Habari wakuu,
Niko hapa Dodoma katika uwanja wa Barafu ambapo mkutano wa Operesheni Pamoja Daima umeshaanza.Hivi sasa ni viongozi wa ngazi wa ngazi za kata,wilaya na mkoa ndio wanaongea na kutupa matumaini kuwa viomgozi wa kitaifa watatua muda si mrefu.
Hata hivyo,mpaka muda huu saa 11:20 viongozi wanaosubiriwa kufika kwa "chopa" hawajafika na muda ndio unakwisha.Hakika hili ni kosa kwani wananchi wanasubiri kwa hamu viongozi hao wafike.
Hata hivyo,tunambiwa mafuta ya "chopa" yalicheleweshwa kwa dakika 15.Tunavuta subira.Uzuri hali ya hewa ni nzuri na watu wametulia wakisubiri viongozi wafike.
Makamanda wanaosubiriwa ni mh.Lissu na kamanda Heche.
Update:Muda huu ikiwa ni saa 11: 28 "chopa" ndio inazunguka angani ikitaka kutua.Watu wanashangila.
Jamani watu ni wengi sans na inatia moyo kwakweli.