Parata
JF-Expert Member
- Jul 26, 2011
- 3,090
- 675
Tanzania inajulikana ulimwenguni kote kwamba ni nchi ya maajabu. Ndio maana watu kutoka pande zote za dunia husafiri umbali mrefu na kutumia fedha nyingi ili kuja kujionea maajabu mengi yaliyosheheni nchini. Maajabu hayo ni pamoja na mbuga na hifadhi kubwa zenye wanyama wengi ambao hawapatikani mahali pengine popote duniani, milima mingi na mabonde ya kushangaza ikiwa ni pamoja na mlima Kilimanjaro ambao pamoja na kuwa karibu sana na ikweta huwa na theluji mwaka mzima.
Ipo pia mito mirefu yenye maji matamu, na maziwa makubwa yanayo izunguka Tanzania na kuifanya ionekane kama mwanamwali anaelindwa na majemedari wa vita. Ndege, samaki, nyoka na viumbe vingine vya ajabu vyote vimeweka makazi yake nchini Tanzania kana kwamba ndio nchi pekee yenye rutuba.
Tanzania imejaliwa pia kuwa na vito vya thamani ikiwa ni pamoja na almasi, dhahabu, yaspi, yakuti, yakuti manjano, yaspi na zabarajadi. Vyote hivyo vimelundikana katika ardhi kubwa ya nchi hii kiasi cha kuwafanya wataalam washindwe kujua waanzie wapi kuvichimba.
Si hivyo tu, tanzania imejaliwa pia kuwa na mfumo wa siasa na uchumi wa ajabu kuliko nchi nyingine yoyote duniani. Mfumo unaotoa mwanya kwa wageni kuwa mamilionea kwa rasilimali za watanzania huku wazawa wakiendelea kuwa masikini katika nchi yao; na huku serikali yao ikiendelea kuwa ombaomba siku baada ya siku.Si ajabu kwamba nchi hii ya ajabu inaongoza kwa kuwa na viongozi wa ajabu walio tayari kufanya lolote ili kulinda maslahi yao binafsi, lakini wasio tayari kufanya jambo lolote la maana ili kuinua maisha ya wananchi wao, na kuwafanya wapate japo milo mitatu ya uhakika kwa siku.
Zaidi ya yote Tanzania imebarikiwa mno kuwa na raia wa ajabu, wasiojua kulalamika wala kupiga kelele wanapo onewa, au kudhulumiwa mali yao. Ni raia wa ajabu sana, wepesi kulaghaiwa kwa maneno matupu na walio tayari kuuza KURA yao kwa sahani ya pilau, fulana za rangirangi, doti za kanga na hata kwa burudani nzuri tu za wakata viuno na waimba taarab. Ni watu wa ajabu mno ambao hufurahi na kupiga makofi hata pale wanapoambiwa "kila mtu abebe msalaba wake mwenyewe..." Nchi nzuri sana hii.
Acha wazungu walipe mamilioni ya dola kuja kutuona maana kwa kuambiwa hawawezi kuamini. Wakati wenzetu walioendelea walianzia chini na kujikokota taratibu kuelekea juu hadi kufikia mahali walipo leo hii, sisi tumeanzia juu na kujivurumisha kuelekea chini kwa kasi ya fataki. Wakati wenzetu walianza na usafiri wa punda,(miaka 3,500 iliyopita) baadae wakaunda merikebu, magari ya stima, aeroplane, na sasa wanaenda kwenye mwezi na sayari ya Mars; sie tumeanzia kwenye mabasi ya icalus (UDA) tukaja kwenye DCM, chai maharage, vipanya, bajaji na sasa bodaboda. Bila shaka tunaelekea kwenye punda...Ndio! lazima tutoe mfano wa kutunza mazingira maana magari yanaongeza uharibifu wa ozone.
Acha wazungu wamiminike kuja kuona maajabu yetu. we uliona wapi ambulance za pikipiki? unampakia mama mjamzito kwenye ambulance ya pikipiki akifikia muda wa kujifungua wakati hajafikishwa hospitali inakuwaje? Acha hiyo, mgonjwa akizidiwa wakati safari inaendelea, huyo muuguzi (nurse) anamuhudumia vipi? Na mvua ikinyesha je! nani atakae mshikia mgonjwa mwamvuli ili asilowane? Halafu cha kushangaza ghalama ya ambulance hizo inakaribiana kabisa na gari aina ya Toyota Hiace ambayo inaweza kufanyiwa ukarabati kidogo kuwa ambulance bora zaidi.
Hata kama ni msaada wa bure MIMI ningeukataa. Mwalimu Nyerere aliwahi kusema kwamba "mtu akikupa ushauri wa kipumbavu, nawe ukaukubali ushauri huo huku ukijua kuwa ni ushauri wa kipumbavu...mtu huyo anakudharau. Hivi kwa nini hatukuchukui sehemu ya posho za wabunge tukanunulia ambulance za kweli?
Sishangai Kenya wanapoongoza duniani kwa kuuza vinyago vya mpingo wakati mti huo haumei kwao, wanauza tanzanites kwa wingi wakati mashimo yako Tanzania tu, wanasambaza kahawa na chai ya Tanzania wakati mazao hayo yanalimwa nchini mwetu. Hainishangazi kuona kwamba wageni wengi wanajua mlima Kilimanjaro uko Kenya, maana wenzetu walishauhodhi siku nyingi wakati sie tunacheza dogoli. Na sasa wanataka kujenga uwanja wa ndege Taveta, hivi KIA itapata mtu kweli?
Sioni ajabu kwamba tumeamua kugawa shahada za udaktari kwa kila mtu bure, maana hakuna haja ya kwenda shule! Kwanza nani kasema mtu akisoma ndio anaelimika au kuwa kiongozi mzuri? Shauri yao akina Salim Ahmed salim walioupata udaktari kwa kuutolea jasho. Kizazi chetu sie ukipata udiwani na udaktari huo unakufata nyuma. Labda usiutake.
Hapa nilipo nasubiria 'ankal' issa michuzi apewe udaktari wake. Ndio, nani asiyejua kuwa blog yake ina mafanikio kuliko blog nyingine yoyote? Kwa nini asipewe udaktari wa kublog? kwani tumewapa wangapi? Tumejidai kuwakataza kina Profesa Vulata, Maji Marefu na Dr Remmy wasijiite maprofesa eti wanaharibu sifa na heshima ya wadhifa huo kumbe na sie tunautamani...ajabu sana, tena ya Mwajabu kuolewa na Rajabu.
Namuomba sana Mungu anipe uhai na kuendelea kulilinda Taifa hili la ajabu na hasa tunapoelekea uchaguzi ujao. Nina hakika huo utakuwa uchaguzi wa AJABU sana.
Ipo pia mito mirefu yenye maji matamu, na maziwa makubwa yanayo izunguka Tanzania na kuifanya ionekane kama mwanamwali anaelindwa na majemedari wa vita. Ndege, samaki, nyoka na viumbe vingine vya ajabu vyote vimeweka makazi yake nchini Tanzania kana kwamba ndio nchi pekee yenye rutuba.
Tanzania imejaliwa pia kuwa na vito vya thamani ikiwa ni pamoja na almasi, dhahabu, yaspi, yakuti, yakuti manjano, yaspi na zabarajadi. Vyote hivyo vimelundikana katika ardhi kubwa ya nchi hii kiasi cha kuwafanya wataalam washindwe kujua waanzie wapi kuvichimba.
Si hivyo tu, tanzania imejaliwa pia kuwa na mfumo wa siasa na uchumi wa ajabu kuliko nchi nyingine yoyote duniani. Mfumo unaotoa mwanya kwa wageni kuwa mamilionea kwa rasilimali za watanzania huku wazawa wakiendelea kuwa masikini katika nchi yao; na huku serikali yao ikiendelea kuwa ombaomba siku baada ya siku.Si ajabu kwamba nchi hii ya ajabu inaongoza kwa kuwa na viongozi wa ajabu walio tayari kufanya lolote ili kulinda maslahi yao binafsi, lakini wasio tayari kufanya jambo lolote la maana ili kuinua maisha ya wananchi wao, na kuwafanya wapate japo milo mitatu ya uhakika kwa siku.
Zaidi ya yote Tanzania imebarikiwa mno kuwa na raia wa ajabu, wasiojua kulalamika wala kupiga kelele wanapo onewa, au kudhulumiwa mali yao. Ni raia wa ajabu sana, wepesi kulaghaiwa kwa maneno matupu na walio tayari kuuza KURA yao kwa sahani ya pilau, fulana za rangirangi, doti za kanga na hata kwa burudani nzuri tu za wakata viuno na waimba taarab. Ni watu wa ajabu mno ambao hufurahi na kupiga makofi hata pale wanapoambiwa "kila mtu abebe msalaba wake mwenyewe..." Nchi nzuri sana hii.
Acha wazungu walipe mamilioni ya dola kuja kutuona maana kwa kuambiwa hawawezi kuamini. Wakati wenzetu walioendelea walianzia chini na kujikokota taratibu kuelekea juu hadi kufikia mahali walipo leo hii, sisi tumeanzia juu na kujivurumisha kuelekea chini kwa kasi ya fataki. Wakati wenzetu walianza na usafiri wa punda,(miaka 3,500 iliyopita) baadae wakaunda merikebu, magari ya stima, aeroplane, na sasa wanaenda kwenye mwezi na sayari ya Mars; sie tumeanzia kwenye mabasi ya icalus (UDA) tukaja kwenye DCM, chai maharage, vipanya, bajaji na sasa bodaboda. Bila shaka tunaelekea kwenye punda...Ndio! lazima tutoe mfano wa kutunza mazingira maana magari yanaongeza uharibifu wa ozone.
Acha wazungu wamiminike kuja kuona maajabu yetu. we uliona wapi ambulance za pikipiki? unampakia mama mjamzito kwenye ambulance ya pikipiki akifikia muda wa kujifungua wakati hajafikishwa hospitali inakuwaje? Acha hiyo, mgonjwa akizidiwa wakati safari inaendelea, huyo muuguzi (nurse) anamuhudumia vipi? Na mvua ikinyesha je! nani atakae mshikia mgonjwa mwamvuli ili asilowane? Halafu cha kushangaza ghalama ya ambulance hizo inakaribiana kabisa na gari aina ya Toyota Hiace ambayo inaweza kufanyiwa ukarabati kidogo kuwa ambulance bora zaidi.
Hata kama ni msaada wa bure MIMI ningeukataa. Mwalimu Nyerere aliwahi kusema kwamba "mtu akikupa ushauri wa kipumbavu, nawe ukaukubali ushauri huo huku ukijua kuwa ni ushauri wa kipumbavu...mtu huyo anakudharau. Hivi kwa nini hatukuchukui sehemu ya posho za wabunge tukanunulia ambulance za kweli?
Sishangai Kenya wanapoongoza duniani kwa kuuza vinyago vya mpingo wakati mti huo haumei kwao, wanauza tanzanites kwa wingi wakati mashimo yako Tanzania tu, wanasambaza kahawa na chai ya Tanzania wakati mazao hayo yanalimwa nchini mwetu. Hainishangazi kuona kwamba wageni wengi wanajua mlima Kilimanjaro uko Kenya, maana wenzetu walishauhodhi siku nyingi wakati sie tunacheza dogoli. Na sasa wanataka kujenga uwanja wa ndege Taveta, hivi KIA itapata mtu kweli?
Sioni ajabu kwamba tumeamua kugawa shahada za udaktari kwa kila mtu bure, maana hakuna haja ya kwenda shule! Kwanza nani kasema mtu akisoma ndio anaelimika au kuwa kiongozi mzuri? Shauri yao akina Salim Ahmed salim walioupata udaktari kwa kuutolea jasho. Kizazi chetu sie ukipata udiwani na udaktari huo unakufata nyuma. Labda usiutake.
Hapa nilipo nasubiria 'ankal' issa michuzi apewe udaktari wake. Ndio, nani asiyejua kuwa blog yake ina mafanikio kuliko blog nyingine yoyote? Kwa nini asipewe udaktari wa kublog? kwani tumewapa wangapi? Tumejidai kuwakataza kina Profesa Vulata, Maji Marefu na Dr Remmy wasijiite maprofesa eti wanaharibu sifa na heshima ya wadhifa huo kumbe na sie tunautamani...ajabu sana, tena ya Mwajabu kuolewa na Rajabu.
Namuomba sana Mungu anipe uhai na kuendelea kulilinda Taifa hili la ajabu na hasa tunapoelekea uchaguzi ujao. Nina hakika huo utakuwa uchaguzi wa AJABU sana.