Maandamano dhidi ya ubaguzi huko Israel

Maandamano dhidi ya ubaguzi huko Israel

Absolute

JF-Expert Member
Joined
Jan 19, 2007
Posts
333
Reaction score
62
waethiopia waandamana.jpg

Walowezi wanaoishi katika ardhi zilizoghusubiwa za Palestina wamefanya maandamano wakipinga ubaguzi wa rangi na wa kizazi ndani ya utawala wa Kizayuni wa Israel. Ripoti zinasema kuwa maandamano hayo yaliwahusisha zaidi Waethiopia waliohamishiwa katika ardhi za Palestina wakipinga ubaguzi wa rangi na wa kimbari wanaokabiliana nao huko Israel.

Zaidi ya Waethiopia elfu tano walioshiriki katika maandamano hayo mbele ya bunge la Israel wametoa wito wa kufutwa sheria za kibaguzi na kupewa haki sawa za kijamii. Waandamanaji hao walikuwa wakipiga nara za kulaani ubaguzi wa rangi wanaofanyiwa na utawala ghasibu wa Israel kutokana na rangi ya ngozi yao. Waandamanaji wa Kiethiopia pia walikusanyika mbele ya nyumba ya Waziri Mkuu wa Israel Benjamini Netanyahu na kutoa maneno yanayolaani siasa za kibaguzi za Israel.

SOURCE: Maandamano dhidi ya ubaguzi huko Israel
 
Hawawezi kuona kwamba hawapendwi wala hawatakikani warudi kwao Ethiopia. Ukienda kwa mtu ukaona amezidi kukunyanyasa wakati una kwenu ni vizuri ukaamua kuondoka badala ya kulalamika.

Au waendelee kung'ang'ania siku Israel ikiingia vitani wawekwe mstari wa mbele kuuwawa.
 
Wana haki ya kulalamika jamani kwa sasa vitendo vya ubaguzi havina nafasi tena ni vya kupigwa vita haswa.
 
Back
Top Bottom