Maandamano makubwa ya CHADEMA kumng'oa Meya wa Ilemela - Agosti 19, 2013

Makala Jr

JF-Expert Member
Aug 25, 2011
3,395
1,110
Ndugu wana JF, bila shaka mtakumbuka kuwa hakuna Meya Tanzania asiyekuwa na chama lakini Meya Henry Matata alitimuliwa uanachama na CHADEMA kwa makosa ya kukihujumu chama kwa maslahi ya CCM na kufuja mali za chama alipokuwa Diwani kupitia CHADEMA lakini halmashauri ya jiji la Mwanza ilipogawanywa; alichaguliwa kwa hila na CCM kupitia madiwani wake katika kikao haramu ambacho siyo tu kwamba akidi haikutimia kutokana na madiwani wa CHADEMA kutokuwepo, bali pia hawakupewa taarifa sahihi kuhusu uchaguzi.

Maandalizi yote ya maandamano kushinikiza Henry Matata yamekamilika, muda huu gari za matangazo zinapita kuwakumbusha wana Ilemela waliokuwa na shauku ya muda mrefu kumtaka achaguliwe Meya halali nje ya kibaraka wa CCM asiyekuwa na malengo na wananchi zaidi ya kulinda ufisadi wa CCM.Maandamano hayo yataongozwa na Mbunge wa Ilemela, Mhe. Highness Kiwia, Mbunge wa Nyamagana Mhe.Ezekiel Wenje, viongozi wa kitaifa wa CHADEMA na madiwani wote wa chama hiki tegemeo la kuleta demokrasia.

=============
 
Ango,olewe tu matata nchi haiwezi kuchezewa namna hiijangiri lenzake Mkurugenzi kabwe anabwia vumbi la Dar pepo ya Mwanza kaisahau kabisa
 
Jee haiwezekani kungolewa kwa kura mpaka maandamano. Hii culture ya maandamano sasa inaleta matatizo mengi, Arusha imetuharibia maisha, biashara zimekufa, watalii wamekimbilia kenya na moshi, Wamachinga wanaharibiwa mitaji yao. Hivyo kweli kama CDM ina numbers hapo ilemela kwanini msitumia nguvu ya kura na kumuondoa. Ikiwa mnashirikisha maandamano inamaanisha ya kuwa ccm ndio wenye numbers , ila CDM inafanya uchochezi.


 
hatuwezi kukubali mahayawani wachache wabake demokrasia na kuchezea sheria halali,lazma ang'olewe huyo meya wa kuchonga
 

Linalowezekana leo lisingoje kesho, nyerere angesema asubiri hadi mkoloni atoe uhuru free bibi ako angekuwepo?
 
tuko pamoja comrade."asante Mungu wana Ilemela tumepata kibali na baraka zote za rpc kama taratibu zingine''
"nikwombe Mungu kesho niamke kama siku zingiiine"
"apatae taarifa hii asisahau kumfahamisha mtu mwingine"
"na umfahamishe yataanzia FRAHISHA kama siku zingine"
"usisahau azimio letu ni saa 3 asb kama maazimio mengine"

"Big up mleta mada kama waanzisha thread wengine"
 

kuandika unajua ila ulichoandika ndo ukijui. omba ueleweshwe, karibu sana mwanza. kesho tupo barabarani mpaka kieleweke.
 
Meya Matata ana haki wakazi wa Kitangiri ndiyo wamemchagua kuwa diwani wao haiwezekani Dr Slaa na Mbowe wamfukuze.

Safi sana Meya endelea kuwatumikia wakazi wa Jiji la Mwanza.

Chadema hamna uwezo wa kumng'oa Meya Matata.
 
Matata kwisha ! Naihurumia sana familia yake kwa aibu iliyosababishwa na baba yao !
 
lazima niwepo kuhakikisha tunamng'oa huyo meya feki,WANG'OLEWE TU MAANA NA CC TUMECHOKA
 
Mkirindi; Soma vizuri thread kabla ya ku comment, box la kura lishahujumiwa tangu siku nyingi. Hawataki kuitisha uchaguzi huru na haki!
 
Last edited by a moderator:
Meya Matata ana haki wakazi wa Kitangiri ndiyo wamemchagua kuwa diwani wao haiwezekani Dr Slaa na Mbowe wamfukuze.

Safi sana Meya endelea kuwatumikia wakazi wa Jiji la Mwanza.

Chadema hamna uwezo wa kumng'oa Meya Matata.

Vitz sisi wana Kitangiri haohao ndo tunamuondoa kwa maandamano!!
 
Meya Matata ana haki wakazi wa Kitangiri ndiyo wamemchagua kuwa diwani wao haiwezekani Dr Slaa na Mbowe wamfukuze.

Safi sana Meya endelea kuwatumikia wakazi wa Jiji la Mwanza.

Chadema hamna uwezo wa kumng'oa Meya Matata.

mbona mnajing'oa ubongo , hivi nani alimchagua matata kuwa meya wa Ilemela ?
 
Ritz; Kwa hiyo unataka kupuuza katiba ya nchi inayotaka kiongozi aliyefukuzwa uanachama pia uongozi wake hukoma? Isitoshe Matata hakuchaguliwa kuwa Meya na wana Kitangiri bali madiwani wa CCM!
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…