Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,241
- 33,002
Sunday, July 05, 2009 11:43 PM
Mwanaume mmoja nchini China ambaye alizaliwa akiwa na uume mwingine wa ziada ameukata uume wake mmoja baada ya mpenzi wake kumwambia achague moja, aukate uume wake mmoja wa huo wa ziada au wavunje uhusiano wao. Ang Qiang mkazi wa mji wa Guangzhou nchini China alizaliwa akiwa na uume mmoja wa ziada lakini baada ya mpenzi wake kuchukizwa na hali yake hiyo na kutishia kumkimbia, Qiang aliamua kuukata uume mmoja.
"Wakati tulipoanza uhusiano wetu, mpenzi wangu alishtushwa na hali yangu lakini baada ya muda alianza kuogopa" alisema Qiang.
Mpenzi wake alimwambia kuwa aidha aukate uume wake mmoja wa ziada au itabidi wauvunje uhusiano wao kwani hawezi kuendelea naye akiwa katika hali hiyo.
Qiang mwenye umri wa miaka 23 aliamua kuukata uume wake wa ziada ili kulinda mapenzi yake na mpenzi wake.
Qiang anaamini kuwa kwa kuuondoa uume wa ziada aliokuwa nao atakuwa amemridhisha mpenzi wake na mapenzi yao yataendelea vizuri kama awali.
Hali aliyo nayo Qiang inajulikana kitaalamu kama "Diphallus" na humtokea mwanaume mmoja kati ya wanaume milioni 5.5.
Nchini Italia mfanyabiashara mmoja marufu wa nchini humo ambaye naye alizaliwa akiwa katika hali kama hiyo na yeye aliukata uume wake wa ziada.
http://www.nifahamishe.com/NewsDetails.aspx?NewsID=2403254&&Cat=7
Last edited by a moderator: