Maaskofu mnaoleta siasa madhabahuni kumbukeni busara za mzee Makamba

Kuna watu mnamuandalia mazingira magumu sana Rais wa nchi hii na kibaya zaid na yeye ameshindwa kutegua huu mtego.
Naamini kwa kiasi kikubwa wote mnaomtetea na kutopenda aguswe wala kukosolewa mnafanya hivyo kwa ajili ya matumbo yenu tu na sio kitu kingine, nyinyi ni masalia ya Waafrika wasaliti. Ukitaka kujua nyinyi ni wanafiki kwa Rais basi rejeeni ya rafiki zenu wa Zimbabwe, hawa ndugu zenu walikuwa tayari kutoa roho ya mtu yoyote aliyethubutu kusema Mugabe ni mzee, wapo watu walifungwa huko kwa vitendo vyao vya kumuomba Mzee Mugabe aondoke au asiingoze nchi kifamilia na walipingwa na wakaitisha press kama zenu kumtetea Mugabe na hata kumuita baba wa demokrasia na mtetezi wa wanyonge kama mnavyomuita Rais Magufuli, lakini jambo la kustaajabisha siku jeshi lilipojaribu tu kumtisha Mugabe basi huwezi amini nchi nzima iliingia mitaani kumkataa Mugabe utafikri sio wale siku tatu zilizopita waliomshangilia Mugabe.
Nyinyi wote mnaokataa Rais asikosolewe kwa visingizio kuwa huyu ana mamlaka kutoka kwa Mungu hamumtakii mema na ni wasaliti wakubwa sana.
 
MAASKOFU MNAOLETA SIASA MADHABAHUNI KUMBUKENI BUSARA ZA MZEE MAKAMBA.

Najiuliza sana hawa Maaskofu wanaotokwa mapovu kumshambulia Rais Magufuli madhabuhini dhamira yao nini?

Au nao wanataka kupata ubatizo wa moto kama anavyosema Mzee Yusuf Makamba?

Wamegeuza madhabahu kuwa uwanja wa siasa za upinzani kumshambulia Rais. Bahati nzuri wote tunawafahamu kwa historia zao, maana historia ni Mwalimu mzuri.

Juzi kati nimemsikia Askofu wa KKKT Dayosisi ya Karagwe Askofu Benson Bagonza baadaye akafuata Askofu Zakaria Kakobe. Huko nyuma alikuwa Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Rulenge Ngara Askofu Severin Niwemugizi na alitanguliwa na Askofu wa KKKT Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Askofu Steven Munga.

Hawa wote tangu Rais Magufuli aingie madarakani sijawasikia wakitambua juhudi za kupambana na Rushwa na Ufisadi, Sijawasikia wakisema kuhusu kufutwa ada ya wanafunzi shuleni, sijawasikia wakitambua kuongezwa kwa bajeti ya dawa hospitali, sijawasiki wakitambua kununuliwa ndege za serikali kwa ajili ya usafiri wa anga na utalii, sijawasikia kwa chochote juu ya juhudi za kuondoa ubabaishaji katika ofisi za serikali, sijawahi kuwasikia wakisema chochote juu ya kuanza kwa ujenzi wa reli ya kati, sijawasikia wakisema kitu kuhusu uboreshaji wa miundombinu ya barabara, madaraja, vivuko.

Wala sijawahi kuwasikia wakizungumzia ongezeko la makusanyo ya kodi, wala sijawasikia wakieleza namna bandari zinavyoboreshwa, sijawasikia wakitambua namna matumizi ya anasa yalivyopigwa pini, sijawahi kuwasikia wakieleza jinsi Rais anavyosisitiza kufanya kazi.

Hata linalowahusu la Rais kumtaja Mwenyezi Mungu, kumtambua na kuhudhuria Ibada makanisani. Hawajawahi kuunga mkono.

Badala yake nawasikia mapovu yanawatoka wakidai Kupewa haki ya kumkosoa na kumdhalilisha Rais, kumsema na kuwachochea wananchi wamchukie Rais na Serikali. Zaidi nawasikia wakitamba madhabahuni kuwa wao wana pesa na hawababaishwi, wakati tunatambua wanaishi kwa sadaka zinazotolewa na walala hoi kabisa ambao wanakwenda kwenye nyumba zao za ibada ili wasali.

Juzi Askofu Bagonza anamshambulia Rais kwa kumtetea Askofu Kakobe. Eti anadai ni haki kwao kufanya siasa madhabahuni. Ebooo!!! Askofu tunapokuja kanisani tunakuja kusali, hatuji kwenye mkutano wa siasa. Na tunaokuja kanisani tunatoka vyama tofauti, baadhi ni wanachama wa CHADEMA unayoishabikia na wengine ni wanachama wa CCM ambao Mwenyekiti wao ni Rais unayemponda. Askofu unatuvuruga.

Kama unataka kuzungumza mambo ya siasa, madhabahuni sio mahali pake. Na hoja yako kuwa mkifanya masuala ya maji, umeme na hospitali hamsemwi lakini mkimsema Rais mnasemwa sio hoja yenye mashiko. Tofautisha masuala ya maendeleo na masuala ya siasa unazozifanya wewe na huyo Askofu Kakobe. Ni lini Rais ama kiongozi wa siasa umemsikia akiwashambulia viongozi wa dini kwa kazi zenu?

Watanzania tunafahamu kuwa wewe Askofu Bagonza na Askofu Kakobe ni miongoni mwa Majeruhi wa safari ya matumaini. Mlijiingiza kwenye siasa, mkapanda basi la safari ya matumaini na dereva wenu Edward Lowassa akashindwa akaukosa Urais, sasa mmegeuza kuwa hasira ya kumshambulia Rais Magufuli.

Wewe Askofu Bagonza ndiye uliyempa madhabahu Mtuhumiwa wa Ufisadi Edward Lowassa afanye kampeni zenye ubaguzi wa kidini, tukawasikia mkisema sasa zamu yetu Walutheri. Bisha sio wewe?

Wewe Askofu Bagonza ndiye umetoa kauli ya kuwaunga mkono wanasiasa wa upinzani juu ya agizo la Rais Magufuli kutaka Watoto wanaopata mimba wasirudishwe darasani kuchanganywa na watoto ambao sio wazazi. Bisha???

Wewe Askofu Bagonza ndiye uliyeungana na upinzani kupinga kauli ya Rais aliyeweka wazi kuwa Katiba Mpya sio kipaumbele chake, anataka maendeleo aliyowaahidi watanzania kwanza. Tena ukaungana na mwenzako Askofu Munga. Bisha???

Kibaya zaidi tunakufahamu Askofu Bagonza unaunga mkono ndoa za mashoga. Na huu mradi baada ya kugonga mwamba kupitia Serikalini sasa unapenyezwa kupitia viongozi wa upinzani na kupitia kwa viongozi wa dini na wewe Askofu Bagonza tunakujua unatuletea mashoga kila siku kwa kivuli cha kuwa viongozi wa dini ama marafiki wa kanisa lako.

Leo unamuunga mkono Askofu Kakobe ambaye anamshambulia Rais tena bila hata kujali makandokando ya Kanisa lake ambalo lipo kwenye hifadhi ya barabara.

Maana nimeshangaa sana Askofu Kakobe huyu ambaye anajiita mtabiri na hasemi kama ni Mtabiri anayeshindwa kila jambo anamshambulia Rais Magufuli na anataka tumuamini kuwa ni kiongozi wa dini wakati ni mwasiasa kabisa huyu.

2015 Askofu Kakobe alitabiri kuwa mtuhumiwa wa Ufisadi Edward Lowassa atakuwa Rais, akaongea kwa hamasa madhabahuni. Akapigiwa makofi na waumini wake. Hakuishia hapo akaenda kwenye mikutano ya Chadema ya M4C na picha zipo akaendelea kuunga mkono siasa za upinzani na akaendelea kusema Lowassa atakuwa Rais, leo anataka tumuamini kuwa ni kiongozi wa dini tu wakati ni mwanasiasa kabisa huyu.

Huyu Askofu Kakobe tunamjua na sielewi kwa nini mpaka sasa hajakamatwa kwa sababu nina hakika anatuhuma za uhujumu uchumi na utakatishaji wa fedha. Na vyombo vilianza kumchunguza akakimbilia nje ya nchi. Wazee wa kanisa lake walikuwa na mgogoro nae juu ya matumizi mabaya ya fedha za kanisa, wakaburutana hadi kwenye vyombo vya sheria.

Leo anatamba madhabahuni kuwa ana fedha kuliko Serikali? Anaidhalilisha Serikali mchana kweupe eti ana fedha za kuwagawia mawaziri. Mwizi kabisa huyu nae anataka kuiyumbisha nchi kwa fedha za sadaka anazowatapeli wananchi mchana kweupe kwa miujiza yake ya uongo?

Halafu anajifanya mtu wa Mungu na anataka tumuamini.

Nashangaa sana sana. Na navishangaa vyombo vya dola vimekaa kimya dhidi ya mtu huyu maana mimi nilijua tangu amekimbilia nje ya nchi hajarudi. Kumbe karudi na wanaendelea kumuangalia?

Na kwa kweli vyombo vya ukaguzi vizuri viyaangalie haya makanisa. Ikiwezekana kama ambavyo Mkurugenzi wa Habari Maelezo Dk. Hassan Abbas alivyoandikisha upya magazeti na majarida, umefika wakati hata haya makanisa yasajiriwe upya na kuwekwe vigezo vya kanisa kuitwa kanisa. Maana vinginevyo baadhi ya makanisa yatakuwa yanatumiwa kuivuruga nchi na sisi tunayaangalia. Au kama vipi nakuomba Mhe. Rais kama ulivyopiga marufuku mikutano ya hadhara piga marufuku pia mahubiri ya kisiasa kama ya akina Askofu Kakobe, Bagonza, Gwajima na Niwemugizi.

Angalieni pia na taasisi zinazoongozwa na haya makanisa. Maana mimi najua mfano Askofu Munga, Chuo Kikuu cha Sebastian Kolola kipo chini ya KKKT Dayosisi ya Kaskazini Mashariki. Alichokifanya yeye ni Mkuu wa Chuo, Makamu Mkuu wa Chuo ni Mke wake, Mhasibu ni Mtoto wake na Mkwewe nae ana cheo hapo. Ukifuatilia kwa undani utaona wakati anaomba ufadhili wa kujenga chuo hiki na kukiendesha aliomba kwa jina la wananchi, lakini hapa kakifanya mali ya familia.

Yapo mengi ya kuwahoji hawa Maaskofu na uswahiba wao wa siasa. Wasitudanganye na wasituyumbishe.

Hivi kweli hiyo hoja feki ya demokrasia waliyoibeba kutoka upinzani, najiuliza tu hivi kuna watu wabinyaji demokrasia wanaowashinda viongozi wa dini? Maana kwenye dini humu anachosema Askofu hakina mjadala. Ni wapi waumini huwa wanahusishwa kwenye kupanga matumizi ya mapato ya Kanisa?

Ndio maana viongozi hawa wanatamba kuwa wanapesa kuliko Serikali, wengine wanatamba wananunua ndege na treni, wanatembelea magari ya kufahari. Ni fedha za walala hoi wanaotoa sadaka ama unyonge wao unatumika kuomba misaada huko nje. Tusidanganyane.

Sisi watanzania tutaendelea kumuunga mkono Mhe. Rais Magufuli kwa sababu tunatambua anafanya alichoahidi wakati anatuomba kura, ananyoosha nchi iliyokuwa imeoza kwa ufujaji wa fedha za umma na mali za umma, iliyokuwa imetapakaa wizi, ilikuwa haina Mswalia Mtume kwa wanyonge.

Tunakuomba Mhe. Rais wewe chapa kazi, hawa wanaopiga kelele washughulikie bila haya. Kwani ukimkamata Askofu Kakobe kwa madudu yake hata leo nani atahoji? Kwa sababu tunamjua na madudu yake. Funga kanisa lake analotumia kufanya uchochezi, mbona yeye mwenyewe aliwahi kulifunga kwa muda mrefu wakati ana mgogoro wa ndani ya kanisa? Na wengine hivyo hivyo. Tena wengine hata sio raia wa nchi hii. Shughulika nao, ndio kazi tuliyokupa. Ukiwaacha hawa watatuvuruga, maana wengine sasa hatupendi hata kwenda kanisani siasa tu kila mahali.

Halafu Mhe. Rais hivi Lowassa mpaka leo vyombo havimkamati kwa nini? Maana huyu ndio mfadhili wa fujo zote hizi. Na kisa ni kimoja tu, ulivyomchapa kwenye uchaguzi wa Chama mwaka 2015 na baadaye akakimbilia CHADEMA nako ukamchapa. Sasa kaamua kutumia fedha alizoiba serikalini kukuvuruga usifanye kazi kwa amani. Unamuachaje huyu. Mbona akina Rugemalila na yule Singasinga Seth wapo ndani? Kamata huyu, kaiba sana. Ukimweka ndani utaona watu watakavyokuletea ushahidi wa madudu yake akiwa huku nje ni ngumu sana. Anahonga sana huyu Mzee, ana hela nyingi mno. Ndio maana akina Freeman Mbowe hawamuachi wanajia ile ni ATM muda wote inatema hela.

Hata hii Kamati ya kuhakiki mali za CCM katika changamoto itakayokumbana nayo ni nguvu ya Lowassa, maana huko kwenye CCM ndio kaiba mpaka basi. Hata watoto wanajua kuwa ni mwizi licha ya juhudi za CHADEMA kumsafisha.

Haya naishia hapa
Viva Tanzania

*Jackson Masendoke*
*Mkazi wa Ilala, Dsm*
*28 Desemba, 2017*
Si kwa povu hili...Lumumba mbona hamtulii... Na bado sindano zitawaingia tu
 
Umeandika mengi sana kudhihirisha ujinga kama siyo upumbavu wako.

1. Taasisi za dini ni mkono wa imani wa serikali kwa maana ya kuwajengea imani wananchi juu ya serikali yao. Na serikali zote msingi wake ni utaratibu unaoelekezwa na dini zote. Ndiyo maana kuna dini rasmi za serikal na watawala kuapishwa kwa imani za dini zao. Baadhi tumejiridhisha kuwa hapa kwetu dini rasmi ya serikali ya ccm ipo.

2. Kwenye biblia viongozi wa dini walitabiri anguko la serikali walipokuwa hawawatendei haki wanadamu viumbe wa Mungu. Watawala wa namna ile husababisha laana kwa nchi nzima kama hapa kwetu.

3. Kwa bahati mbaya sana nchi yetu imeshuhudia watawala wasio na hofu ya Mungu wanaodhulumu haki za raia viumbe wa Mungu kwa kukosa hekima na busara, hadi kuua au kujaribu kuua.

i. Bei za mazao kwa wakulima imekuwa kitendawili miaka yote kwenye nchi ya wakulima na wafanyakazi.

ii.Viwanda vimebaki mshangao haijulikani ilitokea nini na ifanyike nini zaidi ya kauli tata za awamu ya viwanda na uchumi wa kati.

iii. Mungu hapendi dhulma, mateso, mauaji na uonevu kwa viumbe wake kama namna tunayoshudia hivi sasa. Ni sawa kwa watumishi wote wa Mungu kuwaonya watawala ndiyo kazi yao ya kwanza.

4. Tupe takwimu za ukusanyaji wa kodi ulioongezeka. Mbona kimya hakuna taarifa?

Hoja yako haishangazi maana mafanikio ya shetani ni kuitia ganzi na upofu roho ya neema ya Mungu na kutoa ufahamu wa viongozi batili wasio na hofu ya Mungu hususan yanayofanywa na mtawala huyu.
 
Bora ziende mazabauni tu maana si asa mpaka 2020 sasa siasa ziende wapi ulitaka
 
MAASKOFU MNAOLETA SIASA MADHABAHUNI KUMBUKENI BUSARA ZA MZEE MAKAMBA.

Najiuliza sana hawa Maaskofu wanaotokwa mapovu kumshambulia Rais Magufuli madhabuhini dhamira yao nini?

Au nao wanataka kupata ubatizo wa moto kama anavyosema Mzee Yusuf Makamba?

Wamegeuza madhabahu kuwa uwanja wa siasa za upinzani kumshambulia Rais. Bahati nzuri wote tunawafahamu kwa historia zao, maana historia ni Mwalimu mzuri.

Juzi kati nimemsikia Askofu wa KKKT Dayosisi ya Karagwe Askofu Benson Bagonza baadaye akafuata Askofu Zakaria Kakobe. Huko nyuma alikuwa Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Rulenge Ngara Askofu Severin Niwemugizi na alitanguliwa na Askofu wa KKKT Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Askofu Steven Munga.

Hawa wote tangu Rais Magufuli aingie madarakani sijawasikia wakitambua juhudi za kupambana na Rushwa na Ufisadi, Sijawasikia wakisema kuhusu kufutwa ada ya wanafunzi shuleni, sijawasikia wakitambua kuongezwa kwa bajeti ya dawa hospitali, sijawasiki wakitambua kununuliwa ndege za serikali kwa ajili ya usafiri wa anga na utalii, sijawasikia kwa chochote juu ya juhudi za kuondoa ubabaishaji katika ofisi za serikali, sijawahi kuwasikia wakisema chochote juu ya kuanza kwa ujenzi wa reli ya kati, sijawasikia wakisema kitu kuhusu uboreshaji wa miundombinu ya barabara, madaraja, vivuko.

Wala sijawahi kuwasikia wakizungumzia ongezeko la makusanyo ya kodi, wala sijawasikia wakieleza namna bandari zinavyoboreshwa, sijawasikia wakitambua namna matumizi ya anasa yalivyopigwa pini, sijawahi kuwasikia wakieleza jinsi Rais anavyosisitiza kufanya kazi.

Hata linalowahusu la Rais kumtaja Mwenyezi Mungu, kumtambua na kuhudhuria Ibada makanisani. Hawajawahi kuunga mkono.

Badala yake nawasikia mapovu yanawatoka wakidai Kupewa haki ya kumkosoa na kumdhalilisha Rais, kumsema na kuwachochea wananchi wamchukie Rais na Serikali. Zaidi nawasikia wakitamba madhabahuni kuwa wao wana pesa na hawababaishwi, wakati tunatambua wanaishi kwa sadaka zinazotolewa na walala hoi kabisa ambao wanakwenda kwenye nyumba zao za ibada ili wasali.

Juzi Askofu Bagonza anamshambulia Rais kwa kumtetea Askofu Kakobe. Eti anadai ni haki kwao kufanya siasa madhabahuni. Ebooo!!! Askofu tunapokuja kanisani tunakuja kusali, hatuji kwenye mkutano wa siasa. Na tunaokuja kanisani tunatoka vyama tofauti, baadhi ni wanachama wa CHADEMA unayoishabikia na wengine ni wanachama wa CCM ambao Mwenyekiti wao ni Rais unayemponda. Askofu unatuvuruga.

Kama unataka kuzungumza mambo ya siasa, madhabahuni sio mahali pake. Na hoja yako kuwa mkifanya masuala ya maji, umeme na hospitali hamsemwi lakini mkimsema Rais mnasemwa sio hoja yenye mashiko. Tofautisha masuala ya maendeleo na masuala ya siasa unazozifanya wewe na huyo Askofu Kakobe. Ni lini Rais ama kiongozi wa siasa umemsikia akiwashambulia viongozi wa dini kwa kazi zenu?

Watanzania tunafahamu kuwa wewe Askofu Bagonza na Askofu Kakobe ni miongoni mwa Majeruhi wa safari ya matumaini. Mlijiingiza kwenye siasa, mkapanda basi la safari ya matumaini na dereva wenu Edward Lowassa akashindwa akaukosa Urais, sasa mmegeuza kuwa hasira ya kumshambulia Rais Magufuli.

Wewe Askofu Bagonza ndiye uliyempa madhabahu Mtuhumiwa wa Ufisadi Edward Lowassa afanye kampeni zenye ubaguzi wa kidini, tukawasikia mkisema sasa zamu yetu Walutheri. Bisha sio wewe?

Wewe Askofu Bagonza ndiye umetoa kauli ya kuwaunga mkono wanasiasa wa upinzani juu ya agizo la Rais Magufuli kutaka Watoto wanaopata mimba wasirudishwe darasani kuchanganywa na watoto ambao sio wazazi. Bisha???

Wewe Askofu Bagonza ndiye uliyeungana na upinzani kupinga kauli ya Rais aliyeweka wazi kuwa Katiba Mpya sio kipaumbele chake, anataka maendeleo aliyowaahidi watanzania kwanza. Tena ukaungana na mwenzako Askofu Munga. Bisha???

Kibaya zaidi tunakufahamu Askofu Bagonza unaunga mkono ndoa za mashoga. Na huu mradi baada ya kugonga mwamba kupitia Serikalini sasa unapenyezwa kupitia viongozi wa upinzani na kupitia kwa viongozi wa dini na wewe Askofu Bagonza tunakujua unatuletea mashoga kila siku kwa kivuli cha kuwa viongozi wa dini ama marafiki wa kanisa lako.

Leo unamuunga mkono Askofu Kakobe ambaye anamshambulia Rais tena bila hata kujali makandokando ya Kanisa lake ambalo lipo kwenye hifadhi ya barabara.

Maana nimeshangaa sana Askofu Kakobe huyu ambaye anajiita mtabiri na hasemi kama ni Mtabiri anayeshindwa kila jambo anamshambulia Rais Magufuli na anataka tumuamini kuwa ni kiongozi wa dini wakati ni mwasiasa kabisa huyu.

2015 Askofu Kakobe alitabiri kuwa mtuhumiwa wa Ufisadi Edward Lowassa atakuwa Rais, akaongea kwa hamasa madhabahuni. Akapigiwa makofi na waumini wake. Hakuishia hapo akaenda kwenye mikutano ya Chadema ya M4C na picha zipo akaendelea kuunga mkono siasa za upinzani na akaendelea kusema Lowassa atakuwa Rais, leo anataka tumuamini kuwa ni kiongozi wa dini tu wakati ni mwanasiasa kabisa huyu.

Huyu Askofu Kakobe tunamjua na sielewi kwa nini mpaka sasa hajakamatwa kwa sababu nina hakika anatuhuma za uhujumu uchumi na utakatishaji wa fedha. Na vyombo vilianza kumchunguza akakimbilia nje ya nchi. Wazee wa kanisa lake walikuwa na mgogoro nae juu ya matumizi mabaya ya fedha za kanisa, wakaburutana hadi kwenye vyombo vya sheria.

Leo anatamba madhabahuni kuwa ana fedha kuliko Serikali? Anaidhalilisha Serikali mchana kweupe eti ana fedha za kuwagawia mawaziri. Mwizi kabisa huyu nae anataka kuiyumbisha nchi kwa fedha za sadaka anazowatapeli wananchi mchana kweupe kwa miujiza yake ya uongo?

Halafu anajifanya mtu wa Mungu na anataka tumuamini.

Nashangaa sana sana. Na navishangaa vyombo vya dola vimekaa kimya dhidi ya mtu huyu maana mimi nilijua tangu amekimbilia nje ya nchi hajarudi. Kumbe karudi na wanaendelea kumuangalia?

Na kwa kweli vyombo vya ukaguzi vizuri viyaangalie haya makanisa. Ikiwezekana kama ambavyo Mkurugenzi wa Habari Maelezo Dk. Hassan Abbas alivyoandikisha upya magazeti na majarida, umefika wakati hata haya makanisa yasajiriwe upya na kuwekwe vigezo vya kanisa kuitwa kanisa. Maana vinginevyo baadhi ya makanisa yatakuwa yanatumiwa kuivuruga nchi na sisi tunayaangalia. Au kama vipi nakuomba Mhe. Rais kama ulivyopiga marufuku mikutano ya hadhara piga marufuku pia mahubiri ya kisiasa kama ya akina Askofu Kakobe, Bagonza, Gwajima na Niwemugizi.

Angalieni pia na taasisi zinazoongozwa na haya makanisa. Maana mimi najua mfano Askofu Munga, Chuo Kikuu cha Sebastian Kolola kipo chini ya KKKT Dayosisi ya Kaskazini Mashariki. Alichokifanya yeye ni Mkuu wa Chuo, Makamu Mkuu wa Chuo ni Mke wake, Mhasibu ni Mtoto wake na Mkwewe nae ana cheo hapo. Ukifuatilia kwa undani utaona wakati anaomba ufadhili wa kujenga chuo hiki na kukiendesha aliomba kwa jina la wananchi, lakini hapa kakifanya mali ya familia.

Yapo mengi ya kuwahoji hawa Maaskofu na uswahiba wao wa siasa. Wasitudanganye na wasituyumbishe.

Hivi kweli hiyo hoja feki ya demokrasia waliyoibeba kutoka upinzani, najiuliza tu hivi kuna watu wabinyaji demokrasia wanaowashinda viongozi wa dini? Maana kwenye dini humu anachosema Askofu hakina mjadala. Ni wapi waumini huwa wanahusishwa kwenye kupanga matumizi ya mapato ya Kanisa?

Ndio maana viongozi hawa wanatamba kuwa wanapesa kuliko Serikali, wengine wanatamba wananunua ndege na treni, wanatembelea magari ya kufahari. Ni fedha za walala hoi wanaotoa sadaka ama unyonge wao unatumika kuomba misaada huko nje. Tusidanganyane.

Sisi watanzania tutaendelea kumuunga mkono Mhe. Rais Magufuli kwa sababu tunatambua anafanya alichoahidi wakati anatuomba kura, ananyoosha nchi iliyokuwa imeoza kwa ufujaji wa fedha za umma na mali za umma, iliyokuwa imetapakaa wizi, ilikuwa haina Mswalia Mtume kwa wanyonge.

Tunakuomba Mhe. Rais wewe chapa kazi, hawa wanaopiga kelele washughulikie bila haya. Kwani ukimkamata Askofu Kakobe kwa madudu yake hata leo nani atahoji? Kwa sababu tunamjua na madudu yake. Funga kanisa lake analotumia kufanya uchochezi, mbona yeye mwenyewe aliwahi kulifunga kwa muda mrefu wakati ana mgogoro wa ndani ya kanisa? Na wengine hivyo hivyo. Tena wengine hata sio raia wa nchi hii. Shughulika nao, ndio kazi tuliyokupa. Ukiwaacha hawa watatuvuruga, maana wengine sasa hatupendi hata kwenda kanisani siasa tu kila mahali.

Halafu Mhe. Rais hivi Lowassa mpaka leo vyombo havimkamati kwa nini? Maana huyu ndio mfadhili wa fujo zote hizi. Na kisa ni kimoja tu, ulivyomchapa kwenye uchaguzi wa Chama mwaka 2015 na baadaye akakimbilia CHADEMA nako ukamchapa. Sasa kaamua kutumia fedha alizoiba serikalini kukuvuruga usifanye kazi kwa amani. Unamuachaje huyu. Mbona akina Rugemalila na yule Singasinga Seth wapo ndani? Kamata huyu, kaiba sana. Ukimweka ndani utaona watu watakavyokuletea ushahidi wa madudu yake akiwa huku nje ni ngumu sana. Anahonga sana huyu Mzee, ana hela nyingi mno. Ndio maana akina Freeman Mbowe hawamuachi wanajia ile ni ATM muda wote inatema hela.

Hata hii Kamati ya kuhakiki mali za CCM katika changamoto itakayokumbana nayo ni nguvu ya Lowassa, maana huko kwenye CCM ndio kaiba mpaka basi. Hata watoto wanajua kuwa ni mwizi licha ya juhudi za CHADEMA kumsafisha.

Haya naishia hapa
Viva Tanzania

*Jackson Masendoke*
*Mkazi wa Ilala, Dsm*
*28 Desemba, 2017*
Punguani mkubwa wewe, tutolee upuuzi wako hapa,jibu hoja za maaskofu kwanza, kamawaliyosema ni uongo au la?
 
Andiko refu kulimaliza nimeshindwa kwa sababu limejaa upumbavu na ujinga mwingi hebu mtoa mada nenda katubu huenda ukarudi kuandika vitu vya maana
 
we una laana huyo lowasa unahangaika nae una Evidence yoyote kwamba ni mwizi Acha kunyoosha mdomo wako kama mademu wa mipasho au wewe ni wa mipasho na udaku!?
 
Huyu jamaa amejiandaa na kuandika maneno meengi unfortunately it is rubbish like human manure!
 
Back
Top Bottom