Waridi
JF-Expert Member
- Mar 30, 2008
- 1,025
- 172
Kutoka gazeti la Mtanzania
[h=2]NCCR- Mageuzi kuandamana Mtwara [/h]Jumamosi, 10 Machi 2012 09:23 Na Mwandishi Wetu, Newala
CHAMA cha NCCR-Mageuzi, kinatarajia kufanya maandamano ya amani Mjini Mtwara ili kuishinikiza Serikali iwajali wakulima wa zao la korosho mkoani Mtwara.
Akizungumza na MTANZANIA Mjini Newala jana, Katibu Mwenezi wa chama hicho, Moses Machali, alisema maandamano hayo yatafanyika kesho kuanzia saa 8 mchana.
Pamoja na suala la zao la korosho, alisema pia maandamano hayo yatafanyika kama sehemu ya kuhitimisha ziara ya wiki moja ya viongozi wakuu wa chama hicho mkoani Mtwara.
Kama unavyojua, Mkoa wa Mtwara una changamoto nyingi na mojawapo ni kuhusu kudorora kwa bei ya zao la korosho ingawa pia zao la karanga nalo halina faida kwa wakulima wa mkoa huu.
Ni ukweli ulio wazi kuwa, Serikali imewasahau kabisa wakulima wa korosho, bei ya korosho iko chini na hata wanapoiuza wanakopwa wakati ikijulikana kuwa kuwakopa ni njia mojawapo ya kudhoofisha maisha yao.
Kwa kuwa tuko katika mkoa huu kuanzia Machi 4, mwaka huu, tunatarajia kuhitimisha ziara yetu kesho Jumapili kwa kufanya maandamano makubwa ya amani Mjini Mtwara ili kuishinikiza Serikali iwajali wakulima wa korosho ambao wengi wao wanaishi maisha ya shida bila sababu za msingi.
Sisi ni wazalendo wa kweli, hatutaki kuona Watanzania wenzetu wakinyanyasika katika nchi yao, hatutaki kuona wakulima wanalima kilimo kisichokuwa na faida, kwa hiyo, tutaitisha maandamano hayo ili kuwaamsha wakulima na wananchi wa Mtwara kwamba CCM si chama chao bali ni chama cha wachache.
Kwa bahati nzuri katika ziara hii yupo Mwenyekiti wetu wa Taifa, James Mbatia, sasa huyo ndiye atakayeongoza maandamano hayo na watakuwapo pia viongozi wengine wa kitaifa waliopo katika ziara yetu hii, alisema Machali ambaye pia ni Mbunge wa Kasulu Mjini.
Kwa mujibu wa Machali, uongozi wa NCCR- Mageuzi, Jimbo la Mtwara Mjini, umeshatoa taarifa kwa Jeshi la Polisi, Wilaya ya Mtwara Mikindani kwa ajili ya kuomba ulinzi wakati wa maandamano hayo.
Polisi wameshapewa taarifa kama ilivyo kawaida, maandamano yataanzia eneo la Mkanaredi Magomeni kupitia mkoani, Bima, Soko Kuu, Chilindima na yataishia katika Uwanja wa Mashujaa uliopo Mtwara Mikindani.
Kwa maana hiyo, tunawoamba wananchi wa Mtwara wajitokeze kwa wingi katika maandamano hayo kwa sababu tutatoa tamko zito kuhusu zao la korosho linaoonekana kuwa kero kwa wananchi ingawa ni muhimu kwao, alisema.
[h=2]NCCR- Mageuzi kuandamana Mtwara [/h]Jumamosi, 10 Machi 2012 09:23 Na Mwandishi Wetu, Newala
CHAMA cha NCCR-Mageuzi, kinatarajia kufanya maandamano ya amani Mjini Mtwara ili kuishinikiza Serikali iwajali wakulima wa zao la korosho mkoani Mtwara.
Akizungumza na MTANZANIA Mjini Newala jana, Katibu Mwenezi wa chama hicho, Moses Machali, alisema maandamano hayo yatafanyika kesho kuanzia saa 8 mchana.
Pamoja na suala la zao la korosho, alisema pia maandamano hayo yatafanyika kama sehemu ya kuhitimisha ziara ya wiki moja ya viongozi wakuu wa chama hicho mkoani Mtwara.
Kama unavyojua, Mkoa wa Mtwara una changamoto nyingi na mojawapo ni kuhusu kudorora kwa bei ya zao la korosho ingawa pia zao la karanga nalo halina faida kwa wakulima wa mkoa huu.
Ni ukweli ulio wazi kuwa, Serikali imewasahau kabisa wakulima wa korosho, bei ya korosho iko chini na hata wanapoiuza wanakopwa wakati ikijulikana kuwa kuwakopa ni njia mojawapo ya kudhoofisha maisha yao.
Kwa kuwa tuko katika mkoa huu kuanzia Machi 4, mwaka huu, tunatarajia kuhitimisha ziara yetu kesho Jumapili kwa kufanya maandamano makubwa ya amani Mjini Mtwara ili kuishinikiza Serikali iwajali wakulima wa korosho ambao wengi wao wanaishi maisha ya shida bila sababu za msingi.
Sisi ni wazalendo wa kweli, hatutaki kuona Watanzania wenzetu wakinyanyasika katika nchi yao, hatutaki kuona wakulima wanalima kilimo kisichokuwa na faida, kwa hiyo, tutaitisha maandamano hayo ili kuwaamsha wakulima na wananchi wa Mtwara kwamba CCM si chama chao bali ni chama cha wachache.
Kwa bahati nzuri katika ziara hii yupo Mwenyekiti wetu wa Taifa, James Mbatia, sasa huyo ndiye atakayeongoza maandamano hayo na watakuwapo pia viongozi wengine wa kitaifa waliopo katika ziara yetu hii, alisema Machali ambaye pia ni Mbunge wa Kasulu Mjini.
Kwa mujibu wa Machali, uongozi wa NCCR- Mageuzi, Jimbo la Mtwara Mjini, umeshatoa taarifa kwa Jeshi la Polisi, Wilaya ya Mtwara Mikindani kwa ajili ya kuomba ulinzi wakati wa maandamano hayo.
Polisi wameshapewa taarifa kama ilivyo kawaida, maandamano yataanzia eneo la Mkanaredi Magomeni kupitia mkoani, Bima, Soko Kuu, Chilindima na yataishia katika Uwanja wa Mashujaa uliopo Mtwara Mikindani.
Kwa maana hiyo, tunawoamba wananchi wa Mtwara wajitokeze kwa wingi katika maandamano hayo kwa sababu tutatoa tamko zito kuhusu zao la korosho linaoonekana kuwa kero kwa wananchi ingawa ni muhimu kwao, alisema.