Mabadiliko Mawaziri tuliingizwa Kingi

Mabadiliko Mawaziri tuliingizwa Kingi

voicer

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2020
Posts
5,545
Reaction score
11,943
Mabadiliko yaliyofanywa na Rais Samia kwenye baraza la Mawaziri.Ni kiini macho.

Uhalisia ni kwamba Rais Samia alikusudia na anaendelea kujisimika na kujiimarisha kwa mbinu zozote zile ili kujiwekea mazingira ya ushindi wa urais 2025. Hili kumuweka mkwewe kwenye Tamisemi ni mpango rasmi kujipanga na uchaguzi mkuu. Sababu huyo ni mtiifu na mwanafamilia hivyo anaaminika na pia hata Msoga.Maana ni mswahili wa hapohapo pwani.

Rais amemuweka pale nwanafamilia ili kuhakikisha hamuangushi mama mkwe.Na soon kidogo tutaanza kuona mikeka mipya ya ma - RC's na ma- DC's kwa kutegemea nani yuko kundi lipi na mlengo upi ndani ya CCM.
Na Makamba jr,kapelekwa Mambo ya nje kwa mpango maalumu.Despite kwamba Kikwete na kundi lao wanataka kumuandaa na kuweka mtu wa kulinda na kuyaendeleza maslahi yao ifikapo 2030.

Endapo kama watakuwa wameponyoka na kupora tena 2025. Pili Makamba kawekwa pale Mambo ya nje na Uhusiano wa Afrika Mashariki.Sababu ndiyo wizara pekee ambayo waziri anasafiri mara nyingi kwenda nje kimajukumu tofauti na wizara zingine.

Pia ileweke kwamba Makamba kule Tanesco na kwingineko wizarani "Nishati" ameingiza serikali mikataba mingi mikubwa yenye utata, na tena yenye kugharimu maabilioni kama sio trilioni.Ambapo yeye na washirika wake ni wanufaika wakubwa. Hata kwenye Bwawa la Nyerere kuna harufu kubwa ya ufisadi kutokana na kucheleweshwa kwa ukamilishwaji wa Mradi. Ambapo kisheria ya mkataba.

Mhandisi wa mradi alipaswa na anapaswa kuilipa serikali riba ya ucheleweshaji.Lakini wizara imekuwa bubu hata pale ambapo wabunge wamejaribu kuhoji kupitia vikao vya bunge bila mafanikio. Sasa basi...Kwa kigezo hicho itakuwa rahisi Makamba kufanya monitoring muda wote endapo itahitajika kurekebisha hitilafu vaina ya kundi lao na wapewa tender zenye rushwa huko nje hususan India.

Ni rahisi kwake Makamba kukimbia nje huko na kuyatatua juu kwa juu na kisha kurudi kwa kigezo cha uwaziri mambo ya nje. Nashauri kama kweli bunge lina wazalendo ni wakati sasa Serikali kupitia Bunge iunde tume huru na ikachunguze madudu ya Tanesco chini ya uongozi wa makamba pamoja na Bodi yake aliyoiteua muda mfupi baada ya kuteuliwa kuiongoza wizara ya Nishati.

Na matokeo ya tume yatolewe hadharani Na kusomwa bungeni. Badala ya kumuuzia Biteko mbuzi wa Tanesco kwenye gunia! Serikali ingetimiza wajibu wake kwa maslahi mapana ya ustawi na Maendeleo ya nchi yetu.

Tunachezewa mno.....

Sakata la mafuta liwe kianzio

Nawakilisha!

Ni wakati sahihi kwa watanzania kuamka na kutetea haki zetu na maliasili zetu.
 
Magufuli kama angefufuka leo moja ya jambo angetubu mbele ya Watanzania na vile hana unafiki ni hili bunge! Ni kama ameishia kuwasaidia wapigaji.

Kweli sisi binadamu si kitu, hata uzungukwe na nani! Mungu pekee ndio anaijua kesho! Magufuli akifufuka sasa hivi ataisaliti CCM hadharani na kumuomba radhi Lissu.
 
Hivi kweli Samia ana mpango wa kugombea 2025?!

Kama ana mpango huo bora aache tu, yule akili yake inamtosha kuongoza mawe yasiyojua kuongea, hayo ndio akayazibie masikio, lakini sio wanadamu wenye maarifa ya kuuliza maswali yenye kuhitaji majibu sahihi.
 
Mabadiliko yaliyofanywa na Rais Samia kwenye baraza la Mawaziri.Ni kiini macho.
Uhalisia ni kwamba Rais Samia alikusudia kujisimika na kujiimarisha kwa mbinu zozote ili kumuweka mkwewe kwenye Tamisemi kwa mpango rasmi kujipanga na uchaguzi mkuu...
Ngoja nikupe mkakati ulivyokuwa.

1. Makamba aliwekwa nishati na madini atafute fedha za kuhonga siku zijazo atakapowania urais ambao anauota kila siku.

2. Fedha anazo tayari, tena nyingi kweli kweli, hivyo amepelekwa mambo ya nje ili kupata uzoefu na kufuata mkondo wa Mkapa na Kikwete.
 
Ngoja nikupe mkakati ulivyokuwa.
1. Makamba aliwekwa nishati na madini atafute fedha za kuhonga siku zijazo atakapowania urais ambao anauota kila siku.
2. Fedha anazo tayari, tena nyingi kweli kweli, hivyo amepelekwa mambo ya nje ili kupata uzoefu na kufuata mkondo wa Mkapa na Kikwete.
Uko sahihi mkuu.hilo liko wazi kabisaa!
Na ndio maana ninasema au kutoa Rai kwa bunge kuunda tume kuyachunguza madudu ya Tanesco chini ya Makamba kabla ya kumuuzia Biteko mbuzi kwenye Gunia.
 
Hivi kweli Samia ana mpango wa kugombea 2025?!

Kama ana mpango huo bora aache tu, yule akili yake inamtosha kuongoza mawe yasiyojua kuongea, hayo ndio akayazibie masikio, lakini sio wanadamu wenye maarifa ya kuuliza maswali yenye kuhitaji majibu sahihi.
Tuna Imani na Samia
 
Hivi kweli Samia ana mpango wa kugombea 2025?!

Kama ana mpango huo bora aache tu, yule akili yake inamtosha kuongoza mawe yasiyojua kuongea, hayo ndio akayazibie masikio, lakini sio wanadamu wenye maarifa ya kuuliza maswali yenye kuhitaji majibu sahihi.
U rais ni mtamu sana asikwambie mtu, kuna mikataba mingi sana ameshaisani hasa na waarabu hawezi kuwaacha hewani atagombea ili kumaliza mission, ili amsimike mtu wake wa kumlinda
 
Hivi kweli Samia ana mpango wa kugombea 2025?!

Kama ana mpango huo bora aache tu, yule akili yake inamtosha kuongoza mawe yasiyojua kuongea, hayo ndio akayazibie masikio, lakini sio wanadamu wenye maarifa ya kuuliza maswali yenye kuhitaji majibu sahihi.
Samia akigombea atapata kirahisi kabisa, lakini siyo kihalali. Atapata kwa kuiba na watu waliomzunguka wako desperate kweli kweli agombee tena kwani ''wanakula kilaini'' sana chini ya uongozi wake.

Na mbaya zaidi wako tayari kufanya chochote ili apite siyo kwa sababu wanampenda, la hasha. Ni kwa sababu wanapiga fedha ndefu bila kuulizwa.

Ikiwa ataamua kutogombea 2025 basi wameweka Makamba kama plan B. Alipewa nishati ili apige fedha ndefu ya kuusaka urais na baada ya kuzichuma amelekwa mambo ya nje ili kupata uzoefu. Pona yetu ni litokee la kutokea na Babu Jinga Mpango achukuwe kiti.
 
Kitu kingine, hivi kwanini mnamuona Makamba ana nafasi kubwa sana ya kuwa Rais wa Tanzania mbele ya safari?

Naona wengi wenu kigezo mnachotumia ni hicho cha "uwaziri wa mambo ya nje" mbona hata Membe nae alipita huko lakini mwisho wa siku akaangukia pua?

Hata kama mwenyekiti wa CCM anakuwa na nguvu kubwa kwenye maamuzi ya mwisho, hasa kuteua mgombea, lakini binafsi naona kuna mambo mengine makubwa zaidi lazima yazingatiwe ambayo Makamba hana..

- His past and present record; huyu anaonekana wazi ni fisadi, na sio fisadi akiwa serikalini pekee, ameshakuwa fisadi tangu shuleni aliposoma, hafai.

- Utendaji mbovu; wizara karibia zote alizowahi kupelekwa hajawahi ku deliver chochote cha maana, ni mtu wa showoff zaidi anayesubiri kubebwa na jina la baba yake, na marafiki wa familia yao.

- Kukubalika; hapa ndio hamna kitu kabisa, Makamba hata kama wakilazimisha kumpitisha watakuwa na kazi ya kumuibia kura kwa nguvu sana, hii ni tofauti na wakati wa Kikwete kwa mfano, ambaye tayari alikuwa akikubalika kwa asilimia kubwa ya watanganyika.

- Egoism; kujitutumua kutaka aonekane anajua wakati kiuhalisia hajui chochote, hili nalo linachangia sana kumshusha miongoni wa watanganyika.
 
Samia akigombea atapata kirahisi kabisa, lakini siyo kihalali. Atapata kwa kuiba na watu waliomzunguka wako desperate kweli kweli agombee tena kwani ''wanakula kilaini'' sana chini ya uongozi wake. Na mbaya zaidi wako tayari kufanya chochote ili apite siyo kwa sababu wanampenda, la hasha. Ni kwa sababu wanapiga fedha ndefu bila kuulizwa. Ikiwa ataamua kutogombea 2025 basi wameweka Makamba kama plan B. Alipewa nishati ili apige fedha ndefu ya kuusaka urais na baada ya kuzichuma amelekwa mambo ya nje ili kupata uzoefu. Pona yetu ni litokee la kutokea na Babu Jinga Mpango achukuwe kiti.
Hii sababu uliyoitoa nakubaliana nawe, kuna wajanja wengi serikalini kwa sasa wanafaidi matunda ya ujinga wa Samia, hao lazima wapige kelele za mama mitano tena.
 
Back
Top Bottom