Maamuzi magumu vs Utapeli wa CCM

whizkid

JF-Expert Member
Aug 2, 2010
357
240
maamuzi.jpg

Pua ndefu kama Pinocchio ni ishara ya uongo uliopindukia. Tumeshuhudia mambo mengi ya kisanii yakiendelea hasa katika ulingo wa siasa za Chama Cha Mapua-ndizi. Yameongelewa mengi na viongozi wa chama hicho kishika dola, mikutano ikafanyika mpaka ikafikia hatua ya chama kujivua magamba yake ya kijani. Green mamba wa kibisa?

Leo hii, ni dhahiri kwamba magamba yaliyoongelewa si yaliyovuliwa. Maamuzi "magumu" yaliyotolewa kwenye vikao yameshindikana kufanyiwa kazi. Najiuliza. Nahoji. Serikali inayoshikiliwa na chama kinachoendeshwa na viongozi waliojifananisha na nyoka na kuajiri panya wa majaribio (Nape na vijana wake), inaposhindwa kuyafanyia kazi maamuzi yoyote "magumu" ya kutatua matatizo ya chama chake, itaweza vipi kufanya maamuzi magumu kulinusuru Taifa letu? Huu sio utapeli wa kisiasa? Wanachama na wakereketwa hili hawalioni kama linakereketa?

Tunaongelea kila siku jinsi Rais wa nchi asivyoijali nchi na watu wake, Rais ambaye amewekwa na nyoka wanaokimbizana na panya kwenye mifereji ya siasa zisizokuwa na tija kwa Taifa bali kwa wakamata nyoka (Mafisadi). Rais ambaye hajui kwanini wananchi wake ni maskini, na anashangaa tu kisha anapanda ndege na kwenda kusalimia au kutafuta familia na/au marafiki zake nje ya nchi! Kiongozi kama huyu ambaye inaonekana wazi kuwa hasomi hata mikataba na majalada yanayomfunga (na kututesa wananchi), ana uwezo gani wa kutoa maamuzi "magumu"?

Unapotumia akili zako za kawaida (common sense), ukiwa kama Mtanzania na unatambua jinsi maisha yako ya kila siku yanavyoathiriwa na kuporwa na utapeli wa watu wachache, upo tayari kuendelea kutumika kama panya wa majaribio katika banda la nyoka? Kwanini tunaendekeza ushabiki badala ya kudai haki zetu za msingi?

Wakati unajiandaa kuchangia hoja, tafakari tena picha hiyo hapo juu. Hebu waangalie na hawa jamaa hapa chini:

mafisadi.jpg
 
Sijaelewa Vizuri Hoja yako. Ingawaje Ni kweli Wame hakikishia Taifa Kuwa Utekelezaji wa Maamuzi (mimi siiti Magumu kwasababu ndio Maamuzi yaliyo hitajika) Imeshindikana.

LAbda mtoa Mada na wachangiaji watakaofuata,

1. Je....Utekelezaji wa haya Maamuzi ungekuwa vipi labda? Kuwafukuza hawa wanachama kwenye chama....hapa na swali kidogo ( Je, hawa
wandugu kwa madhambi yao wanatekeleza Ilani ya nani? yao Binafsi au na wengine walioko kimya!!!!!! wao ni baadhi tu wanaowajua ilhali
wengine wapo ila hawajadhihirika?,

2. Je, nikweli walilijua hili kuwa halitekelezeki kabla hawaja anzisha harakati VUA GAMBA?,

3. Inawezekana kuwa ni maigizo haya, to win Public?,

4. Je inatubidi kuangalie Upya tatizo ninini na vipi linatatulika?


Naomba Msaada.....
 
What goes around comes around,yana mwisho na mwisho wa udhalimu ni aibu,sura nzuri bonge ya smile lakini siku ikifika smile hiyo itakuwa ni kilio na tayari wengine wamesha poteza sura za mvuto.

Pata picha zao za leo leo uone muonekano wao,ni balaa kwa kuwa hakuna usingizi,usingizi wa magutu magutu, kustukiza ukumawazo kibao kutojua kesho itakuaje.

Wenzetu wanamsemo unasema time will tell!!!!!!!!!!!.Believe me muda ukifika maandishi yatasomeka kwenye ukauta.
 
maamuzi.jpg

Pua ndefu kama Pinocchio ni ishara ya uongo uliopindukia. Tumeshuhudia mambo mengi ya kisanii yakiendelea hasa katika ulingo wa siasa za Chama Cha Mapua-ndizi. Yameongelewa mengi na viongozi wa chama hicho kishika dola, mikutano ikafanyika mpaka ikafikia hatua ya chama kujivua magamba yake ya kijani. Green mamba wa kibisa?

Leo hii, ni dhahiri kwamba magamba yaliyoongelewa si yaliyovuliwa. Maamuzi "magumu" yaliyotolewa kwenye vikao yameshindikana kufanyiwa kazi. Najiuliza. Nahoji. Serikali inayoshikiliwa na chama kinachoendeshwa na viongozi waliojifananisha na nyoka na kuajiri panya wa majaribio (Nape na vijana wake), inaposhindwa kuyafanyia kazi maamuzi yoyote "magumu" ya kutatua matatizo ya chama chake, itaweza vipi kufanya maamuzi magumu kulinusuru Taifa letu? Huu sio utapeli wa kisiasa? Wanachama na wakereketwa hili hawalioni kama linakereketa?

Tunaongelea kila siku jinsi Rais wa nchi asivyoijali nchi na watu wake, Rais ambaye amewekwa na nyoka wanaokimbizana na panya kwenye mifereji ya siasa zisizokuwa na tija kwa Taifa bali kwa wakamata nyoka (Mafisadi). Rais ambaye hajui kwanini wananchi wake ni maskini, na anashangaa tu kisha anapanda ndege na kwenda kusalimia au kutafuta familia na/au marafiki zake nje ya nchi! Kiongozi kama huyu ambaye inaonekana wazi kuwa hasomi hata mikataba na majalada yanayomfunga (na kututesa wananchi), ana uwezo gani wa kutoa maamuzi "magumu"?

Unapotumia akili zako za kawaida (common sense), ukiwa kama Mtanzania na unatambua jinsi maisha yako ya kila siku yanavyoathiriwa na kuporwa na utapeli wa watu wachache, upo tayari kuendelea kutumika kama panya wa majaribio katika banda la nyoka? Kwanini tunaendekeza ushabiki badala ya kudai haki zetu za msingi?

Wakati unajiandaa kuchangia hoja, tafakari tena picha hiyo hapo juu. Hebu waangalie na hawa jamaa hapa chini:

mafisadi.jpg
Msiogope hii ni dalili tosha ya utawala uliofitinika. uwezo wa kufikiri na kuchambua hushuka ghafla, hawaoni hatari iliyo mbele yao tena ili wasije wakapona.
Maandishi tayari yako ukutani kwenye utawala wa CC magamba na Jaa la Kaya . MENE MENE TEKELI NA PERESI.
 
maamuzi.jpg

Pua ndefu kama Pinocchio ni ishara ya uongo uliopindukia. Tumeshuhudia mambo mengi ya kisanii yakiendelea hasa katika ulingo wa siasa za Chama Cha Mapua-ndizi. Yameongelewa mengi na viongozi wa chama hicho kishika dola, mikutano ikafanyika mpaka ikafikia hatua ya chama kujivua magamba yake ya kijani. Green mamba wa kibisa?

Leo hii, ni dhahiri kwamba magamba yaliyoongelewa si yaliyovuliwa. Maamuzi "magumu" yaliyotolewa kwenye vikao yameshindikana kufanyiwa kazi. Najiuliza. Nahoji. Serikali inayoshikiliwa na chama kinachoendeshwa na viongozi waliojifananisha na nyoka na kuajiri panya wa majaribio (Nape na vijana wake), inaposhindwa kuyafanyia kazi maamuzi yoyote "magumu" ya kutatua matatizo ya chama chake, itaweza vipi kufanya maamuzi magumu kulinusuru Taifa letu? Huu sio utapeli wa kisiasa? Wanachama na wakereketwa hili hawalioni kama linakereketa?

Tunaongelea kila siku jinsi Rais wa nchi asivyoijali nchi na watu wake, Rais ambaye amewekwa na nyoka wanaokimbizana na panya kwenye mifereji ya siasa zisizokuwa na tija kwa Taifa bali kwa wakamata nyoka (Mafisadi). Rais ambaye hajui kwanini wananchi wake ni maskini, na anashangaa tu kisha anapanda ndege na kwenda kusalimia au kutafuta familia na/au marafiki zake nje ya nchi! Kiongozi kama huyu ambaye inaonekana wazi kuwa hasomi hata mikataba na majalada yanayomfunga (na kututesa wananchi), ana uwezo gani wa kutoa maamuzi "magumu"?

Unapotumia akili zako za kawaida (common sense), ukiwa kama Mtanzania na unatambua jinsi maisha yako ya kila siku yanavyoathiriwa na kuporwa na utapeli wa watu wachache, upo tayari kuendelea kutumika kama panya wa majaribio katika banda la nyoka? Kwanini tunaendekeza ushabiki badala ya kudai haki zetu za msingi?

Wakati unajiandaa kuchangia hoja, tafakari tena picha hiyo hapo juu. Hebu waangalie na hawa jamaa hapa chini:

mafisadi.jpg
what is your point? au kutuwekea picha? sisi sio chekechea. after all hujui ukiandikacho.
 
what is your point? au kutuwekea picha? sisi sio chekechea. after all hujui ukiandikacho.

Is it too hard to understand or you simply failed to read between the lines? And you can't even see how the pictures relate? I am not going to rephrase anything. Read again.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom