala kuu ambalo linaenda kubadili mustakabali wa Taifa letu. Kwa njia zozote zile tunapaswa kufanya kila liwezekanalo sio tu Samia na washirika wake wanatolewa hati za kukamatwa na Mahakama ya Makosa ya Jinai ya Kimataifa ICC bali pia Wanatolewa hati za Kukamatwa na Mahakama nyingine zilizopo maeneo mbalimbali Duniani ikiwemo Marekani na Mataifa ya Ulaya.
Samia, CCM na Viongozi wa vyombo vya ulinzi na usalama hawatatishwa na vikwazo vya kusafiri au kiuchumi au vya kununua silaha, hawatatishwa na wito mwingine wa maandamano au migomo au kelele tunazopiga humu, mitaani na kwenye social media's ( zaidi ya kutingishwa kidogo tu). Jambo pekee la kuwatisha na kuwafanya warudi nyuma na kutusikiliza Wananchi ni uwezekano wa kushtakiwa na kufungwa jela tu.
Wito wangu kwa Watanzania tuliopo ndani ya nchi na wengineo mliopo nje ya nchi, Vyovyote vile katika mwaka huu wa 2026 tuhakikishe Samia na Washirika wake wote wanatolewa hati za kukamatwa na Mahakama ya ICC, Mahakama yeyote ya Marekani au Mahakama yeyote katika Taifa lolote la Ulaya alafu tushughulikie kuzishurutisha nchi hizo wawakamate na kuwafikisha katika Mahakama hizo.
Kupitia haya ni lazima Wananchi tutasikilizwa kweli, kutendewa haki kweli na Taifa letu litapata Katiba Mpya iliyo bora kweli.