Maandamano marufuku Dar es Salaam

Maandamano marufuku Dar es Salaam

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,346
Reaction score
26,138
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Mh. Said Mecky Sadik amepíga marufuku maandamano ndani ya Dar es Salaam katika kipindi cha kampeni. Marufuku hiyo imepokewa na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,Kamanda Suleiman Kova.

Kamanda Kova ametamba kuwa wanao askari wa kutosha na wenye nguvu na ari kwakuwa ndiyo kwanza wametoka Depo. Amewaonya wananchi wasitende kinyume cha Sheria na kusababisha kukamatwa.

Chanzo: ITV Habari
 
UKAWA na wanachama na wapenzi wake watii amri hii endapo CCM wanaitii. Wagombea wawakute watu kwenye eneo la tukio au watu wawakute wagombea pale; na wakati wa kuondoka wagombea baada ya mkutano wa kampeni basi wagombea waondoke kwanza then wananchi.

Nasema hivi ili kuonyesha amri hiyo si kitu chochote.
 
Badala ya kuongelea kipindupindu na kuchukua hatua yeye anahangaika na maandamano, kwamba yanahatarisha usalama. Hivi ni kipi kinachohatarisha usalama wetu zaidi kwa sasa kati ya maandamano na kipindupindu?

Fanyeni kazi.... *by wagosi
 
Kwa hilo naliunga mkono kwani maandamano husitisha shughuli nyingi za ujenzi wa taifa na ni usumbufu mkubwa kwa wasiohusika na hayo maandamano pia husaidia kupunguza madhara ambayo yanaweza kutokea kutokana na hayo maandamano,pia tuache ushabiki hayo maandamano yamepigwa kwa vyama vyote kwani kwa upofu tulionao wengine watadhani wanalengwa wao,haijakatazwa mtu kuenda kwenye shughuli za kampeni lakini nenda kama unavyoenda kuangalia Simba na Yanga,unatoka nyumbani kwako peke yako na kujumuika na wenzako kwenye sehemu ya kukutana,tusiwe na ubinafsi wa kuangalia upande mmoja tu,najua wengine watakuja na jaziba na matusi kama kawaida yao .
 
UKAWA na wanachama na wapenzi wake watii amri hii endapo CCM wanaitii. Wagombea wawakute watu kwenye eneo la tukio au watu wawakute wagombea pale; na wakati wa kuondoka wagombea baada ya mkutano wa kampeni basi wagombea waondoke kwanza then wananchi.

Nasema hivi ili kuonyesha amri hiyo si kitu chochote.

Na wakati wa kuondoka msubiriano ili isionekane mnaandamana mnaondoka kumi kumi kwanza.
 
Na wakati wa kuondoka msubiriano ili isionekane mnaandamana mnaondoka kumi kumi kwanza.

Kwani maandamano maana yake ni nini? Iwe kama kwenye ibda ya misa kanisani kama wewe unajua taratibu za kanisani.
 
Kwani maandamano maana yake ni nini? Iwe kama kwenye ibda ya misa kanisani kama wewe unajua taratibu za kanisani.

Mie nadhani CCM watalitolea ufafanuzi manake binafsi nahisi kuna target fulani juu ya maagizo haya.
 
hahhaahah, marufuku. !!kampeni zitakosaje maandamano?mkuu wa mkoa anajua kibarua kimegusa kitumbua Edo akiingia madarakani
 
Wakiandama na sisi Tutandamana nini depo bwana wasitutishe! wasitutishe! Wasitutishe! Sawasawa
 
Kinachotakiwa kusubiri oktoba na kuonyesha wingi wenu Kwenye sanduku LA Kira sio kuvua mashati na kuandana barabarani kughasi RAIA wengine
 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Mh. Said Mecky Sadik amepíga marufuku maandamano ndani ya Dar es Salaam katika kipindi cha kampeni. Marufuku hiyo imepokewa na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,Kamanda Suleiman Kova.

Kamanda Kova ametamba kuwa wanao askari wa kutosha na wenye nguvu na ari kwakuwa ndiyo kwanza wametoka Depo. Amewaonya wananchi wasitende kinyume cha Sheria na kusababisha kukamatwa.

Chanzo: ITV Habari

Siku wakijua kuwa hata hao askari wanaowategemea hawawezi kupambana na uma watakuwa wamechelewa.
 
Hii itakuwa ni baada ya mbwembwe za Kipindupindu kushindwa!!!!!!
 
Back
Top Bottom