CARLOS MAJURA
Binafsi naiunga mkono CHADEMA lakini siungi mkono maandamano; hayana tija.
Lazima Watanzania tutafute mbinu mbadala za kudai haki KWA AMANI, na si kwa njia ya maandamano au mikutano mingi ya hadhara, ambapo wananchi wasio na hatia yoyote wanaishia kupigwa, kujeruhiwa, wengi wao kupata vilema, kwa kuwa Jeshi la Polisi limedhihirishwa KWA USHAHIDI USIOPINGIKA kwamba lipo kwa ajili ya CCM na si kwa Watanzania wote!
Halitendi haki na halitatenda haki! Kwa nini tuwapeleke Watanzania hawa "machinjioni"?
CHADEMA ni chombo/chama chenye utajiri mkubwa wa fedha kwa kuwa kinaungwa mkono na wadau wengi ndani na nje ya nchi, hivyo chochote kikitaka kufanya, ufadhili utakuwapo.
Bw. Majura, wewe kama mwanahabari, unaijua vema nguvu ya Media, The Fourth Estate, kwa hiyo unajua vema kwamba CHADEMA ikianzisha na kumiliki vyombo vyake vya habari, kama vile Redio na Luninga, itakuwa na uwezo mkubwa wa kuwafikia wananchi kuliko hata mikutano. Hii ni njia nyepesi na inawezekana.
Ninaufahamu vema umuhimu wa mikutano, kwani Watanzania wamezoea kuwasikiliza viongozi wa vyama kwenye majukwaa ya hadhara, lakini kama tutaweza kuwafikia wananchi hawa kwa njia ya redio na luninga, hebu fikiria tutaweza kuwafikia wananchi wangapi tena kwa gharama nafuu zaidi?
SIUNGI MKONO MAANDAMANO! Watu wataumizwa bure! Halafu wimbo utakuwa ule ule: CHADEMA chama cha vurugu!