Mabadiliko ya kweli Tanzania ni lazima yaanze na kutengeneza mihimili 3 juu iliyo huru

ego

JF-Expert Member
Apr 10, 2013
1,620
1,407
Imekuwa ni kasumba ni kasumba kwa watanzania baada ya kuona watanzania hawaridhiki na mwenendo wa mambo kila mtu anakuja na kuwaahidi watanzania mabadiliko.

wanasiasa hawa wamekuwa kila mmoja anatafuta fikra zake au itikadi ya chama chake na kuamka kuyabeba kwa bendera ya kutaleta mabadailiko.

tumekwisha pitia hatua nyingi ni wakati sasa kutafakari na kusema hakuna mtu mmoja anaweza kuleta mabadiliko katika nchi hii bali watanzania wote kushirikiana ndio inaweza kuleta mabadiliko.

kwa mfumo wa utawala uliopo ni wazi kila kiongozi atakayekuja atalazimisha watanzania kutekeleza mitizamo yake, fikra zake hata kama watanzania hawa watakuwa wanaona vingine.

ili watanzania wote kushiriki katika mabadiliko ya nchi yao ni lazima kuwe na namna inayomwezesha mtanzania aliyepewa jitihada za kuongoza mabadiliko analeta mawazo ya ni kitu gani anataka kufanya na watanzania hawa wanakubaliana naye au wanamkosoa.

hili haliwezi kufanyika bila kuwa na mihimili mitatu iliyo huru na ikisimamiana.

kwa tanzania yetu bado mahakama na bunge ni kama taasisi ndani ya serikali, hakuna anayeweza kusimama kupinga au kukosoa jambo lolote linalofanywa na serikali kama halielekei uleta matokeo mazuri.

wabunge mmoja mmoja watakosoa sana lakini mahusiano yaliyopo baina ya bunge na serikali yanasababisha bunge kwa ujumla likae kimya.

mahakama kwa upande wake imo ndani ya serikali hivyo haionekani kama inaweza kupinga jambo zito lililoagizwa na serikali.

hoja kwa nchi yetu iwe ni kufanya mambo ambayo watanzania wanataka na sio kama viongozi wanavyodhani kuwa watanzania wanatakiwa kufanya wao wanavyotaka.

mfano mzuri tunaotaka katika nchi yetu ni kama kilichotokea marekani juzi, raisi akatoa amri na mahakama ikatengua. hayo ndiyo tunayoyataka kuwa kama baadhi ya mambo wanayotaka kufanya watawala watanzania kama hawariziki vipo vyombi vya kukosoa na hiyo ndiyo mantiki ya kutaka vyombo huru.

mfano : moja ya jambo ambalo linasemekana kukwamisha maendeleo ya nchi yetu ni hulka ya ufanyaji kazi.

watanzania wanatofautiana katika sababu zinazosababisha watanzania wasiwe wachapa kazi.

wapo wanaodhani watanzania watanzania ni wavivu, wapenda kukaa tu na kusubiri kupewa vitu vya bure, na hii ndiyo dhana iliyobebwa na utawala wa awamu ya tano kwa kuhamasisha na kulazimisha watu wafanye kazi.

wapo wanaopingana na dhana hii kuwa uvivu ni matokeo ya mambo mengi. wao wakiamini kuwa mfumo wa maisha wa sasa ulivyo kila mtu anasukumwa na mahitaji yake na familia yake kuhangaika kutafuta kipato. lakini mtu huyu anapokuwa haoni la kufanya atabaki kukaa tu hivyo kusema kukaa tu ni ukosefu wa ajira kwa namna moja na hili linaletwa na mambo mengi.

kwanza ni mifumo ya elimu.
hapa ina maana kuwa mifumo rasmi na isiyo rasmi ya elimu ni nguzo kubwa katika kujenga hulka na tabia za watu katika kazi. Wana jamii kama ukiwalea kwa elimu za kukaa tu kusubiri kupewa, wasipopata basi wajue eti hawakupangiwa na kama wamepangiwa watapata tu unategemea nini juu ya watu kuhangaika kutafuta maisha ukubwani? hivyo wapo wanaoamini mafundisho ya imani yanayoanza kwa watu wakiwa wadogo, wahubiri hawa wakiwaeleza wananchi hawa elimu zao hazina maana, mungu ndiye mtoaji wa kila kitu, hakuna anayeweza kupata chochote bila kuomba, watoto wanaambiwa mali hazigombaniwi bali mtu akae chini aombe.

matokeo yake ni masikini wanashinda kwenye nyumba za ibada wakiombewa eti ili waachane na umasikini na sio kushinda wakitafuta kazi, je tatizo liko wapi? utaondoaje umasikini kwa matajiri kuwa bize wakifany6a kazi na masikini wako bize wakiomba? utasikia huduma za maombi za kuleta utajiri zinaanzishwa na zinaendeshwa kisheria na wazi wazi. mtu akikwama katika shughuli zake haendi kukaa chini kutafakari kuna tatizo gani kupitia maarifa ya kiuzalishaji au kibiashara bali anakimbilia kwenye nyumba za maombi na waganga wa kienyeji akiamishwa kila kitu anachofanya kiko sahihi isipokuwa kuna mkono wa shetani.

unategemea nini kumuona yule tunayemkabidhi dhamana ya kubadili hulka za kufanya kazi kwa watanzania hawa au anayetaka kupewa fursa anaposhinda kwenye maombi au waganga eti kutafuta nafasi hiyo? unategemea nini unapomsikia huyu kila siku akiwaambia hawa wamuombee kuwa ndio njia ya kutimiza kile anachotakiwa kufanya?

lakini pia wapo anaoamini kabisa kuwa uvivu katika mfumo huu wa maisha yanayosukumwa na biasahara uvivu ni matokeo ya kukosa ajira. moja ya factor kubwa katika biashara ni mzunguko wa pesa. mzunguko wa pesa ukiwa mdogo ajira na ubora wa maisha ya watu unakuwa chini. hawa wanaenda mbali zaidi kwa kusema sio kwamba watu wa mijini wanafanya kazi sana kuliko watu wa mijini, yawezekana watu wa vijini wanafanya kazi zaidi lakini tofauti kubwa baina yao ni mzunguko wa pesa.

unategea nini unapoona yule anayejinasibu kutaka kubadilisha hulka ya watu ya kufanya kazi hatua anazozichukua zinaathiri mzunguko wa pesa unapungua kasi na atharizinaonekana wazi lakini yeye anasema wao ni kwa sababu ni wavivu. wahandisi katika taaluma zao huwa wanasema kama kuna kitu kinatoa huduma katika jamii lakini kikawa kibaya , unapotaka kukiondoa hiki kuweka kitu kizuri ni lazima kwanza utengeneze kitu cha mda cha watu kutumia wakati ukitengeneza kipya, kama ni jengo ni lazima ujue waliokuwa wakitumia jengo hilo watakwenda wapi kwa mda, kama ni barabara ni lazima ujue watumiaji watapita wapi kwa mda. taaluma zote zinatumia principle zilezile, sasa kama huko nyuma tulitengeneza njia haramu zilizotumika kuingiza fedha kwenye mizunguko ya kwenye jamii tulihitaji wataalamu hawa kutueleza kuwa tunapoziba fedha hizi biashara kwenye jamii hazitaathirika kwa maana tunawanyanganya fedha hizi haramu tunawapa fedha hizi halali hivyo mizunguko itakuwa salama. mfano kama watu walikuwa wanachukua posho zisizostahili wanatumia na kudunduliza kwa ajili ya kujenga nyumba basi tunafuta posho lakini tumeandaa mpango wa mikopo ya nyumba hivyo mtu atajenga na kulipa kidogokidogo kiasi kwa bajeti ya mtu aliyokuwa akitumia kwa mwezi katika matumizi ya kawaida haitaathirika, hivyo biashara mitaani hazitaathirika na hatua hizi.

lakini tunachokiona ni wanasiasa kuja anawaza jambo moja katika possibilities nyingi na kulazimisha watu kufuata analowaza yeye.

kwa mazingira yetu nani anaweza kukosoa uongozi, si kwa kuandika mitandaoni bali kwa kulazimisha utekelezaji wa mambo.

tunahitaji mihimili mitatu inayosimamiana na si kutumia mifumo ya mtu mmoja kulazimisha yeye analowaza tu.
 
Mawazo mazuri sana Mkuu. Lakini dunia hii imeshaendelea mbele sana. Nchi maskini kama zetu zingekuwa na kazi rahisi sana kama watawala wangekuwa wanafuata baadhi ya kanuni. Kwa mfano, huhitaji sana kujaribu jaribu principles za uchumi, kwa sababu zilishajaribiwa na zipo zilizofanikiwa na zipo zilizoshindwa. Je unafanyaje? unachukua zilizozindwa kisha unajaribisha kama zitafanya kazi kwako??, you must be nuts to do that.. Tatizo letu ni kwamba, huwa tunaacha kufanya mambo mazuri na ambayo yako proven kwamba ukiyafuata unaleta maendeleo haraka zaidi katika nchi. Badala yake, tunachukua mifumo mibaya na kuikumbatia. Macho tunayo na yanaona, lakini hupendelea zaidi kufunga vitambaa vyeusi machoni na kutembea kama vipofu....
 
Mawazo mazuri sana Mkuu. Lakini dunia hii imeshaendelea mbele sana. Nchi maskini kama zetu zingekuwa na kazi rahisi sana kama watawala wangekuwa wanafuata baadhi ya kanuni. Kwa mfano, huhitaji sana kujaribu jaribu principles za uchumi, kwa sababu zilishajaribiwa na zipo zilizofanikiwa na zipo zilizoshindwa. Je unafanyaje? unachukua zilizozindwa kisha unajaribisha kama zitafanya kazi kwako??, you must be nuts to do that.. Tatizo letu ni kwamba, huwa tunaacha kufanya mambo mazuri na ambayo yako proven kwamba ukiyafuata unaleta maendeleo haraka zaidi katika nchi. Badala yake, tunachukua mifumo mibaya na kuikumbatia. Macho tunayo na yanaona, lakini hupendelea zaidi kufunga vitambaa vyeusi machoni na kutembea kama vipofu....

Tatizo kubwa tulilonalo kwa afrika ni kushindwa kutmbua udhaifu wetu ni upi?

popote pale mchukue mtu amekulia mjini hajawahi kushika jembe hata siku moja unamkuta akitazama mashamba yamelimwa, akaona watu wameinama wanalima, akaona mvua zinanyesha na kumwagilia, akanona wanavuna nakupeleka sokoni basi yeye anajenga simple imaginations kichwani kuwa kilimo ni kitu chepesi na anawashangaa wakulima kutokwenda kulima na kupata.

hajui changamoto wanazokumbana nazo wakulima bali yeye anaamini wakulima watakuwa masikini kwa uvivu wao.

haya ndiyo mawazo ya viongozi wa kiafrika.

uzoefu wetu katika uongozi ni corruption kutumia ofisini za umma kwa manufaa binafsi kama kuomba rushwa, kuajiri ndugu zao kwenye nafasi za umma, kulewa madaraka,

kutumia fedha za wananchi bila tija yaani miradi inatumia gharama mara mbili au zaidi ya thamani yake na hakuna mwenye machungu watabaki kuhesabu mradi iliyofanyika na kujipongeza, kufanya miradi isiyokuwa na faida mfano kiongozi anachukua kodi anajenga rami kijijini kwao,

uzoefu wa uongozi afrika ni uongozi wa kitapelitapeli yaani mtu anajifanya anaumia kwa matatizo ya wananchi kumbe anatafuta nafasi ya kupiga dili.

principle za uchumi zipo lakini kuendesha taifa ni nery complex, si swala rahisi na ukijumuisha watu hawa wenye uzoefu katika kufanya maendeleo hasi ni complex zaidi.

nguzo kubwa ya kupambana na haya ni elimu au maarifa.

lakini cha kusikitisha ni kuwa ignorant people huwa wako very confident sana katika mambo ambayo yako very complex bila shaka ni kutokana na kutoona ugumu unaowakabili. Theoretical knowledge without experience ndio hao wanaosemwa ignorant wenye confidence.

akitizama mashamba anawashangaa wakulima kuwa masikini wakati hajui changamoto hata moja ya kulima. akienda kulima ndio anagundua ukipanda mazao ya miezi mitatu kama mvua haijanyesha katika kipindi hicho ujue huvuni na mazao hayasubiri mda ukipita yameharibika.

akienda kulima ndio anagundua kumbe kulima kwa mkono kwa siku unazalisha kama elfu tano tu kama ukizalisha sana na kuona huwezi kuwa tajiri kwa kulima kwa mkono.

akienda kulima ndio anagundua bei hupangi wewe mkulima kama wazalisha bidhaa viwandani bali wanunuzi wanapanga wenyewe na wakikosa kuna mazao hayatunziki yanaharika

changamoto kibao ambazo practically anagundua ni kazi ngumu kuendesha kilimo kwa wakulima wa kawaida bila kusapotiwa na serikali yao. umelima umevuna sasa unataka kuuza serikali inahisi kuna njaa inakuja katika taifa inapiga marufuku baadhi ya masoko mtunze vyakula vyenu na sio kwa kufidiwa, hivi huyu mkulima atatokaje?

kwa afrika hatuna watu wenye uzoefu katika kuongoza na kuleta positive change bali ama tuna wenye uzoefu wa kurudisha maendeleo nyuma au wale wenye kuangalia vitu na kuvirahisisha bila uzoefu.

wajanja huwa wanajifunza kwa wenzao wanapigaje hatua.

wanaunda vyombo ili vikosoane kuondoa makosa makubwa yanayofanywa katika kuongoza.

na ndio hapo hatua ya kwanza inatakiwa kuwa kutengeneza mihimili mitatu ya juu.

ikisha kaa sawa watasiamamia na kushauriana na hatua zozote taifa itapiga kutoa hapo zitakuwa zinapimwa na kurekebishwa kama kuna makosa. chombo chochote kitakachoundwa kutokea hapo kitakuwa kinatizamwa kutokea fikra tofauti na makosa yatapunguzwa.

lakini kuwa na muhimili mmoja wenye nadharia tatu ndani yake kama hii yetu probability ya kupoteza uelekeo ni kubwa sana na kuendelea kufuata njia hizi ni kugangania "ignorance" inayotutafuna
 
Ma
Maana yake Katiba mpya (ile rasimu ya Waryoba!!) ndicho cha kupiganiwa!

katiba mpya inaweza kuwa suluhisho lakini tutizame sana pengine kutoka nchi nyingine ni kwa jinsi gani chombo kiidogo kama takukuru kinaweza kumshitaki let say mkuu wa nchi,

tuliwahi kusikia waziri mkuu wa italia akishitakiwa wakati yuko bado madarakani,

tutizame ni kwa jinsi gani mahakama inaweza kusitisha agizo la serikali, tumesikia marekani raisi anatoa agizo na mahakama inatengua.

tuone ni kwa jinsi gani bunge linaweza kukataa mpango wa serikali, tunasikia wabunge wetu wakipiga kelele sana lakini hawana maamuzi.

tatizo letu kubwa tumekuwa tukijaribu kutatua changamoto hizi kubwa kwa njia nyepesi na kuzirudisha kwa njia nyepesi.

mfano mtu anajifanya anataka kuleta kifungu cha kuwezesha mkuu wa nchi kushitakiwa lakini anaenda kwenda kuunda chombo kinachoweza kumshitaki anampa raisi madaraka ya kuteua mtu huyo anayeweza kumshitaki amtakaye, anakwenda kwa anayetakiwa kufanya maamuzi anampa raisi madaraka ya kumteua.

hizi ni technical blanda ambazo zinadhihisha uwezo wetu afrika kuwa mdogo hata kama tunakuwa na initial kubwa za kielimu.

jambo lolote ni process hivyo kulitatua ni lazima kutizama katika process nzima hakuna kikwazo. kuweka kifungu cha kumshitaki mkubwa na ukampa mkubwa madaraka mkubwa huyo ya kuteua wa kumshitaki ni blanda inayoweza kufanywa na aliyekuwa "minor" katika taaaluma hiyo.
 
katiba mpya inaweza kuwa suluhisho lakini tutizame sana pengine kutoka nchi nyingine ni kwa jinsi gani chombo kiidogo kama takukuru kinaweza kumshitaki let say mkuu wa nchi,

tuliwahi kusikia waziri mkuu wa italia akishitakiwa wakati yuko bado madarakani,

tutizame ni kwa jinsi gani mahakama inaweza kusitisha agizo la serikali, tumesikia marekani raisi anatoa agizo na mahakama inatengua.

tuone ni kwa jinsi gani bunge linaweza kukataa mpango wa serikali, tunasikia wabunge wetu wakipiga kelele sana lakini hawana maamuzi.

tatizo letu kubwa tumekuwa tukijaribu kutatua changamoto hizi kubwa kwa njia nyepesi na kuzirudisha kwa njia nyepesi.

mfano mtu anajifanya anataka kuleta kifungu cha kuwezesha mkuu wa nchi kushitakiwa lakini anaenda kwenda kuunda chombo kinachoweza kumshitaki anampa raisi madaraka ya kuteua mtu huyo anayeweza kumshitaki amtakaye, anakwenda kwa anayetakiwa kufanya maamuzi anampa raisi madaraka ya kumteua.

hizi ni technical blanda ambazo zinadhihisha uwezo wetu afrika kuwa mdogo hata kama tunakuwa na initial kubwa za kielimu.

jambo lolote ni process hivyo kulitatua ni lazima kutizama katika process nzima hakuna kikwazo. kuweka kifungu cha kumshitaki mkubwa na ukampa mkubwa madaraka mkubwa huyo ya kuteua wa kumshitaki ni blanda inayoweza kufanywa na aliyekuwa "minor" katika taaaluma hiyo.
Yote hayo yanatokana na Katiba bora au bora katiba.
 
Back
Top Bottom